Monday 30 July 2012

KARUBANDIKA LIVE STOCKHOLM-MAKONDE BAND&SAMMY KASULE

GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

                       

TAMKO LA SERIKALI
GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA
            Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia kutochapishwa gazeti la MwanaHalisi kuanzia 30 Julai, 2012 kwa muda usiojulikana kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchochezi, uhasama na uzushi likiwa na nia ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya dola hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.
            Katika matoleo yake hivi karibuni, gazeti la MwanaHalisi toleo Na. 302 la Jumatano Julai, 11 – 18, 2012 na toleo Na. 303 la Jumatano Julai 18 – 24, 2012 na toleo Na. 304 la Jumatano Julai 25 hadi 01 Agosti, 2012 na mengine yaliyotangulia yamekuwa yakichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.
            Mhariri wa gazeti la MwanaHalisi, ameitwa na kuonywa mara nyingi, lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.
            Mhariri, mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi yetu ambacho kinatoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutonukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru.
            Uamuzi wa Serikali
            Serikali imeamua kulifungia kutochapishwa kwa muda usiojulikana gazeti la MwanaHalisi, kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976, kifungu Na. (25) (i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa Tangazo la Serikali (Government Notice) Na. 258 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Julai, 2012.
             Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari katika kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.
            Kama ilivyoelezwa Bungeni wakati wa kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni waandishi na watangazaji wa habari wanatakiwa kuhakikisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoandaa vinazingatia  taaluma na kuweka mbele maslahi ya Taifa letu na uzalendo. Uhuru na haki ya vyombo vya habari uendane na wajibu.
            Kuanzia sasa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo kwa maksudi vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu uliopo nchini mwetu.
Imetolewa na
OFISI YA MSAJILI WA MAGAZETI
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
30 Julai, 2012

Uganda's Yoweri Museveni warns of Ebola threat


Breaking news
Uganda's President Yoweri Museveni has called on people to avoid physical contact, after the deadly Ebola virus spread to the capital, Kampala.
Fourteen people have died, including one in Kampala, since the outbreak began in western Uganda three weeks ago, he said in a special broadcast.
Ebola is one of the most virulent diseases in the world.
It is spread by close personal contact and kills up to 90% of those who become infected.
Mr Museveni said health officials were trying to trace everyone who had had contact with victims so that they could be quarantined.
People should avoid shaking hands, kissing or having sex to prevent the disease from spreading, he added.
Mr Museveni said relatives and friends should not bury anyone who is suspected to have died of Ebola.
"Instead call health workers because they know how to do it," he said.
Mr Museveni said seven doctors and 13 health workers at Mulago hospital - the main referral hospital in Kampala - are in quarantine after "at least one or two cases" were taken there.
One victim later died.
"I wish you good luck, and may God rest the souls of those who died in eternal peace," Mr Museveni said, as he ended his address to the nation

bbc

Dekula Band"Ngoma Ya Kilo"present's Lady Neema ft.Gabby,Bobo & Sella


 
Akadevu-Music present's
Lady Neema ft.Gabby,Bobo & Sella
Dekula Band"Ngoma Ya Kilo"
Place:Lilla Wien"Little Nairobi"
Date:03-04/10-11 August 2012
...

