Saturday 30 June 2012

TUMETIMIZA MIAKA MIWILI YA NDOA YETU!


isabell kellner unakubali kuolewa na isaac mwamgogwa kwa moyo mmoja kwa shida na raha.


ndio nakubali.   (pete kabaaaa)

"haya na sasa nawaunganisha nyinyi kuwa mume na mke enendeni mkaijaze dunia".
maneno ya padri sio yangu mdau.
na sisi tutaijaza kweli.
maana tunafuata wito.

                                he he hee,mkono huo utadhani nilikua nahofia kuporwa pete dah.






 ILIKUA TAR 25 JUNE 2010 TULIPOAMUA MIMI NA MKE WANGU KUFUNGA NDOA AMA PINGU ZA MAISHA,ALHAMNDULLILAH TULIFANIKISHA NA MUNGU KATUSAIDIA TUMEMPATA KIJANA ANA MWAKA SASA
KWA PICHA ZAIDI ZA TUKIO GOOGLE
 (Isaac +isabell wedding) 
utapata link zote za tukio hilo

Sweden to give illegal immigrants healthcare



The Swedish government, together with the Green Party, on Thursday presented a framework agreement that will allow undocumented immigrants in Sweden to access state subsidized healthcare.
“So-called undocumented immigrants have a legal right to subsidized healthcare,” Christian Democrat head and social affairs minister Göran Hägglund said at a Thursday morning press conference unveiling the migration policy agreement.

The healthcare agreement will give undocumented immigrants who entered Sweden illegally the same rights currently offered to legal asylum seekers.

Children up to 18 years of age will have the right to health coverage. Adults will also receive subsidized care for conditions that require urgent medical attention.

Maria Ferm of the Greens thanked the government for the cooperation on the issue, which her party says was key to a previous pledge to work with the centre-right Alliance parties on a common immigration policy.

“Children and adults are getting an extended right to healthcare and I want to say thank you that we are able to ensure an important step in human rights. The right to healthcare is a human right,” she said.

The original goal of the Green party was to provide the same healthcare rights for undocumented immigrants as those with permanent residence permits in Sweden.

Although this goal won't be achieved, Green Party spokesperson Åsa Romson sees the proposal as a step in the right direction.

“This has been a really important reform for the undocumented immigrants to have confidence in Swedish healthcare and to be able to get care when they need it, and to be able to turn to the hospital and health clinics,” she said.

The biggest success, according to her, is that children under 18 will have the same rights as Swedish children.

This means that they will not only have the right to emergency care, but also to dentistry and preventive care.

However, there still remain details that the Green Party are working on improving.

“There is, for example, undocumented immigrants’ right to education, which will be resolved shortly. But there will also be related to labour migration and the reunion of families,” Romson told TT.

TT/The Local/og

Thursday 28 June 2012

FC KILIMANJARO CONTRIBUTION PARTY IN STOCKHOLM ON 29JUNE 2012


Wapendwa ktk Michezo, maendeleo na FC.K.
Uongozi na kamati kuu ya FC Kilimanjaro unapenda kutoa salaam za dhati kwenu na kwa wote wanaohusika katika kuchangia maendeleo ya chombo hiki. Timu yetu inazidi kusonga mbele. Pia kuna uwezekano FC Kilimajaro ikashiriki mashindano ya daraja la 4 au la 3 (professionalism) mwaka huu au siku za mbeleni ikiwa kuwa na wafadhili (sponsor) katika muda mwafaka wa kukisimamisha chombo hiki muhimu cha maendeleo ya nchi yetu TZ na Afrika mashariki, Afrika na Sweden na kwingineko. Tafadhari husika kichwa cha habari na jarada/attach hapo juu. Michango na Maendeleo ni watu na watu ndio sisi. 
 
COME COME COME/NJOO NJOO NJOONI!!! ITS FC KILIMANJARO CONTRIBUTION PARTY / NI PARTY MCHANGO YA FCKILIMANJARO...
TENA NA TENA WAKARIBISHWA TUJUMUIKE TUKIJUMUISHA FC.K / WELCOME ONCE AGAIN AND LET GET TOGETHER IN SUPPORTING FC.K @KISTA TRÄFF MO-INFO: PS OPEN ATTACHED FILE ABOVE.
WELCOME ONE WELCOME ALL / KARIBU KARIBUNI
Mulashani, Adrey Eustace and Administration

FC Kilimanjaro ORGNR: 802461-7808
TFN FCK: + 46 764405741TFN/TFX WORK: + 46 8 370274 MOBILE + 46 73 7106092

