Monday 31 October 2011

SWALI TOKA MWANANCHI

Wanyamapori wetu wataendelea kusafirishwa nje mpaka lini?

GAZETI hili katika ukurasa wake wa kwanza, limechapisha habari inayoeleza uovu wa baadhi ya wafanyabiashara kusafirisha nje ya nchi kinyemela wanyamapori hai kutoka Hifadhi ya Wanyamapori ya Saunyi wilayani Kilindi.

Habari hiyo inaeleza kuwa wanyama hao wamekuwa wakiwindwa na kukamatwa kwa njia ya wizi kisha kusafirishwa kwa magari wakiwa hai, wakisaidiwa na baadhi ya maofisa wa wanyamapori wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Tayari vitendo hivyo vimewashtua baadhi ya viongozi wilayani humo akiwamo Mbunge wa Wilaya hiyo, Beatrice Shelukindo ambaye amelalamikia kuwa vitendo hivyo vinafanywa na maofisa wanyamapori wasiokuwa na uzalendo na nchi yao.

Katika Kikao cha Madiwani wa Wilaya ya Kilindi kilichofanyika juzi, suala hili pia lilibuka na Diwani wa Kata ya Saunyi, Michael Lesindiyo Yeiyoo, alisema ni jambo la kusikitisha kuona kuwa wanyamapori mbalimbali waliokuwa katika Mbuga ya Saunyi, hivi sasa wapo hatarini kutoweka kutokana na kasi ya uwindaji wa kijangili na kusafirishwa nje ya nchi.

Diwani huyo, alisema jambo la kushangaza ni kuwa wawindaji wanapohojiwa na walinzi wa vijiji vya Kata ya Saunyi wamekuwa wakidai kwamba wanavyo vibali vilivyotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii ambavyo vinawaruhusu kuwinda mnyama yeyote bila kubughudhiwa na mtu wa ngazi ya wilaya, kata na hata kijiji.

Kashfa hii inakuja wakati Agosti mwaka huu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipiga marufuku biashara ya kukamata na kusafirisha wanyamapori kwenda nje ya nchi.

Pinda alisema eneo la wanyamapori utaratibu, usimamizi na hata namna biashara yenyewe inavyofanyika, linahitaji kutazamwa upya.

Katika Bunge hilo la Bajeti, serikali ilitangaza kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Wanyamapori nchini, Obed Mbangwa na watumishi wengine wawili wa Wizara ya Maliasili na Utalii ili kuruhusu kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za kutoroshwa kwa wanyamapori 116 na ndege 16 kwenda nje ya nchi.

Wanyamapori hao wanadaiwa walikamatwa katika hifadhi za taifa na kutoroshewa nje ya nchi Novemba 26 mwaka 2010 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Tunachukua nafasi hii kulaani vikali vitendo vya wanyamapori kusafirishwa nje ya nchi wakati tayari serikali ilishapiga marufuku.

Tunaamini kuwa wanaofanya mchezo huu ni watu wanaofahamika na maofisa wa wanyamapori na pengine ni viongozi wa juu serikalini.

Ni wazi kutokana na tukio hili la Kilindi, Wizara ya Maliasili na Utalii, inatakiwa kufanya mabadiliko makubwa ikiwamo kuwaondoa haraka maofisa wake wa wanyamapori wasiokuwa waaminifu.

Inaonyesha kwamba Idara ya Wanyamapori haina tena uwezo wa kulinda wanyamapori dhidi ya majangili. Tunayo mifano hai ni hivi karibuni tulishuhudia faru walioingizwa nchini kutoka Afrika Kusini mmoja aliuawa wakati Rais Jakaya Kikwete alishaagiza wapewe ulinzi wa kutosha.

Tunahoji, Waziri wa Maliasili na utalii na timu yake ya watumishi wako wapi katika kuhakikisha kuwa wanazui mchezo huu mchafu


Thursday 27 October 2011

CONFIRMED AMANI TO PERFOM LIVE IN STOCKHOLM 29th OCT 2011 DNT MISS

WEMA,WOLPER NA DIAMOND TENA




 MADUU wa Kiwanda cha Filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu na Jacqueline Wolper Massawe, wapo kwenye vita nzito, chanzo kikiwa ni penzi la mwana Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.

Wema na Wolper kwa sasa ni afadhali ya paka na panya, wanapakana mbovu, ‘wanavuana nguo’ mbele ya jamii na kila mmoja ‘amemtangazia njaa’ mwenzake.

Amani linamiliki data za uhakika kuwa kutokana na ‘bifu’ la mastaa hao, tayari makundi mawili yameshaibuka, moja likimpa kampani Wema, lingine lipo ‘beneti’ na Wolper.

Upande wa Wema, mashosti wake wakubwa ni Kajala Masanja na Elizabeth Michael ‘Lulu’, wakati kwa Wolper, shoga yake mkubwa ni Christine Manongi ‘Sintah’.

Sistaduu anayevutia zaidi kwenye muvi, Aunt Ezekiel ‘Gwantwa’ inadaiwa yupo kotekote na anapigwa dongo kwamba ni msaliti (snitch).

AMANI LIMEJUAJE?
Ijumaa iliyopita (Oktoba 21, mwaka huu), gazeti dada la hili, Ijumaa, toleo namba 745, liliandika habari ya Wema na Diamond kumwagana.

Baada ya Wolper kunasa habari hiyo, alichukua kipande cha gazeti hilo na kukitundika kwenye safu yake ya mtandao wa ujumbe wa simu aina ya Blackberry (Blackberry Messenger, BBM).
Pamoja na kipande hicho cha gazeti, Wolper aliandika: “Yamekwisha.”

Wolper anadaiwa kuendelea kuchombeza maneno: “Kuachwa kubaya.”
Baadaye Wema alijibu mapigo kupitia anuani yake ya BBM kwa kuandika: “True love never die (penzi la kweli halifi).”
Wema aliendelea kushusha madongo: “Mimi na Diamond tunapendana, ananipenda sana, hatuwezi kuachana. Wewe ndiyo unakimbiwa na wanaume.”

Kwa upande mwingine, Wolper baada ya habari kwamba Wema na Diamond wametosana, alimuandikia SMS ‘bwa mdogo’ huyo anayebamba ‘kitaa’ kwa ‘songi’ lake la Moyo Wangu. Ujumbe ulisomeka: “Hi baby.”
Diamond alijibu: “Usiniite baby, mke wangu hapendi.”

Baada ya hapo, mazungumzo kati ya mwana Bongo Fleva huyo na Wolper yaliendelea hivi;
Wolper: Kama mkeo hapendi, mimi nina nafasi yangu na yeye anayo ya kwake.
Diamond: Wewe una nafasi gani kwangu?