SAKATA LA GPL NA CHAMELEON LINAENDELEA,SOMA HAPA


Joseph Mayanja ‘Chameleone’.
Na Saleh Ally
KUMEKUWA na maswali mengi sana kuhusiana na mgogoro ulioibuka kati ya Kampuni ya Global Publishers (GPL) na msanii Joseph Mayanja ‘Chameleone’ wa Uganda ambaye anadaiwa dola 3,500 (zaidi ya Sh milioni 5) alizochukua halafu hakuzifanyia kazi.
Global iliingia mkataba na Chameleone kupitia wakala wake aitwaye George kwa ruhusa ya Chameleone mwenyewe. Mganda huyo alikubali GPL iingie mkataba na wakala huyo kwa niaba yake ili aje nchini Julai 7, kutumbuiza katika Tamasha la Usiku wa Matumaini kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Msanii Kidumu raia wa Burundi, ndiye aliiwakilisha GPL na baada ya kuwasiliana na Chameleone, walikutana naye akamtambulisha George. Baada ya kuingia mkataba huo, dola 3,500 ambazo zilikuwa za utangulizi zikatolewa maana msanii huyo alitaka dola 5,000 katika malipo yote. Baada ya hapo maandalizi yakiwemo matangazo ya tamasha hilo yakaendelea.
Alipoanza kuulizwa kuhusiana na kuja, Chameleone akagoma kwa madai kwamba George hakumpa fedha! Alipoulizwa kwamba yeye ndiye alimtambulisha wakala huyo, sasa vipi liwe tatizo la GPL? Akasisitiza haelewi lolote na hatakuja.
GPL ilishaanza matangazo, hivyo ikaona ni vizuri kuzungumza naye upya ili imlipe tena dola 5,000. Ajabu, safari hii akageuza bei, akasisitiza kama wanamhitaji, wamlipe dola 8,000 (zaidi ya Shilingi milioni 12) na si kwa advance, alitaka alipwe yote.
Kwa ajili ya kulinda heshima kwa kuwa GPL ilishatangaza kuwa atakuwepo katika tamasha, meneja wake Abdallah Mrisho, akafunga safari hadi Kampala na kumlipa Chameleone kitita cha dola 8,000. Mkataba mpya ukatengenezwa, ule wa mwanzo ukaendelea kuwepo.
Chameleone alitua nchini kwa ajili ya shoo, safari hii GPL ikiwa imelazimika kulipa tiketi za ndege za watu watatu badala ya wawili kama yalivyokuwa makubaliano ya mwanzo. Alipewa Range Rover Vogue ambalo alilitumia kwa safari zake zote akiwa hapa nchini.
Alifikia katika hoteli inayomilikiwa na GPL. Baada ya shoo, uongozi wa GPL ulitaka kujua kuhusiana na fedha za mkataba wa kwanza ambazo Chameleone alitoa maagizo wakala wake asaini mkataba huo halafu baadaye akaruka. Yakatokea mabishano, naye akaondoka hotelini hata bila ya kuaga.
Kawaida katika hoteli hiyo kumekuwa na utaratibu wa kuhifadhi pasi za kusafiria za wageni, baada ya kutokea matatizo kadhaa na wateja kutoka nje ya nchi. Baada ya kuondoka, siku iliyofuata Chameleone alituma mtu arudie pasi zake akidai yeye alikuwa Zanzibar katika tamasha.
Uongozi wa hoteli uligoma kuzitoa hadi afike mwenyewe, naye akagoma kwa madai hana shida kwa kuwa anajua zitapelekwa. Baada ya hapo, ndiyo akarejea kwao kufuatia kupata pasi za kusafiria kutoka ubalozi wa Uganda nchini. Mbaya zaidi akavamia ubalozi wa Tanzania nchini Uganda na kufanya vurugu akidai pasi zake.
Kwa kuwa uongozi wa hoteli ulikabidhi pasi ya kusafiria ya Chameleone kwa uongozi mkuu, nao siku chache baadaye ukazikabidhi kwa serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Baada ya hapo, jambo hilo limezidi kupasua anga huku baadhi ya watu wakionekana kulikuza bila ya kujua lolote linaloendelea. Ili mradi wamerukia tu huku wakitangaza eti, pasi ya kusafiria ya Chameleone ni ya kidiplomasia kwa kuwa alipewa na Rais Yoel Museven, kitu ambacho ni uzushi mtupu tena usiokuwa na maana.
Wapo wanaotangaza eti GPL imemtapeli Chameleone, kivipi? Wakati yeye ndiye amefanya utapeli kupitia wakala wake George, utaratibu ambao amekuwa akiutumia kwa watu wengine ambao amewahi kuwatapeli. Chameleone maana yake ni kinyonga, mnyama ambaye ngozi yake inaweza kubadilika rangi kutokana na mazingira aliyopo, ndicho anachokifanya.