VUMBI DEKULA BAND LIVE SODRA&BOBO SUKARI+LADY NEEMA 29-30 JUNE





Place: Lilla Wien “Little Nairobi”
Date: 29-30 June 2012

Time: 21.00-01.00

Address: Swedenborgsg.20

Pendel: Södra Station

Welcome…new ngoma & new sound

lunch time leo:"BIRYANI YA NYAMA YA NG"OMBE"

nyama ikiwa tayari KWA KUPIKWA


 



Vipimo Vya Masala


Nyama vipande                                     3 LB

Mtindi                                                   ½ kopo

Thomu                                                  1½ kijiko cha supu

Tangawizi                                             1½ kijiko cha supu 

Nyanya                                                2  

Pilipili mbichi                                         kiasi  

Nyanya kopo                                      4 vijiko vya supu

Vidonge supu                                      2

Pilipili nyekundu paprika                       kiasi  

Bizari zote saga                                 2 vijiko vya supu  

Viazi                                                  4

Mafuta                                             2 mug

Samli                                                ½ kikombe

Vitungu                                             6



Namna Ya Kutayarisha Na Kupika


  1. Kwenye sufuria tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, tangawizi. Mimina kwenye nyama na mtindi, tia na nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi kisha changanya  vyote pamoja weka motoni.

2.     Katika sufuria nyengine tia mafuta na samli kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi toa weka pembeni.

3.     Kanga viazi  weka pembeni.

4.     Chukua mafuta kidogo uliyokangia tia kwenye nyama  acha katika moto wa kiasi mpaka nyama iwive na maji ya punguke.

5.     Tia  viazi na vitunguu vivunje vunje tia ndani ya nyama  acha moto mdogo.


Vipimo Vya Wali 



Mchele                                                      5 mug

Maji                                                         kiasi

Chumvi                                                   kiasi

Mafuta uliyokaanga vitungu                        kiasi

Rangi ya biriani                                        ¼  kijiko cha chai

*Zafarani                                                 ½ kijiko cha chai


*roweka rangi  na zafarani kwenye kikombe na maji ¼ weka pembeni.

  
Namna Ya Kutarisha Na Kupika Wali

  1. Osha mchele roweka muda wa saa.

  1. Chemsha maji kama magi 10 hivi  na chumvi tia mchele.

  1.  Uache uchemke ukishaiva kiini nusu, mwaga maji chuja.


  1. Mimina juu ya nyama tia rangi na mafuta kwa juu funika.

Aacha kidogo katika oveni kwa muda wa dakika 20 hivi kisha epua ikiwa tayari

KATUNI MIX!

DIAMOND NA WEMA WANASWA HOTELINI



Wema.
Diamond.
Hoteli ya Giraffe walimolala Diamond na Wema.
Gari la Wema likiwa eneo la hoteli ya Giraffe.