Wolper: Unajua mwenyewe nafasi yangu kwako.
Inadaiwa kuwa Diamond alimuonesha Wema SMS za Wolper, hivyo kuzidi kumtibua.

BBM TENA!
Baada ya Wema kuona Wolper anamsakama, alirejesha mashambulizi yake kwa njia ya BBM.
Kwa kuanzia, Wema aliponda picha za Wolper alizopiga akiwa amenyoa nywele na kuweka rangi nyeupe mithili ya Amber Rose.

Katika picha hizo, Wolper aliandika Amber Rose bila kuongeza neno lolote.
Wema alimponda Wolper kwa kuandika kwamba si Amber Rose kisha aliponda: “Amber Rose Bongo?”
Wolper alijibu mapigo, akachukua picha ya Wema (mbaya), akaiweka mtandaoni, kisha akaandika: “Basi huyu ndiye Amber Rose. Ila nimeipenda sana hii picha.”

Kwa shambulio hilo, Wema alikuja juu na kumchana Wolper kuwa hana ujanja wowote kwa sababu ni mgeni mjini na kwamba tangu ameingia Dar, hana hata Krismasi tatu.
Wolper naye akamvua Wema kuwa ni supastaa ambaye hana hata kitanda kisha akapiga picha pea za viatu vyake na kuahidi kuviuza ili amnunulie ‘cha kulalia’.

MAKUNDI
Kutokana na bifu hilo, Kajala na Lulu wamekuwa wakimsapoti Wema kumchakaza Wolper kwa kuandika au kuchangia ujumbe wenye sura ya kumchana.

Amani lilipozungumza na Kajala kuhusu hilo, alisema Wolper ni mchokozi kwa sababu anaingilia uhusiano wa Wema na Diamond.

Aliendelea: “Asili ya Wolper ni mchokozi. Namsaka, nikimkamata atanitambua.”
Wolper alipoulizwa alijibu: “Mimi sijui chochote, nakumbuka picha zangu ndiyo watu walichangia wakiniita Amber Rose.”

Sintah yeye alipozungumza na Amani alisema: “Wale wote ni marafiki zangu, hizi bifu nafikiri kuna ajenda nyingine ambazo mimi siwezi kuzielewa kwa sababu hazinihusu.”
Wema, Diamond na Lulu hawakupatikana lakini nao muda si mrefu watakaa kwenye 18 na kueleza kinagaubaga.

chanzo:globalpublishers

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WANAJUMUIA WANAOISHI NCHINI AUSTRALIA


 
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa watanzania waishio Australia Asimwe Kabunga katika mkutano unaowajumuisha watanzania waishio Australia okt, 26-2011. Rais Jakaya Kikwete pamoja wanajumuia ya watanzania wanaoishi Australia wamezungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo.
 
Baadhi ya wanajumuia wanaoishi nchini Australia wakimsikiliza. Rais Jakaya Kikwete hayupo pichani alipokutana nao Okt.26.2011 mjini Perth Australia.

 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kulia) akipokea maua kutoka kwa mweka Hazina wa Jumuia ya Watanzania waishio Australia Maryam Powell jana walipokutana na wanajumia mjini Perth Australia. Rais Jakaya Kikwete alikutana na wanajumuia kuzungumza mambo mbalimbali ya maendeleo na kijamii, Rais yupo nchini Australia kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa jumuia ya madola (Commonwealth Heads of Government Meeting- CHOGM 2011, utakaanza Oktoba 28-30, 2011.
 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akibadilisha mawazo na mwanajumuia wa Australia Dr.Joseph Masika wakati Rais Jakaya Kikwete alipokutana na wanajumuia wanaoishi Australia 0ktoba 26, 2011 na kuzungumza nao mambo mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu.
 
Baadhi ya wanajumuia wanaoishi nchini Australia wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete hayupo pichani alipokutana nao Okt.26.2011 mjini Perth Australia.
 
Picha ya pamoja ya wanajumuia wa kike wanaoishi Australia pamoja na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete baada ya kuamlizika mkutano wa Rais Kikwete na Watanzania wanaoishi Australia, jana.
 
Mama Salma Kikwete akisalimiana na mmoja wa wanajumuia.

Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

VODACOM BRINGS WEBBOX INTERNET ACCESS INTO YOUR ROOM



Dear Tanzanians,
Now Vodacom Tanzania brings you an internet access in your living room, a reality with Vodafone WebBox. “The 21st century is all about science and technology, anyone not connected to the internet is left behind. However here at Vodacom, we are at the forefront of enabling people to get connected to the world of internet in a manner which is smart and very affordable. This initiative will greatly increase opportunities for people to communicate and even enhance the way they do business” said Nector Foya Head of Corporate Affairs-Vodacom Tanzania. The Vodafone WebBox is specifically developed for customers in the emerging markets in which technology and high costs of equipment restrict many from enjoying affordable and reliable internet access.
It’s a great relaxed service, convenient… Vodafone WebBox is plug-n-play keyboard with a built-in EDGE modem and memory card that simply plugs into a television, turning your TV into a computer screen, allowing user to access emails, listen to radio, and open documents and social media in the comfort of your sofa.
All you need is an active SIM with data services activated and ANY TELEVISION SET (old or new, hunch back screen, plasma or LCD, 18 inch to 48 inch) so long as it has an RCA inputs.

Tuesday 25 October 2011

KILIO KWA WAFANYAKAZI POSTA BONGO ACHENI WIZI

Habari za mchana,mie nina kilio changu na posta makao makuu dar,sie tulioko ughaibuni tunatuma parcel nyumbani tena inakuwa zawadi ya birthday au harusi,cha ajabu mzigo wenyewe unalipiwa kodi hapa ulaya na mzigo ukishafika tena dar unalipia tena zaidi hata ya zawadi iliyoko ndani...Pia cha kushangaza zaidi wanapekua mizigo wakikuta vitu kama chocolate wanafungua na wanaanza kula bila hata ruhusa!!!,mwaka jana nilituma parcel kwenda nyumbani zilikuwa nguo za mtoto aina ya nike parcel likatokomea palepale posta..sasa jamani posta kubwa kama dar mkianza kudokoa vitu vidogovidogo kama chocolate,pipi na nguo za watoto hivi kweli tutafika...Tunaomba uongozi wa posta dar waangalie ni vitu gani vya kutoza kodi na kodi isiwe kubwa zaidi ya zawadi,inakuwa haina maana kumtumia mtu zawadi halafu kulipia hela nyingi..mie ni hayo tuu.."
Na mdau toka Ughaibuni

Muammar Gaddafi 'buried in desert grave at dawn'



Footage showed what is believed to be a convoy of vehicles taking Gaddafi's body to be buried


The bodies of ex-Libyan leader Muammar Gaddafi, his son Mutassim and a top aide have been buried in secret in the desert, Libyan officials say.