Kwa nini yeye?
Jiulize mara mbili au tatu kwamba kwani ni mara ngapi GPL imewahi kufanya kazi na wasanii wa nje bila ya kuzuka mgogoro wowote? Hata Chameleone mwenyewe hajalalamikia malipo kutoka GPL, badala yake kampuni ndiyo inamlalamikia yeye kwa utapeli.
Kumjua George:
GPL ingeweza vipi kufika kwa George bila ya kutambulishwa na Chameleone mwenyewe? Yeye ndiye alimtambulisha George kwa Kidumu aliyekuwa mwakilishi wa GPL, kwamba aingie naye mkataba kwa kuwa ndiyo utaratibu wake anaoutumia kwa mawakala. Kama kweli George hakumpa Chameleone fedha, vipi tatizo liwe la GPL?
Kenya v Uganda:
Rekodi zinaonyesha Chameleone hafanyi shoo Kenya na hasa Nairobi, ikitokea akaenda huko, basi atalazimika kuwa chini ya ulinzi mkali. Yote ni kutokana na utapeli mkubwa ambao ameufanya huko kwa zaidi ya mara moja. Wakenya aliowatapeli, wote alitumia mfumo huohuo wa wakala.
Angalia Wakenya namna walivyokuwa wakali na kushikilia msimamo wa kutaka haki zao zilipwe, hapa nyumbani Watanzania wanadai haki yao kwa Mganda huyo lakini wanaopiga vita tena kwa juhudi kubwa ni Watanzania wenzao! Yote hiyo ni chuki, ndiyo maana wapo wanaothubutu kunyoosha mkono kwa GPL bila hata kujua chanzo cha tatizo, yote hiyo kwa kuwa Watanzania wengi chuki ndiyo msingi unaotuongoza!
DJ JD:
Ameibuka na kusema aliwahi kutapeliwa na Chameleone dola 3,000 (zaidi ya Sh milioni 4.5), hiyo ilikuwa mwaka 2004. Hadi leo amekuwa akipiga chenga kumlipa na kuna wakati alimwambia aandae onyesho aje atumbuize ili wawe wamemalizana, akafanya hivyo na kwa mara ya pili hakutokea tena!
Wapo ambao wanaamini Chameleone hawezi kufanya utapeli, wanaona ni mtu ‘smati’ sana. Huenda amefanya upuuzi huo sehemu nyingi lakini hakuwahi kukutana na watu wanaojua kudai haki yao na wasiokubali kukaa kimya kwa kuhofia kelele za watu wengi ambazo unaweza kuzilinganisha na za chura.
JD aliwahi kumkimbiza Chameleone kama mwizi alipokuja hapa nchini, alitaka kumtia nguvuni katika mikono ya Jeshi la Polisi. Lakini DJ huyo anasema Merrey Balhabou na Rita Poulsen walimuombea msamaha wakidai atamlipa, naye akaahidi hivyo, hadi leo changa la macho. Kula fedha za bure kuna utamu wake, lakini mwisho wake utakuwa mbaya kwake.
Biashara:
Kuna mpango, kampuni moja ambayo hufanya masuala ya burudani, imeonyesha kufurahia sana kutokea kwa utapeli huo wa Chameleone. Inachofanya sasa ni kulikuza suala hilo kwa nguvu zote, kwanza ni kama faraja kwao kusikia GPL inaingia katika mgogoro kwa kuwa wamekuwa na mafanikio makubwa katika matamasha yao ukilinganisha na wao ambao hufanya kwa msimu maalum.
Kuna taarifa wanataka kulikuza zaidi suala hilo ili baada ya muda Chameleone awe gumzo halafu wamlete wao nchini kutumbuiza. Hivyo, kwa kutumia vyombo vyao na watu wa kutengeneza katika mitandao, wamekuwa wakilikuza na kusukuma kashfa nyingi, taarifa tunazo na nguvu ya kupambana nao hadharani na ikiwezekana mafichoni, tunayo.
Kawaida ya Watanzania huona kila kilicho nje ya nchi ni bora zaidi, ndiyo maana hadi leo wengi hawaamini kwamba Uwanja wa Taifa ni mzuri na bora kuliko viwanja vingine ndani ya Afrika Mashariki na Kati. Huenda kingekuwa Uganda au Kenya, basi wangeambiwa ni bora wangekubali.
Huo ni utumwa wa mawazo na kuwapa nafasi wale wanaoamini wao ni bora kwa hisia na kwa kuwa wanakuzidi kuzungumza Kingereza tu, basi unaamini kweli wao ni bora. Tuache uwoga, hapa GPL tunaheshimu lakini hatuhofii yeyote yule hata chembe, tena hasa unapofikia wakati wa kudai haki yetu ambayo tunaamini tunastahili kuipata, sisi ni Watanzania.