Gari la Diamond likiwa nje ya hoteli hiyo.
Musa Mateja na Imelda Mtema
NDIVYO ilivyokuwa, staa mkali wa filamu Bongo, Wema Sepetu na mwanamuziki wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa yupo juu, Nasibu Abdul a.k.a Diamond ‘Plantinum’ wamenaswa katika hoteli yenye hadhi ya nyota tano Giraffe iliyopo Mbezi, jijini Dar es Salaam.
MESEJI YA KWANZA KWENYE SIMU YA PAPARAZI
Asubuhi ya Juni 26, 2012, ujumbe mfupi wa maneno (sms) uliingia kwenye simu ya paparazi wetu ukidondosha madai mazito kuwa, mastaa hao waliowahi kuwa wachumba na baadaye kumwagana kinomanoma, wako kwenye hoteli hiyo ‘wakiponda raha kwani kufa kwaja’.
Meseji hiyo ikafafanua: “Tena wapo toka jana, Wema yeye yupo toka alipomaliza ile shughuli yake na Omotola yule mdada wa Naijeria (Nigeria).”
MAPAPARAZI WAINGIA MZIGONI
Baada ya kupata ujumbe huo, waandishi wetu walikaa kama kamati mbele ya mhariri wao, wakaandaa zana mbalimbali zikiwemo kamera na vifaa vya kurekodia kwa ajili ya kufuatilia ukweli wa meseji hiyo.
GARI LA DIAMOND NJE YA HOTELI
Waandishi wetu walifika hotelini hapo saa 3:46 ambapo nje ya hoteli hiyo, mapaparazi hao walianza kuamini Platinum yupo ndani baada ya kuliona gari lake aina ya Toyota Prado, lakini katika kuzungusha makengeza yao hawakuweza kulitia machoni gari la Wema.
MBELE YA MAPOKEZI YA HOTELI
Mbele ya kaunta ya mapokezi, waandishi waliomba kuonana na Wema Sepetu.
Mtu wa Mapokezi: Nimwambie nani?
Musa: Mwambie baby wake.
Mtu wa Mapokezi: Baby wake yupi?
Musa: Musa Mateja.
Mtu wa Mapokezi alimtwangia simu Wema ambapo alipoambiwa ni Musa Mateja aliamuru asubiri eneo hilo mpaka atakapoitwa kwenda chumbani.
DIAMOND HUYO!
Waandishi wakiwa wamepiga kambi wakisubiri kuitwa, ghafla Diamond alishuka akiwa mbiombio kuelekea kwenye gari lake kama mtu anayewahi. Mapaparazi wetu walimfuata hadi kwenye gari ambapo alikuwa ameshaingia.
MSIKIE ALICHOSEMA
Bila kupoteza muda alisomewa mashitaka yake ‘eituzedi’ ambapo alivuta pumzi kwa nguvu kisha akafunguka:
“Mimi hata sijui kama Wema yupo hapa hotelini, kwani yupo hapa? Chumba namba ngapi? Mimi nilikuja kwenye mambo yangu, kwa sasa natunga mashairi ya wimbo mwingine kwa hiyo nilikuja tangu jana ili kufanya kazi yangu kwa ufanisi, unajua napenda kuwa sehemu yenye utulivu mkubwa.
“Unajua nini, nilikuwa Morogoro, nimerudi jana, nikaja hapa kumfuata Jeff, si unajua yule mshikaji wangu sana? Kuna wakati pia huwa nakuja pale kwenye hoteli moja ipo jirani na ofisini zenu, pale napo pazuri sana, nimewahi kulala. Ha! Ha! Ha! Musa bwana!”
MENEJA WA WEMA
Meneja wa Wema, Martin Kadinda naye alikutana na waandishi wetu ambapo alishtuka kumwona Diamond kwenye gari lake.
Martin: Khaa! Diamond unaweza kuja hapa hotelini halafu unaondoka usinitafute wakati unajua mimi nipo na tuna ishu yetu?
Diamond: (kicheko tu).
WAANDISHI WARUDI MAPOKEZI, WAITWA KWA WEMA
Baada ya kumalizana na Diamond waandishi wetu walirudi mapokezi ambapo walipelekwa kwenye chumba alichomo supastaa mwenye chemchemi za skendo Bongo, Wema na kumkuta akiwa na rafiki yake kipenzi (lakini asiyekubalika na mama yake), Snura Mushi.
Wema, baada ya kusomewa mashitaka yake alishtuka sana na kuonesha mshangao kusikia Diamond alilala hotelini hapo.
Alisema kuwa yeye ndiyo kwanza yuko kitandani na alikuwa amelala na Snura, habari ya Diamond kuwepo hotelini hapo anasikia kutoka kwa mapaparazi lakini yeye hajui chochote.
“Jamani mnavyoniona mimi hapa ndiyo kwanza nimeamka, hata nje sijatoka na watu wa kwanza kuongea nao ni nyinyi, mimi sijui kabisa kama huyo mtu yuko hapa. Kwanza alifuata nini hapa jamani?”
Amani: Sisi tulivyosikia alikuwa na wewe, sasa wewe tena unatuuliza sisi, tutajua vipi? Si ndiyo maana tumekuja?
Wema: Jamani kusema kweli… (akachukua simu na kumpigia mwanaume aliyedai ni mpenzi wake) dady, wamekuja waandishi hapa wanasema wamesikia nimelala na Diamond, we si tumeongea hadi usiku sana?
MASWALI MAGUMU
Inawezekana Diamond akafika hotelini hapo bila Wema kuwa na taarifa?
Ni kweli kwamba, Wema aliweka kambi pale kwa lengo la kujipumzisha tu akiwa na shoga yake Snura?
Utulivu anaodai Diamond aliufuata pale hotelini ulikosekana sehemu nyingine yoyote (hasa nyumbani) ikiwemo ufukweni?
Kwa nini Wema aliharakisha kumpigia simu huyo aliyemuita mpenzi wake kumwambia kuhusu waandishi kufuatilia habari ya kulala na Diamond wakati akidai walizungumza hadi usiku sana?
UKWELI UPO KWA WEMA, DIAMOND
Kwa maelezo yao hayo, bado ukweli unabaki kuwa siri yao. Hata hivyo, penzi halina siri, kama wanaficha, mapaparazi wapo macho kuwafuatilia na kama ni kweli wanatoka, siku moja mambo yatakuwa hadharani

toka GPL

MH.PINDA ASITISHA KUTANGAZA TAMKO LA SERIKALI KUHUSU MADAKTARI

 

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni na Waziri Mkuu, Pinda, alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, aliyetaka kujua Serikali ina mipango gani ya dharula ya kuumaliza mgomo huo.