A National Transitional Council (NTC) official told the BBC the bodies were buried at dawn in an unknown location.

This follows days of apparent uncertainty among the new leadership about what to do with the bodies.

Gaddafi's family wanted them buried outside the former leader's hometown of Sirte.

NTC leaders had expressed a preference for a secret burial.
Bound by Fatwa
Officials have given few details of the ceremony.

They say it took place early on Tuesday. A few relatives and officials were in attendance and Islamic prayers were read.



The tussle over the body was between the Misratan military brigades who captured and killed Col Gaddafi on Thursday and the politicians - the National Transitional Council - who are now trying to take charge of the whole of this country.
The body of Col Gaddafi was the number-one war trophy after eight months of civil war.
The tussle over it was all part of a behind-the-scenes positioning for power in the new Libya that we'll probably see the aftershocks of reverberating out in the weeks and months to come.

Libya's Minister for Information Mahmoud Shammam said the NTC was following a fatwa, or religious ruling.

"It says that his body should not be buried in Muslim cemeteries and should not be buried in a known place to avoid any sedition," Mr Shammam said.

An NTC official had earlier told Reuters news agency that Col Gaddafi would be buried in a "simple" ceremony with "sheikhs attending" on Tuesday.

"It will be an unknown location in the open desert," he said, adding that a burial was needed because decomposition of the body had reached the point where the "corpse cannot last any longer".

Gaddafi, Mutassim and former Defence Minister Abu Bakr Younis Jabr were killed on Thursday following the fall of Sirte, the last major pro-Gaddafi bastion.

Witnesses said the bodies had been removed late on Monday from the meat storage warehouse in Misrata where they had been on display.

The BBC was told prayers were said over the bodies before they were driven away.

"Our job is finished," a security guard at the warehouse, Salem al Mohandes, told the Arabic television station al-Jazeera. "[Gaddafi] was transferred and the military council of Misrata took him away to an unknown location."
Shrine fears
The BBC's Katya Adler in Tripoli says the question of how to dispose of Gaddafi's body has been a political minefield for the new Libyan leadership, and is the reason why it has taken four days for a decision to be taken.

Islamic tradition dictates a burial should happen within a day of the death.

But the NTC leadership was concerned that any public grave could become a shrine for Gaddafi loyalists or a target of hatred for those who opposed his regime, our correspondent says.

In the end, she adds, the decomposition of the body meant the NTC had to act.

Questions have been raised over the former leader's death after video footage showed him alive at the time of capture. Officials said he had been killed subsequently in a crossfire.

A post-mortem examination carried out on the 69-year-old's body on Sunday showed he had received a bullet wound to the head, medical sources said.

Acting Libyan leader Mustafa Abdul Jalil said the NTC had formed a committee to investigate the circumstances surrounding his death.

Meanwhile another of Gaddafi's sons, Saif al-Islam, remains at large. He is believed to have fled towards the desert border with Niger.

A Niger official said Saif al-Islam Gaddafi was travelling with ethnic Tuaregs - who were among Gaddafi's supporters.

BBC

KANAL GHADAFFI AKILA KIBANO BAADA YA KUKAMATWA

BASI LA DELUXE LAPINDUKA NA KUWAKA MOTO





basi la deluxe likitokea dodoma kuelekea dar limepinduka na kuwaka moto eneo la misugu sugu kibaha pwani,inasemekana abiria zaidi ya 40 wanahofiwa kupoteza maisha  katika ajali hiyo.
tutaendelea kuwajuza kinachoendelea

picha kwa hisani ya michuzi

MJUE VUMBI KAHANGA DEKULA MPIGA SOLO WA MAQUIS ORIGINAL ENZI HIZO

 
Kwa wapenzi wa muziki wa enzi wa Tanzania jina la mpiga gitaa Dekula Kahanga Vumbi si geni, lakini baba yake hakupenda kabisa apige gitaa, lakini bahati nzuri alikulia kwa bibi yake katika mji wa Uvira, mkoa wa Kivu, Jamhuri ya Kongo ambako alikuwa na uhuru zaidi na akaanza kwa kutengeneza magitaa yake, ambalo lilikuwa likivunjwa kila baba yake alipokuwa akija kumtembelea bibi yake.Jirani na alipokuwa akiishi kulikuweko na bar inaitwa Sikiya sosi ambapo palikuweko na bendi ikiitwa Gramick Jazz, bendi iliyopitiwa na wanamuziki wengi waliokuja Tanzania akiwemo Dr Remmy. Alikuwa akisikiliza muziki ukipigwa katika hiyo bar na yeye akawa anafuatisha kwenye gitaa la kutengeza mwenyewe la nyuzi tatu, hatimae bibi yake akamnunulia gitaa dogo la nyuzi nne ambalo alikuwa naaenda nalo mpaka shule, ambapo mwalimu wake siku nyingine alikuwa akimwita awatumbuize wanafunzi wenzie. Hatimae akakutana na jamaa aliyekuwa akipiga katika bendi iliyokuwa ikimilikiwa na mapadri, akawa anamnunulia sigara huyu jamaa nae akaanza kumfundisha chords mbalimbali za kupiga gitaa. Aliendelea vizuri hatimae akajiunga na bendi hiyo ya mapadri iliyoitwa Kyalalo Band akiwa mpiga rhythm. Wanamuziki wa Kyalalo hawakuruhusiwa kujiunga na bendi zilizo kuwa zinapiga muziki kwenye bar, wala bendi yenyewe kwenda kupiga kwenye bar, kulikuweko na ukumbi mkubwa wa kanisa na hapo ndipo walipofanya mazoezi na maonyesho, lakini baadae Vumbi akajiunga na bendi Bavy National tena kama mpiga rhythm,