Alisema kwa hivi sasa, Serikali imechukua dharula, kwa kuwaita madaktari wasitaafu kwenda kwenye baadhi ya Hospitali za Serikali, kushika nafasi maeneo ambayo madaktari waliogoma.

Vilevile Serikali imewataka wananchi waende kuhudumiwa kwenye hospitali za Jeshi, ikiwemo Lugalo.

Pinda ameseama kuwa hata yeye alipopokea taarifa kuwa Dk. Ulimboka ametekwa na kupigwa alisikitika sana, na anamuombea apone haraka ili waendelee na suluhisho la mgomo huo wa madakatari.

Alisema kuwa amemuagiza, Waziri wa Mambo ya ndani kuunda jopo la wataalamu kuchunguza kwa haraka kuhusu tukio hilo.

“Mahakama iliwaonya madaktari wasigome na waende kuvieleza vyombo vya habari kuwa vimesitisha mgomo,” alisema na kuongeza:

“Serikali ikaendelea kuwa sikivu, lakini mgomo uliendelea. Jana tena mahakama kuu ili waomba madaktari wasigome. Tungeweza kuchukua hatua stahiki lakini tulisubiri hatua za Mahakama,” alisema Pinda.

Mjadala huo ulianza baada ya kipindi cha maswali na majibu kwa Mbunge wa Mbozi Magharibi, Godfrey Zambi kuomba mwongozo na kupitia kanuni ya 68 (7)ambapo aliuliza hatua za Serikali kuhusu mgomo huo.
“Ni kweli kwamba Serikali ilishatoa taarifa hapa Bungeni na pia nilishaeleza kwamba, baada ya majadiliano ilibidi turudi kwenye chombo cha kisheria kwenda kutoa taarifa kwamba kuna maeneo hatujaridhiana,” alisema Pinda na kuongeza:

“Kauli ya Serikali ni kwamba, madaktari waheshimu amri ya mahakama…tutatoa kauli rasmi ya Serikali kesho (leo). Tumeamua kulitaarifu Bunge lako Tukufu maana kwa kweli Serikali imechukua jitihada za kutosha sasa hata waswahili wanasema "liwalo na liwe.”

Pinda alisema kuwa, Juni 22, mwaka huu , Mahakama iliwaagiza madaktari hao kusitisha mgomo na Juni 26, mahakama hiyo ilirudia kutoa amri na kwamba Serikali ilichelea kuchukua hatua dhidi ya madaktari hao kwa sababu tayari suala hilo liko mahakamani.

Katika mwongozo wake, Zambi alikumbushia taarifa ya Waziri wa Afya, Dk Hussein Mwinyi aliyoitoa Juni 22, Bungeni kuhusu madai ya madaktari ya kuboreshawa huduma zao katika hospitali karibu zote nchini.
“Nashukuru taarifa ya Serikali ilitolewa vizuri lakini kuanzia jumamosi hiyo, madaktari bila kujali taarifa ya Serikali wakaendelea na mgomo katika hospitali zote za rufaa na leo asubuhi madaktari wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamenithibitishia kuwa mgomo upo, ni madaktari mabingwa tu wachache wanaoendelea na kazi,” alisema Zambi na kuongeza:

“Nimeongea na madaktari wa Mbeya wamenithibitishia kuwa mgomo upo na taarifa hii naweza kukusomea na wabunge wenzangu, imetoka kwa daktari mmoja, kwamba mgomo upo na wanaendelea tangu Juni 23…,”
Zambi aliitaka Serikali kueleza hatua itakazochukua kwa madaktari hao kwa kuendelea kugoma bila kujali maisha ya Watanzania wanaoteseka hospitalini.

“Katika hatua hii naomba kupata mwongozo wako, Watanzania wanateseka na madaktari wanaendelea kugoma, Serikali sasa inachukua hatua gani kama suala hili liko mahakamani…. na mimi nisingeomba wabunge wasimame ili waniunge mkono tulijadili maana liko mahakamani,” alisema Zambi.

Hata hivyo baada ya Waziri Mkuu kutoa maelezo yake, Mbunge wa Ubungo John Mnyika naye alisimama na kushauri kwamba Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii nayo itoe taarifa ili kuwe na taarifa za pande mbili kabla ya kujadiliwa bungeni.

“Taarifa kutoka vyombo vya habari ni kwamba kesi iliyopo mahakamani ni ya MAT siyo Jumuiya ya madaktari… nimeiandikia barua ofisi yako… tuipokee taarifa ya kamati ya Bunge ya mambo ya jamii ili tutakapojadili tuwe na taarifa ya upande wa pili,” alisema Mnyika.

Hata hivyo Naibu Spika, Job Ndugai alisema tayari kamati hiyo ya Bunge ilishalifanyia kazi suala hilo na kwamba hakuna maana ya kurudi tena katika jambo lilelile.
mwisho

Unyama:Dk Ulimboka atekwa, aumizwa


 Send to a friend
Thursday, 28 June 2012 08:31
0digg
Waandishi Wetu
NI unyama. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka ametekwa na watu wasiojulikana, kupigwa na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili, kisha kutupwa katika Msitu wa Pande, nje kidogo ya jiji Dar es Salaam.Daktari huyo ambaye amekuwa akiratibu mgomo wa madaktari unaoendelea, aliokotwa na msamaria mwema akiwa amefungwa mikono na miguu akiwa katika hali mbaya.

Baada ya kuokotwa na wasamaria wema na kufikishwa katika Kituo cha Polisi, Dk Ulimboka aliwahishwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) kwa matibabu, na ilielezwa kuwa hali yake haikuwa nzuri.

Taarifa za kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka zilisambaa kwa kasi katika vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa simu.

Kutokana na tukio hilo, wanaharakati wa haki za binadamu wameituhumu Serikali kuhusika na tukio hilo, huku Serikali ikikana tuhuma hizo, na papohapo ikiagiza Jeshi la Polisi kuwasaka waliohusika.

Akisimulia mkasa huo kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM, Dk Ulimboka alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika klabu ya Leaders jijini Dar es Salaam, alikokuwa na wenzake wawili.

Alisema baada ya kukaa kwenye baa hiyo kwa muda, alianza kujisikia vibaya tofauti na siku zingine.

"Mara, katikati ya maongezi tukaona mtu anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk. Ulimboka)," alieleza na kuongeza,

"Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini ilikuwa haina namba."

Taarifa zaidi zilizolifikia Mwananchi kutoka Moi alikolazwa kwenye chumba cha uangalizi maalumu, zilieleza kuwa baada ya uchunguzi, ilibainika kuwa daktari huyo aliteswa vibaya, ikiwamo kuumizwa sehemu za siri, kuvunjwa meno kadhaa, mbavu na miguu.

Habari zaidi zilisema kuwa, baada ya kufikishwa katika Msitu wa Pande na kupata kipigo, alizimia kwa muda na alipozinduka aliwachomoka watekaji hao na kujaribu kukimbia.

Msitu wa Pande ulioko wilayani Kinondoni, ndiko wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva teksi wa Manzese Dar es Salaam waliuawa na polisi mwaka 2006.

Chanzo chetu cha habari kilisema, baada ya Dk Ulimboka kujaribu kuwatoroka watekaji, walipiga risasi mbili hewani, aliposimama wakamshika na kumpa kipigo na mateso zaidi, hivyo kusababisha avunjike maeneo mbalimbali ya mwili.

Polisi waunda tume
Jeshi la Polisi limeunda jopo kuchunguza tukio la utekaji nyara na shambulio la kudhuru mwili wa Dk Ulimboka.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema jana kuwa tukio hilo ni la aina yake na kwamba halijawahi kutokea hapa nchini.

Alisema jopo hilo ambalo linaongozwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ahmed Msangi linahusisha wapelelezi wa fani mbalimbali.
“Ni issue (jambo) ambayo imetokea bila kutegemea katika namna ambayo ina utata, hivyo kazi yetu ni kutegua utata huo,” alisema Kova na kuongeza:
“Hatutaki katika nchi yetu matukio kama haya yawe ya kawaida, tunataka liwe la mwanzo na la mwisho.”

Kamanda huyo alisema yeye alipata taarifa za kutekwa Dk Ulimboka usiku wa kuamkia jana saa 7 usiku.