Kutoka kulia mstari wa nyuma ni Dekula (Rythm),Packot(Solo na Kiongozi),Maboko(Besi),
Merry-Djo (Drums).
Kutoka kulia mstari wa mbele,Waimbaji ni Djo-Mali,Issa Nundu na Simplice Mofeza.
Mwaka wa 1983 katika "Sikia Sosi Bar" Mjini Uvira Mkoani Kivu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
na hapo akakutana na mwimbaji Issa Nundu ambae alikuwa anafanya hospitali na jioni kujiunga na bendi, hatimae Kyanga Songa ambaye kazi yake ilikuwa Bwana Shamba nae alijiunga nao.
Katika kipindi hicho wakazi wa Kongo ya Mashariki, ambako kunazungumzwa kiswahili, walikuwa wakisikiliza na kuzijua bendi nyingi kutoka Afrika ya Mashariki, bendi kama Tabora Jazz, Mangelepa, Simba wa Nyika, Mlimani Park zilisikilizwa sana, na nyimbo kama Kassim ilikuwa nyimbo maarufu wakati huo na hivyo ikawa ndoto ya Vumbi kuwa lazima siku moja waende huko unakotoka muziki mtamu huo ili nae aweze kushiriki. Katika kipindi hicho Kyanga Songa na Issa Nundu waliondoka kwenye bendi yao ya Bavi National na kuelekea Tanzania. Bendi ikatetereka sana, lakini nae wakati huo akawa anahamu sana ya kuja Afrika Mashariki. Bahati nzuri mtu mmoja Alida Shanga akamjia akiwa ametumwa na Marehemu Mzee John Luanda aliyekuwa anamiliki Chamwino Jazz kuja kutafuta wanamuziki toka Kongo, nae akawachukua na wakatua Tandale jijini Dar es Salaam, na siku waliofika tu na wakaanza mazoezi siku hiyo hiyo. Wakiwa vijana bado yeye na wenzie watatu walikuja wakiwa na staili ya kuimba na steji show ambayo wakati huo iliitwa sarakasi, na pia wao ndo kilikuwa kikundi cha kwanza kuanza kurap katikati ya nyimbo. Waimbaji wakiwa ni Sisko Lunanga, Fanfan Bwami, na mwenzao mmoja Baposta Kilosho ambae hatimae alirudi Kongo. Recording ya kwanza ilimuacha Julius Nyaisanga akishangaa vituko vya vijana hawa. Katika bendi ya Chamwino wakati huo wapiga magitaa walikuwa Vumbi Dekula, Kazembe wa Kazembe (huyu alikuwa Msukuma ambaye aliishi kwa muda Kongo na alikuwa mpiga gitaa hodari sana), na Mzee Albert, na hatimae wakamchukua Muhidin ambae alikuwa mpiga bezi wa Dr Remmy. Siku moja walienda kuomba kupiga na Maquis Original(lift), wakati huo wakipiga nyimbo za kopi, nyimbo kama Mario, Maze na kadhalika, hivyo wakazipiga hizo na watu wakafurahi sana na kuwatuza fedha nyingi, wakachanganyikiwa maana bendi yao ya Chamwino ilikuwa haina mshahara na si mara moja walitembea kwa miguu toka Buguruni hadi Tandale kwa kukosa mapato. Japo wakati huo walikuwa wadogo kwa umri na hata umbo walifika mahala marehemu Kasheba alikuwa anawaita ‘Vimario’, upigaji wao ulikuwa mzuri sana. Nguza aliwashauri wawe wanakuja kupiga kabla Maquis hawajaanza kupiga. Hivyo wakaamua kuacha Chamwino, na wakawa wanasindikizana na Maquis, hili lilimuudhi aliyewaleta na siku moja wakiwa Silent Inn, maafisa wa Uhamiaji walikuja kuwachukua wakalazwa Central Police na kisha kupelekwa gereza la Keko. Wakiwa huko walimwandikia Mzee Luanda kuwa wanarudi Chamwino, basi wakaachiwa na kurudi kusuka upya Chamwino Jazz. Lakini hawakukaa muda mrefu Mzee Makassy akaja kuwaomba waingie katika bendi yake, wenzake waimbaji wakaenda yeye akabaki Chamwino, lakini muda si mrefu Nguza akamwambia aandike barua ajiunge na Maquis. Nae akafanya hivyo na ndio kujiunga rasmi na Maquis kama mpiga gitaa la second solo. Aliwakuta wanamuziki kama Maneno Uvuruge, Omari Makuka, Keppy kiombile, Ilunga Lubaba, William Maselenge na wengine wengi. Aliendelea kupiga second solo hadi siku moja bendi ilikuwa inapiga maeneo ya Ukonga, kwa kawaida Mzee Lubaba alikuwa anapiga kuanzia saa tatu mpaka saa sita, na kisha Nguza Viking akiingia na kuendelea .

Wa pili toka kulia na shati jeusi Vumbi, wapili toka kushoto na suruali nyeusi Issa Nundu
Siku hiyo Nguza hakuonekana Vumbi akaweza kupiga nyimbo zote za Nguza, na kesho yake akaambiwa afike ofisini akasainishwa rasmi mkataba wa kuwa mwanamuziki wa Maquis. Baada ya muda mfupi Nguza akaacha bendi.

Na baada ya hapo walirekodi ule wimbo maarufu wa Makumbele, solo ya wimbo huu ilikuwa awali ikipigwa na Mzee Lubaba, lakini afya ya mzee Lubaba ilianza kuzorota nae akawa anawafundisha nyimbo zake wanamuziki wengine, wimbo wa Makumbele alifundishwa Makuka na akawa anaupiga katika mahonyesho mbalimbali, lakini wakati wa kutaka kurekodi kamati ya uongozi ya Maquis iliamua Vumbi aufanyie mazoezi na aurekodi. Kurekodi kwa album ya Makumbele ilitokana na safari ndefu ya bendi ambayo ilichukua miezi mitatu katika mikoa ya Ziwa, hivyo bendi iliporudi Dar ilikuta sifa ya bendi imepungua, hivyo walirekodi album ya Makumbele iliyokuwa na nyimbo kama Tipwatipwa, Ngalula na Makumbele, sifa ya bendi ikarudi juu tena kwa mara nyingine. Na ni wakati huo ambapo bendi ilihamia katika ukumbi wa Lang’ata  KINONDONI
 
 
habari yote kwa hisani ya kitineblog

Friday 21 October 2011

KARIBU NGUNA


RECIPE YA HII NATUMAI WOTE TUNAIFAHAMU

VUMBI & DEKULA BAND LIVE @ LILLA WIEN BAR STOCKHOLM 22 0CT


                                                                               
                                                


                                               Dekula Band"Ngoma ya Kilo"
Place: Lilla Wien"Little Nairobi"
Date: 22 Oct.2011
Time: 21.00-01.00
Add: Swedenborgsg.20... Pendel: Södra Station

NGOMA YA WATOTO:HATIMAYE WEMA NA DIAMOND WAMWAGANA



hapa wakivalishana pete




maraa







utamuuuu



wakati wa beibeee beibeee





dogo akajitosa mzima na pete




Musa Mateja na Imelda Mtema
NGOMA ikilia sana ujue inakaribia kupasuka na lisemwalo lipo kama halipo, basi li njiani laja! Hatimaye Wema Isaac Sepetu na Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’, wamemwagana rasmi, The Udaku Master, Ijumaa lina ‘eituzedi’ ya mkasa mzima.

Ilikuwa ni Jumanne, saa mbili usiku, Diamond ‘Platinum’ aliita vyombo vya habari katika Hoteli ya Lion Sinza jijini Dar es Salaam na kufunguka:


“Washikaji, nimewaita hapa nifunguke mbele yenu kuwa nimemmwaga rasmi yule demu (Wema) kwa sababu hapatani na mama yangu (Sandra Sammy).

ALINILAZIMISHA NITENGANE NA MAMA
“Kwanza Wema amekuwa akinilazimisha nitengane na mama yangu, yaani nimrudishe kule Tandale tulipokuwa tukiishi mwanzo , halafu mimi na yeye tuishi Sinza (Madukani), jambo ambalo sipo tayari kulifanya.


“Mimi na mama tumetoka mbali, hakuna kama yeye, alikuwa akishinda njaa ili mimi nisome, alinilea kwa shida sana, hata siwezi kuelezea kwani nikikumbuka huwa natokwa machozi, kwa hiyo siwezi kumtelekeza kwa sababu ya Wema.
“Hata katika muziki, nakumbuka nilishamuibia pete yake ya dhahabu nikaenda kuiuza ili nirekodi muziki na alinivumilia.

NI WAKATI WA MAMA ‘KUINJOI’
“Piga ua, huu ni wakati wa mama yangu kula na ‘kuinjoi’ matunda ya mwanaye, mapenzi hayawezi kusababisha nimtende vibaya. Natamka rasmi huyu demu nimemmwaga bwana.”

SWALI LA MWANDISHI WA IJUMAA
“Mlianza mapenzi muda mrefu na ni wiki mbili tu zimepita tangu ulipomvisha pete ya uchumba, je, hukujua kwamba mambo kama haya yangetokea?


DIAMOND AKAJIBU
“Sikuligundua hilo mapema na pia si unajua mambo ya ujana tena? Ukweli ni kwamba tukio hili limenikumbusha kuwa ujana ni jalala linalotupwa kila aina ya takataka.”

UPANDE WA WEMA
Baada ya Diamond kumwaga unga na ishu hiyo kuwa gumzo jijini Dar usiku kucha, kama ilivyo desturi ya gazeti hili namba moja kwa habari za mastaa nchini, asubuhi na mapema (Jumatano), mapaparazi wake wa kuheshimika walimsaka Wema ili kupata mzani wa habari hiyo.


NDANI YA HOTELI YA LAMADA
Kutokana na uzito wa habari yenyewe, Ijumaa lilisaga lami hadi Hoteli ya Lamada Ilala, chumba namba 35 flati ya Mikumi ambapo Wema alikuwa kambini kwa ajili ya kurekodi filamu.

HALI ILIKUWA HIVI
Baada ya kubisha hodi, ‘mkaribisha wageni’ alikuwa Elizabeth Michael ‘Lulu’, alifungua mlango ambapo Wema alishuhudiwa akinyanyuka na kwenda kuosha uso, aliporejea na kuwaona ‘polisi’ wa Ijumaa wakifunga ‘makamera’ yao alipaza sauti na kufuatiwa na kilio: “Maweee! Nimeachwa? Nyiii….nyiiiii.”


Lulu: Nyamaza Wema usikie kilichowaleta.
Ijumaa: Mambo vipi Wema?

Wema: Hata salamu yenu sitaki, niambieni nimeachwa?
Ijumaa: Poa, ili mgonjwa apone lazima achomwe sindano inayouma au ameze vidonge vichungu. Iko hivi Wema; jana pale Lion Hotel, Sinza, Diamond alitangaza rasmi kukutema kwa sababu eti umekuwa ukimlazimisha kumtenga mama yake ili muishi peke yenu, yeye hayupo tayari kufanya hivyo, je, hili unalizungumziaje?


Wema: (kilio) siko tayari kuzungumza chochote.
Ijumaa: Tafadhali waambie mashabiki wako umeipokeaji taarifa hii?

Wema: Amenidhalilisha, nitaweka wapi uso wangu? Anyway, niacheni nitawatafuta baadaye niongee.
Lulu: Dada Wema, funguka tu kile unachokijua, itakusaidia watu wajue ukweli.
Wema: No, please. Waondoke tu nitawatafuta baadaye.


UTABIRI
Ili kuthibitisha kuwa kile kinachoandikwa na Magazeti Pendwa ya Global Publishers kina uhakika asilimia zote, wakati hayo yanatokea, tayari gazeti tumbo moja na hili, Risasi Mchanganyiko toleo namba 844 la Jumatano wiki hii lililokuwa na kichwa cha habari: WEMA, DIAMOND HAKUNA NDOA, lilitabiri na kuweka vigezo kuwa Wema na Diamond hawatadumu.

Aidha, Gazeti la Risasi Jumamosi iliyopita, ukurasa wa 16 kulikuwa na habari yenye kichwa; ETI WEMA, MAMA MKWE WAKE HAWAIVI.
Diamond alionesha kutokubaliana na madai hayo, lakini yaliyotokea yameweka wazi.


WADAU WANASEMAJE?
Kwa mujibu wa wadau walioinyaka habari hiyo walilieleza Ijumaa kuwa haijawahi kutokea Wema akamwagwa na midume kwani yeye ndiye huwa anawamwaga.
“Ama kweli mtenda akitendewa…safari hii kaachwa yeye!” alisema mmoja wa wadau hao.


ANATAMANI DUNIA IRUDI NYUMA
Uchunguzi wa Ijumaa ulibaini kuwa usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii, Wema hakupata usingizi kwa kuwa alishanusa dalili za tukio hilo.

“Ukweli Wema hakulala kabisa, alikuwa akijigeuza mara kwa mara na kutaja jina la Diamond huku akilia, alipoulizwa kulikoni alijibu: “Natamani dunia irudi nyuma ili lile tukio la kuvishwa pete ya uchumba pale New Maisha Club wiki mbili zilizopita lifutike,” alisema mmoja wa wasanii aliyekuwa naye kambini hapo.

chanzo:global publishers

Thursday 20 October 2011

TAARIFA YA MSIBA:FERUZI AHMED AMEFIWA NA BABA YAKE


Kwa Jumuiya ya Watanzania,


Feruzi Ahmed Said (Mume wa Dorina) amefiwa na baba yake mzazi Mzee Ahmed Said leo alfajiri.

Feruzi anapenda aende nyumbani (Dares Salaam) haraka iwezekanavyo kuhudhuria mazishi kama atawahi. Ikishindikana aende kuhani.

Yeye na mke wake wanaleta ombi la msaada wa hali na mali kwa jumuia ya watanzania ili Feruzi aweze kwenda katika mazishi.