Kwa mujibu wa Kamanda Kova, Dk Ulimboka aliokotwa na raia mwema katika eneo la Msitu wa Pande jana saa 2:30 asubuhi karibu na barabara huku akiwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili, ikiwamo kichwani na mikononi.
Alisema raia huyo (jina limehifadhiwa) alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Bunju, na askari walikwenda kwenye gari la raia huyo na kumkuta Dk Ulimboka wakamchukua na kwenda naye ndani.
 Kova alisema: “Aliyemuokota alisema alimkuta amefungwa mikono na miguu, na inaonekana kama watu hao walikuwa wanalipiza kisasi.”
Kwa mujibu wa kamanda huyo, akiwa kituoni hapo, Dk Ulimboka alijieleza kwamba juzi saa 5:30 usiku akiwa katika klabu ya Leaders na wenzake wanapata vinywaji pamoja na wateja wengine, walikuja watu watano na kuwatishia.
Alisema watu hao waliwataka walale chini na kwamba walitii, kisha watu hao walimchukua Ulimboka na kuwaambia wengine waendelee na vinywaji.
“Ulimboka alisema watu hao walikuwa na gari aina ya Escudo lenye rangi nyeusi na hili gari halikuwa na namba na walichukua ufunguo wake wa gari, nyaraka kadhaa na hela alizokuwa nazo,” alisema Kova.
Alisema akiwa katika gari hilo na watu wengine watano, ghafla walianza kumpiga huku wakiwa hawasemi chochote na kwamba baadaye walimfunika kichwani na fulana nyeusi hadi Msitu wa Pande.
Kova alisema baada ya maelezo hayo, Dk Ulimboka alitoa namba za simu za rafiki yake Dk Deogratius, na baada ya hapo alipewa fomu ya matibabu (PF3) na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu.
Kamanda huyo alitoa wito kwa wananchi na mtu yeyote mwenye taarifa kamili kuhusu tukio hilo atoe taarifa, kwani lisipojulikana vizuri linaweza kuzua minong’ono mingi.
Askari ajeruhiwa MNH
Katika hatua nyingine, Kova alisema watu wasiojulikana wamemjeruhi Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi cha Selander Bridge ambaye alikwenda MNH kufanya upelelezi wa tukio hilo.
Kwa mujibu wa Kova, Mkuu huyo wa upelelezi alijeruhiwa wakati akiwa anaongea na simu, na kwamba watu hao pia walimpora vitu alivyokuwa navyo ikiwemo simu.
Mkurugenzi Moi

Mkurugenzi wa Tiba katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), Cuthbert Mchalo alisema majeruhi huyo alifikishwa hospitalini hapo saa 4:25  asubuhi, kwa msaada wa gari la wagonjwa la Kampuni AAR, kutoka Kituo Kidogo cha Polisi Bunju.

“Tumempokea, anaendelea vizuri na amepata maumivu katika maeneo ya kifuani, kichwani na tumboni,” alisema na kuongeza kuwa taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

Alifafanua kwamba kwa sasa wanajitahidi kumpatia matibabu, ingawa alipelekwa hospitalini hapo akiwa katika hali ambayo siyo nzuri, na uchunguzi zaidi unaendelea.

Wanaharakati walaumu Serikali
Miongoni mwa watu wa kwanza kufika katika Kituo cha Polisi Bunju kumuona Dk Ulimboka ni Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba ambaye alisema kilichotokea kinaonyesha jinsi gani Serikali ilivyo na woga katika kushughulikia  matatizo ya wananchi.

Dk Bisimba alisema wao wanaamini kuwa tukio hilo lina mkono wa Serikali na kama ni kinyume cha hapo, basi inapaswa kuwaridhisha wananchi kuwa hawana mkono wao katika sakata hilo.

“Kama wao hawana mkono wao basi wanapaswa kuwaridhisha wananchi kuwa hawahusiki kwa kuwatia mbaroni wahusika na kuwafikisha katika vyombo vya sheria,” alisema Bisimba.

Mkurugenzi huyo alisema matamshi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda bungeni jana kuwa wanashughulikia suala la madaktari na watalimaliza liwalo na liwe inaleta tafsiri kuwa kilichotokea kina mkono wao.

“Alivyosema liwalo na liwe na kinachotokea sasa kinabainisha kuwa mengi zaidi yatafuata,” alisema Bisimba na kuongeza kuwa hali hiyo inasikitisha na haikuwahi kufikiriwa.

Bisimba alisema baada ya wasamaria kumkuta mnamo saa 12:00 asubuhi, walimpeleka katika kituo kidogo cha Polisi cha Bunju ambako polisi walifungua mashtaka ya wizi wa maungoni na kupatiwa RB yenye namba BJ/RB/1870/2012.
“Mimi nilipata taarifa za kutekwa kwake kutoka kwa mwenzie aliyekuwa naye mnamo saa nane usiku, na baada ya kupata taarifa hizo niliwaeleza wanaharakati wenzangu juu ya hatua za kuchukua,” alisema Bisimba.

Bisimba alisema aliwasili katika Kituo cha Polisi cha Bunju, jana mapema asubuhi na kumkuta Dk Ulimboka akiwa amejeruhiwa vibaya, lakini hakuwa amepatiwa huduma yoyote.

“Tulikwenda kumchukua na kukuta hali yake ni mbaya, lakini cha ajabu pamoja na majeraha yote hakupatiwa msaada wowote wa huduma, jambo ambalo lilitusikitisha sana,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sikika, Irenea Kiria alisema kilichotokea ni kitu kibaya na kinaonyesha jinsi gani Serikali inavyoshughulika na watu, badala ya kujali hoja za msingi ambazo zinawasilishwa.

Kiria alisema hoja za madaktari zilipaswa kusikilizwa kwani licha ya madai ya masilahi yao lakini pia wanapigania mazingira bora yenye utu kwa ajili ya wagonjwa.

Madai mengine ni upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa ajili ya kuwahudumia wananchi pamoja na upatikanaji wa dawa, mambo ambayo alisema hayahitaji mjadala.

“Suala la masilahi ya madaktari linazungumzika lakini siyo suala la dawa, mazingira bora ya kuwahudumia wagonjwa na upatikanaji wa vifaa tiba na vipimo vingine,” alisema Kiria.

Nchimbi: Tutawasaka
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi alisema Serikali imeliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka na kuwachukulia hatua watakaobainika kuhusika na utekaji huo.

Dk Nchimbi alisema mjini Dodoma kuwa Serikali haihusiki kwa namna yoyote ile na utekaji nyara huo, na kwamba kitendo hicho kinapaswa kulaaniwa kwani hakikubaliki katika jamii hasa kwa zama hizi.

“Kwanza, madaktari ni watu muhimu ambao wao ndio wanaotuwezesha sisi kuishi, kwa hiyo wapo kwa ajili ya maisha yetu, hata kama asingekuwa daktari, kwa mtu yeyote yule, jambo hili halikubaliki katika nchi yetu,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:

“Tumewaagiza polisi wafanye uchunguzi ili kuwabaini wahusika na wakipatikana wafikishwe katika vyombo vya sheria, maana hatuwezi kwa namna yoyote kuvumilia vitendo vya aina hii.”

Alisema Serikali imestushwa sana na tukio hilo na haitavumilia kwa namna yoyote vitendo hivyo pamoja na vile vya unyanyasaji kwani ni kinyume cha sheria.

Kuhusu kupigwa kwa Mkuu wa Upelelezi (OC- CID), ASP Mukiri, Dk Nchimbi alisema lilikuwa ni tukio la bahati mbaya kwamba madaktari waliokuwapo Muhimbili walishindwa kuwa na uvumilivu kwani askari aliyepigwa alikuwa ameagizwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela kwenda kufuatilia matibabu ya Dk Ulimboka.

“Hapa ndipo ninapotofautiana na watu wengi, mnampigaje polisi, maana yule anapaswa kuwa rafiki wa raia, sasa unampigaje mtu ambaye ni mlinzi na umemwajiri, analipwa kwa kodi yako?” alihoji Dk Nchimbi.

Yaliyojiri bungeni
Tukio hilo lililosambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari, liliibuka bungeni, ambako Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alilaani vikali kitendo cha watu wanaodaiwa ni maofisa wa vyombo vya usalama kumpiga Dk Ulimboka.Alisema kitendo hicho ni unyama unaostahili kukemewa na kila mpenda amani hapa nchini.

“Tumestushwa na tukio hilo na tunalaani vikali kitendo hicho na kumwombea Dk Ulimboka ili apone haraka,” alisema Mdee.Katika hatua nyingine, Mwananchi lilitembelea hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana, kujionea hali ilivyokuwa baada ya kusambaa kwa taarifa za kupigwa kwa Dk Ulimboka.
Katika hospitali ya Mwananyamala, wengi walioonekana walikuwa ni wauguzi huku madaktari wakidaiwa kwenda katika hospitali ya Muhimbili kumuona mwenzao aliyejeruhiwa.
Dk Ulimboka aliwahi kufanya kazi katika hospitali hiyo ya Mwananyamala katika miaka ya nyuma.

Hata hivyo, juhudi za waandishi kuzungumza na uongozi wa hospitali hiyo, hazikufanikiwa baada ya wafanyakazi wa Ofisi ya Mganga Mkuu kusema kuwa mganga huyo amekataa kuzungumza, akiwataka waandishi wafike ofisini kwake leo.
“Ameniambia niwapeleke kwa katibu wake, lakini na yeye nimemkosa, sasa nimerudi kwake ameniambia niwaambie mrudi kesho,” alisema katibu muhtasi wake.
Katika hospitali za Temeke na Amana, hali pia ilikuwa hivyo, baadhi ya wahudumu waliokutwa katika hospitali hizo wakikataa kuzungumza kwa madai kuwa wanaotakiwa kuzungumza hawapo.