Kwa maelezo zaidi ya jinsi ya kumfikishia msaada huu kama una uwezo, tafadhali piga simu Na. 0722982865 (Feruzi) au 0737143048 (Dorina).

Kwa wale wataoweza kwenda kuwaona msiba uko, Konsolvägen 7, Hökarängen, (Green Line kwenda Farsta)

Watashukuru sana kwa msaada wenu.

KANDA BONGO MAN LIVE IN STOCKHOLM 26 NOV 2011

AAMON PROMOTIONS/ORKARINTE.SE PRESENTS AMANI IN STOCKHOLM




                                                  Time : 29 October at 20:00 - 30 October at 05:00




                                           Location   : VÄSTBERGA ALLE 15-15 VÄSTBERGA


Amani has recently been signed to Sony Music under Rockstar 4000 (2010). She recently worked on a ground breaking song with International R n B singer R.Kelly alongside top African stars i.e. Ali Kiba, Navio, Fally Ipupa, 2face Idibia, JK, 4*4 and Movazeleine. The song titled 'Hands Across the World' made it to the billboard 100 and had over 1 million downloads in Africa.

                         
                                            She is currently the brand Ambassador for Airtel kenya.


                                                  -2009 MTV BEST AFRICAN FEMALE AWARD-


                                                                 DJ MIKE IN THE HOUSE
      
           


Libya's Col Muammar Gaddafi killed, say NTC officials




A video grab from al-Jazeera TV apparently showing Colonel Muammar Gaddafi's corpse

dead man ghadaffi

Hole where Gaddafi allegedly captured

he was captured in this hole

The BBC's Gabriel Gatehouse in Sirte: "I have spoken to the man who says that he captured him... he said he found him hiding in a hole"
Libya's ex-leader Col Muammar Gaddafi has been killed after an assault on his home town of Sirte, officials from the transitional authorities have said.
Information Minister Mahmoud Shammam said fighters had told him they had seen Col Gaddafi's body, and other officials also said he was dead.
The claims have not yet been independently verified, and other reports said he was captured alive.
The colonel was toppled in August after 42 years in power.
The International Criminal Court has been seeking his arrest.
Golden gunMobile phone image alleged to be of Muammar Gaddafi - 20/10/11

Nato, which has been running a bombing campaign in Libya for months, said it had carried out an air strike earlier on Thursday that hit two pro-Gaddafi vehicles near Sirte.

Mobile phone image alleged to be of Muammar Gaddafi - 20/10/11
It was unclear whether the strikes were connected with the reports of Col Gaddafi's death.
The head of the National Transitional Council (NTC) Mustafa Abdul Jalil is expected to give a national TV address on Thursday.
Mr Shammam said the NTC leader would officially confirm Col Gaddafi's death.
"He was killed in an attack by the fighters. There is footage of that," he said.
Grainy video footage has been circulating among NTC fighters appearing to show Col Gaddafi's corpse.
AFP news agency reported that the video showed a large number of NTC fighters yelling in chaotic scenes around a khaki-clad body, which has blood oozing from the face and neck.
Another NTC official, Abdel Hafez Ghoga, told AFP: "We announce to the world that Gaddafi has been killed at the hands of the revolution.
"It is an historic moment. It is the end of tyranny and dictatorship. Gaddafi has met his fate."
An NTC fighter told the BBC he found Colonel Gaddafi hiding in a hole in Sirte, and the former leader begged him not to shoot.
The fighter showed reporters a golden pistol he said he had taken from Col Gaddafi.

BBC

Friday 14 October 2011

Swedish Police arrest 32 people in 'human trafficking' raid


Swedish police arrested 32 people in a raid on a food factory south ofStockholm on Thursday for violations of the Aliens Act.
Police now suspect that many of the arrested workers could have been victims of human trafficking.

"That was not in our minds when we started, but after interviews we are having a closer look," said Stefan Hagberg at the Swedish border police told the Aftonbladet daily.

Police officers raided the factory just as many were arriving for work at 8am on Thursday.

The premises belongs to Eat Food Factory Europa AB, one of Scandinavia's largest producers of chilled ready-meals and a supplier to, among others, Coop, Lidl, SJSAS and Mat pÃ¥ jobbet.

According to Aftonbladet the majority of those arrested in the raid come from Uzbekistan or other former Soviet republics.

When the police arrived at the factory in Jordbro south of Stockholm there were 54 people working in the factory, 32 were detained and taken from the premises.

Eat Food Factory's owner Murat Korkmaz played down the significance of the raid.

"There is nothing untoward. The police often carry out these kinds of checks. They are just checking that the identity papers in the the employees' paper checks out," he said to Aftonbladet.

Korkmaz told the newspaper he felt let down by his employees, claiming they tricked him with false papers.

The raid isn't the first time the company has been hit with suspicions of sub-standard labour practices.

In 2008, when the company was called Mo Catering, workers described how asylum seekers and undocumented workers were forced to work under “slave-like” conditions. 

However, the accusations were denied by company officials, who claimed the complaints were unfounded.


the lokal

Tanzania rejects Eritrean footballers' asylum bid



Red Sea footballers

Tanzania has rejected an asylum request by 13 young Eritrean footballers who refused to return home after a regional tournament in July.
The footballers had failed to prove that their lives would be in danger in Eritrea, a government spokesman said.
A UN official said an appeal would be made to other countries to give refuge to the former Red Sea FC players.
Young Eritreans often try to escape poverty, a repressive government and national military service.
Tanzania's home affairs ministry spokesman Isaac Nantanga told the BBC the players seemed to have applied for asylum because they wanted "greener pastures" - not because of a lack of security in Eritrea.
Absconded
The footballers - aged between 18 and 23 - are in the custody of the UN High Commission for Refugees (UNHCR).
UNHCR Tanzania representative Oauseyi Bajulaiye told the BBC the UNHCR was still in discussions with the Tanzanian authorities about their future.
He said the UNHCR would try to find a "safe country" that would give the footballers "resettlement" status, he said.
In July, the 13 Red Sea FC players failed to board a flight to Eritrea after being knocked out of the Cecafa Championship during the semi-final stages.
Instead, they went to the UNHCR offices to seek protection.
It was reportedly the fourth time that Eritrean footballers had absconded while on tour.
Eritrea is a one-party state, ruled by President Isaias Afewerki.
Human rights activists say government critics are routinely arrested and tortured.

BBC

HAMAD NDIKUMANA "KATAUT" BACK TO PLAY RWANDAN LEAGUE



image

RAYON Sport is trying to lure Hamad Ndikumana a.k.a Katauti back to the club according to the club’s Secretary General Olivier Gakwaya.
The 33-year-old center back is currently without a club after being released by Cyprus first division side APOP Kinyras Peyias and is keen on re-uniting with his former club but only on a short-term contract as he continues to look for a European club.
“We are still discussing with him but no agreement has been reached yet,” Gakwaya said.
“He has made it clear that if a European club comes calling, we should not stand in his way but we remain hopeful that we can secure a season-long deal with him,” Gakwaya said.
Rayon believes Katauti can be a perfect replacement for Faustin Usengimana, who is expected to feature for the U-20 side in the Primus League.
The U-20 side is made of players who graduated from the U-17 side that took part in the 2011 Fifa U-17 World Cup in Mexico.
Katauti enjoyed five seasons at Rayon between 1995 and 2000 before joining Anorthosis. The player has also featured for KV Mechelen, APOP Kinyras Peyias, Nea Salamina and KAA Gent.

source.newtimesrw

ikulu yakana jk kuwasamehe askari waliomuua jenerali kombe



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Gazeti la Mwananchi, matoleo ya jana, Jumatano, Oktoba 12 na leo, Alhamisi, Oktoba 13, 2011, limeandika habari zilizodai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alitoa msamaha wa kupunguza adhabu ya kifo iliyowakabili askari polisi wa zamani waliopatikana na hatia ya kumpiga risasi na kumwua kwa makusudi aliyepata kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Luteni Jenerali Imran Kombe Juni 30, 1996.

Gazeti hili limedai kuwa Mheshimiwa Rais Kikwete alitoa msamaha huo kwa kupunguza adhabu ya kifo iliyokuwa inawakabili makonstebo wapelelezi Mataba Matiku na Juma Muswa na kuibadilisha kuwa kifungo cha miaka miwili.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa Mheshimiwa Rais Kikwete hajawahi na hajapata kuhusika hata kidogo kutoa msamaha wa kirais kwa kupunguza adhabu ya wauaji hao wa Luteni Jenerali Kombe tokea kuingia madarakani.Masuala yote yanayohusu polisi hao waliohukumiwa kifo kwa mauaji ya Luteni Jenerali Kombe yalifanyiwa maamuzi kabla ya Rais Kikwete kuingia madarakani Desemba 21, 2005.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
13 Oktoba, 2011

Thursday 13 October 2011

TUKIMKUMBUKA MWALIMU NYERERE-RUSHWA



hayo yalikuwa maneno ya mwalimu enzi hizo kuhusu rushwa,siku hizi rushwa imekua kama fashion maana sasa unaombwa rushwa tena waziwazi.

rushwa hii imetufikisha mahala tunalala gizani ama kutumia vibatari

JB MPIANA &WENGE BCBG NEW SEBEN 2011 "BILOKO" LIVE FIKIN


live



oficial video
 "cheza kadogoooo"
ukisikiaa hivyo unajua anamaanisha nini?
haya tena hii ni kwa wapenzi wa mabolingo na misebene asiyependa atavumilia siku tutampatia kwaya
hii concert imepigwa pale kinshasa fikin hivi karibuni mwezi huu,utaona jinsi jamaa wanavyojibidisha kwa stage maana kama ni show ni ya ukweli.na hii ndio pilipili ya jibe mpiana papa cheri mukulu kulu,ye huwa anawaacha wengine watangulie waimbe weee,wapige vijembe weee siku akija kutoa kitu anawachezesha pande zote nne za stage.werra na koffi inabidi wajipange upya tena kuweza kumpata jibe sasa hivi

WAZIRI MKULO AKUMBWA NA KASHFA






WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo ameivunja Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC), wakati ambao bodi hiyo ilikuwa ikisubiri kupokea ripoti ya ukaguzi uliofanywa na Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ukilenga kubaini tuhuma za kuwapo kwa ufisadi katika shirika hilo.

Msingi wa uchunguzi ndani ya CHC, ni maombi ya Bodi ya shirika hilo hodhi kwa CAG, kufuatia kuwapo kwa tuhuma kwamba menejimenti yake ilihusika na vitendo vya ufisadi, hivyo kusababisha kusimamishwa kwa Kaimu Mkurugenzi wake, Methusela Mbajo.

Ofisi ya CAG ilifanya uchunguzi kwa kutumia kampuni ya kimataifa ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst&Young, ukaguzi ambao pia ulilenga kubaini tuhuma dhidi ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), inayoongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Katika Mkutano wa Nne wa Bunge, Mkulo aliingia katika mvutano na Zitto baada ya waziri huyo kumtuhumu mbunge huyo na Kamati yake kwamba walihongwa ili kutetea nyongeza ya muda wa CHC, tofauti na mawazo ya Serikali ya kutaka kufutwa kwa shirika hilo.

Baada ya tuhuma hizo, Zitto aliapa bungeni kwamba kama uchunguzi utathibitisha yeye au wajumbe wa POAC wamehongwa, angejiuzulu uenyekiti na ubunge na kumtaka Waziri Mkulo nae atoe kiapo chake bungeni kama atajiuzulu akibainika amefanya ufisadi ndani ya CHC.

Mkulo akijibu swali hilo alishindwa kula kiapo na Spika wa Bunge, Anne Makinda akamkumbusha kuhusu kula kiapo kama atajiuzulu, lakini waziri huyo aligoma kufanya hivyo.

Lakini wakati CAG akiwa katika hatua za mwisho kukamilisha ripoti yake ambayo kimsingi ilipaswa kukabidhiwa kwa bodi ya CHC, uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa Mkulo amevunja bodi hiyo kabla ya kumaliza muda wake wa nyongeza ambao ulipaswa kumalizika Desemba 31, mwaka huu.

Uhai wa Bodi ya CHC
Awali bodi ya CHC ilikuwa imalize muda wake Juni 30 mwaka huu, lakini Mkulo aliiongezea muda hadi Desemba 31, mwaka huu na barua ya hatua hiyo ilitumwa kwa wajumbe wa bodi hiyo kuwajulisha hatua hiyo ya waziri Julai 29, 2011.

Hata hivyo, ghafla Mkulo alibadili uamuzi wake Oktoba 10, 2011, kwa kumwandikia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC kwamba awaarifu wajumbe wa bodi kuhusu uamuzi huo.

Sehemu ya barua kutoka Wizara ya Fedha kwenda CHC ambayo Mwananchi imeiona inaeleza: “Nimeelekezwa nikuarifu kwamba Waziri wa Fedha, Mh. Mustafa H. Mkulo (Mb), ametengua uamuzi wake wa kuongeza muda wa Bodi ya CHC hadi tarehe 31 Desemba, 2011 au hapo Rais atakapoteua Mwenyekiti wa Bodi hiyo kuanzia tarehe ya barua hii (10, Oktoba, 2011).”