Madaktari jeshini waitwa kazini
Taarifa zilizotufikia wakati tukienda mitamboni, ambazo hazijathibitishwa, zilieleza kwamba madaktari wote wanaofanya kazi kwenye hospitali za jeshi ikiwamo Lugalo ambao hawakuwa zamu jana jioni, waliitwa kazini, tukio ambalo linahusishwa na tamko la Serikali linalotarajiwa kutolewa leo.

chanzo:mwananchi

Tuesday 26 June 2012

Miss Africa Crown International 2012 Application Deadline: 1st July


  1. Jazmine from Zambia is in the big race

    This is to notify the general public that application for the 3rd Miss Africa Crown Scandinavia will close down on Sunday, July 1st 2012. According to Duke Philip Gomez, a top official of the Ritz Society which organizes the Miss Africa Crown International, interested applicants who shall not have submitted their applications by July 1st will count themselves out of the competition.

    So far, a record 32 applicants have submitted their applications which are currently being processed. An elegant presentation of the contestants will be held on Saturday, 7th September 2012 at Alvik Medborgahuset from 21.00-04.00 hrs followed by a huge boogie that will feature top Africa-Stockholm artists who have consistently been rocking the Africa-Stockholm Entertainment scene without a stop.

    Contestants who wish to apply for the 2012 Miss Africa Crown are kindly requested to hurry up and beat the deadline because as opposed to the situation last year, there will be no extension for applications and late applicants will be rejected. Application can be done directly through the Miss Africa Crown website.

    Once the application is closed, the next stage will be to begin the process of orientating the contestants on basic routines and regulations of the contest. This includes meeting the Miss Africa Crown International Management Team, a briefing of the event’s structure, signing of contracts, photo-shoots, casting of promotional video clips and meeting the Judges before an intensive training by beauty pageant experts begins in earnest.

    During the last two contests, the Management of Miss Africa Crown has learnt a lot of lessons. The experience gained out of past events will help improve this year’s contest whose final will be held aboard Siljaline during a 48hr cruise across the Baltic sea. It is the first time that the event will be held over a 48 hr period across the Baltic.

    Experience has shown that the traditional 24 hour Cruise is not enough and, in increasing the amount of hours for the event, the view of Miss Africa Crown’s management team is that there will be more time to mix relaxation and competition during the cruise. Last year, the Judges had very little time to decide on the winner due to shortage of time. This time, the Judges will have no excuse because there will be plenty of time for them to take breaks, drink coffee and consult adequately before a winner can be pronounced.

    Sound of Blackness to rock the crowd
    An interesting angle is that this time around, a group of contestants will come from London where a Pre-selection of top beauties in the city of London is scheduled this summer. Qualifiers from britain will then clash with their Scandinavian counterparts during the finals at the prestigious Siljaline. With enthusiastic fans coming all the way from London to sample the Stockholm beauties, the event is expected to be the biggest ever. Arrangements are being made to ensure that the whole boat, which has a capacity of 2500 revellers, is fully booked for the event.

    Among the top Judges are Ms Mbova N. Lillian, an accomplished Kenyan diplomat, Justina Mutale, founder & CEO of Perryfield Promotions, Shaul Moalem, Make-Up Artist Director of the, Make Up Institute in Stockholm and Mrs. Brawer Madina, an English Teacher in Stockholm. Discussions are underway with the top-most Kenyan artist in Europe, St James, to play a role during the event. For further information about the Judges, vist the Miss Africa Crown website.

    On the Entertainment front, Sound of Blackness will be blasting the music until the loud speakers blow up into small pieces while the official MC will be none other than the electrifying Joseph Mbaazira of the re-known online based Ugamuzik Radio fame currently running into its third anniversary. We wish him good luck!

    In 2010, the big prize of Miss Africa Crown was scooped by Ms. Michelle Jeng from Tanzania while last year, Jessle from Ugandan beat all contestants to emerge the winner. The winning prize included: a ticket to Africa (any country of choice) which was sponsored by the Ethiopian Airlines; a 500 Euro cash prize, a Louis Vuitton bag (worth SEK 5.000), a photo-shoot by the Make-Up Institute, a make-up kit and a Champaign to boot!

    The prizes, which included other prizes like Miss Photogenic, Miss Elegant, Miss Personality just to mention but a few, were all delivered to the winners during a colourful ceremony which was held in Stockholm and which was attended by tens of Miss Africa Crown fans. The same prizes for the winners apply this year.

    The Management of Miss Africa Crown International appeals to all fun-lovers to support the event so that it can continue to succeed as the struggle to show-case African beauty globally also continues. It will be a perfect opportunity to combine entertainment, leisure and loads of fun, all in the boat across the Baltic before the Miss Africa Crown International beauty queen for 2012 is finally announced. Further details of the event can be accessed at the Miss Africa Crown website. The Ritz Society