Barua hiyo iliyosainiwa kwa niaba ya Katibu Mkuu Hazina na Geoffrey Msella pia inasema; “Kwa barua hii unatakiwa kuwaandikia barua waliokuwa Wajumbe wa Bodi ukiwashukuru kwa michango yao kwa Shirika hili katika kipindi walichotumikia CHC.”

Kufuatia barua hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC, Dome Malosha siku hiyo hiyo ya Oktoba 10, 2011 aliwaandikia barua wajumbe hao wa Bodi akiwaarifu kuhusu uamuzi wa Waziri Mkulo kuvunja bodi hiyo.

Ukaguzi wa CAG
Uchunguzi wa Mwananchi umebiani kuwa hatua ya Mkulo kuvunja bodi ya CHC ilifanyika muda mfupi tu, tangu alipojibu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utuoh kuhusu kile ambacho kinaonekana kuwa ni matokeo ya awali ya ukaguzi uliofanywa na Ernst & Young.

Uchunguzi wetu unaonyesha kuwa kulikuwa na mawasiliano baina ya Mkulo na Utouh kati ya Oktoba 6 na 8, 2011, na baadaye kuvunjwa kwa bodi Oktoba 10.

Oktoba 8, 2011, Mkulo alimwandikia barua Utouh akikanusha kwamba hahusiki na ufisadi wowote ndani ya CHC, kauli inayothibitisha kwamba alitajwa katika taarifa yake hiyo.

Katika barua hiyo ambayo pia Mwananchi imeiona, Mkulo anakanusha kile alichosema kuwa ni tuhuma za kuhusishwa na uuzwaji wa mali za CHC kinyume cha sheria.

Barua hiyo ya Mkulo kwenda kwa CAG ina kumbukumbu Namba TYC/B/70/03 na kichwa cha habari, YAH: UKAGUZI WA CONSOLIDATED HOLDING CORPORATION ikirejea mazungumzo ya simu baina ya viongozi hao wawili Oktoba 7, mwaka huu, pia ujumbe mfupi wa simu kutoka kwa Utouh kwenda kwa Mkulo Oktoba 6, 2011.

Waziri Mkulo katika barua huyo alisema: "Napenda kuthibitisha niliyosema kwenye simu, kwa maandishi kwamba, mimi kama Waziri wa Fedha sijawahi kutoa kibali kwa mwenyekiti wa Bodi ya CHC, kumpa madaraka ya kuuza ama kiwanja au nyumba zinazomilikiwa au kutunzwa na CHC bila kufuata taratibu za zabuni au Sheria ya Manunuzi".

Aliendelea Mkulo akisema, "Kama mwenyekiti wa bodi aliamuru Kaimu Mkurugenzi Mkuu na Bodi ya Wakurugenzi kuuza kiwanja cha shirika bila kufuata taratibu za zabuni, alifanya hivyo kwa ridhaa yake mwenyewe na si kwa maagizo ya Waziri wa Fedha".

Waziri Mkulo alifafanua," Wizara ina utaratibu maalum wa kushughulikia masuala yote yanayohusu mashirika ya umma. Kisheria, huanzia kwa Msajili wa Hazina, kupitia kwa Katibu Mkuu-Hazina (PST/PMG) hadi kumfikia waziri wa fedha kwa uamuzi".

Aliongeza, "Hivyo, utaratibu uliotumiwa na mwenyekiti wa Bodi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC ni kinyume na kanuni za utendaji kazi ndani ya Wizara ya Fedha na pia ni kinyume na kanuni za manunuzi".  

Katika aya ya mwisho ya barua hiyo, Mkulo anasisitiza:, "Nakushukuru sana kwa kunijulisha jambo zito ambalo sikuwa nalifahamu. Natumaini kwa maelezo haya ya maandishi, ofisi yako sasa inaweza kuendelea kukamilisha ukaguzi wa CHC".

Nakala ya barua hiyo, kwa mujibu wa uchunguzi huo zimekwenda kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo na  Mwenyekiti wa Bodi ya CHC iliyovunjwa, Profesa Hamis Kahigi ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Pia nakala imekwenda kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Ramadhani Khijjah na Geofrey Msella ambaye ni Msajili wa Hazina.

Kauli ya Mkulo
Uamuzi wa Mkulo kuvunja bodi hiyo umezuai hisia kwamba umesukumwa na taarifa za CAG zinazomuhusisha na uuzaji wa mali za CHC.

Lakini, Mkulo alijitetea akisema uamuzi huo ulitokana na ukweli kwamba tayari alikwishamwandikia barua Rais Rais Jakaya Kikwete kuhusu kuisha kwa muda wa bodi tangu Juni 30, hivyo kinachosubiriwa ni mkuu huyo wa nchi kuteua mwenyekiti mpya wa bodi.

Mkulo alisema hakuvunja bodi na kusisitiza kwamba, tayari yenyewe ilikwishamaliza muda hivyo haikuwa sahihi iendelee kukaa madarakani.

Mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo iliyomaliza muda wake alikiri bodi yao kumaliza muda, lakini akahoji mantiki ya Mkulo kuivunja wakati huu ambao ripoti ya ukaguzi inakaribia kutoka.

"Nikweli lazima tumtendee haki waziri. Hakuvunja bodi bali muda ulikuwa umekwisha na sisi tulipaswa kuondoka tangu Juni 30, lakini swali ni moja tu, kwanini waziri kavunja bodi juzi badala ya kusubiri tukabidhiwe ripoti?," alihoji mjumbe huyo kwa shariti la kutotajwa jina.

CAG astuka
CAG Utouh alipoulizwa jana kwa njia ya simu kuhusu suala hilo, alistuka na kusema hadi sasa ripoti haijakamilika kwani bado zinakusanywa taarifa nyingi muhimu ili matokeo yake yasiwe na shaka yoyote.

Utouh ambaye anasifika kwa utendaji makini, alisema hadi sasa uchunguzi huo umekamilika kwa asilimia 90 na kusisitiza, "Tunachokifanya ni kukusanya data zote muhimu kwa umakini".

Aliongeza, "Unajua hili jambo ni zito sana, hivyo tunalifanya kwa umakini mkubwa. Tunataka ripoti yetu ikija kutoka iwe iko based on facts. Sasa, ni suala tu la kuwa wavumulivu ripoti itatoka tu".

Utouh alipoulizwa kuhusu barua ya Mkulo ya kujitetea alicheka kidogo, "Haaahaa!" Kisha akahoji:, "Wewe umeiona wapi? Subirini matokeo, kuweni wavumilivu".

Alipoulizwa  Zitto kuhusiana na sakala la CHC, alisema : Kwa sasa siwezi kuzungumza hadi kesho (leo) nitakapokutana na waandishi wa habari Dar es Salaam,” alisema.



CHANZO: MWANANCHI