GPL

Saturday 28 July 2012

SHIGONGO AFUNGUKA KUHUSU SCANDAL YA CHAMELEON


Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric Shigongo(kati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya msanii huyo na kushoto ni Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho.
Baadhi ya wanahabari wa vyombo mbalimbali vya habari wakimsikiliza kwa makini Eric Shigongo.
JD akisisitiza jambo (kulia) Juma Mbizo, Mratibu wa Matamasha.
Eric Shigongo (kulia) akisikiliza maswali kutoka kwa waandishi wa habari.
MD wa Global Publishers Ltd, Eric Shigongo, mapema leo ameongea na media kuhusu madai ya Jose Chameleone kudai paspoti yake, ambaye jana alikwenda Ubalozi wa Tanzania nchini kwake Uganda kushinikiza kurejeshewa paspoti yake.
Eric amefunguka kwa kusema kuwa, kampuni yake na msanii huyo waliingia makubaliano ya kufanya shoo kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini, liliofanyika Uwanja wa Taifa Julai 7 mwaka huu, ambapo katika mazungumzo ya awali, msanii huyo aliomba kulipwa dola 5000 na kulipiwa tiketi 2 za ndege ili kuhudhuria tamasha hilo, masharti ambayo yalikubaliwa.
 Mazungumzo hayo ya awali yalifanyika kati ya Global Publishers na agenti wa Chameleone ajuliikanae kwa jina la George. Kabla ya kutuma fedha hizo, kampuni yake ilihitaji kujiridhisha kama ajenti huyo alikuwa kweli anawasilina na kukubaliana na Chameleone kuhusu shoo ya Dar, ili kuepuka utapeli.
 “Tulipokubaliana nae kupitia ajenti wake, tuliamua kwenda mbele zaidi ili kujiridhisha, ambapo tuliwasiliana na mwanamuziki Kidumu ambaye anamfahamu huyo George na kwenda mpaka Kampala kukutana ana kwa ana na wahusika, kwa niaba yetu”, alisema Shigongo.
 Akielezea zaidi, Shigongo alisema kuwa Kidumu alikwenda Kampala na kukutana na George pamoja na Jose Chameleone, ambaye alikubali kuja kufanya shoo na kumruhusu Kidumu kusainishana mkataba na ajenti wake na kumpatia hizo fedha.
 “Chameleone alitoa ruhusa kwa ajenti wake kusaini mkataba na kupokea advace ya dola 3,500 kwa niaba yake kwa madai kuwa yeye asingeweza kusubiri malipo wakati huo kwa sababu alikuwa anawahi sehemu nyingine.
 “Baadae Jose alikuja kugeuka na kudai hakupewa hizo pesa na ajenti wake, kitu ambacho kilonekana kama mchezo wa kitapeli kati ya Chameleone na ajenti wake kwetu sisi.
 “Kwa kuwa ujio wake Tanzania ulikuwa umeshatangazwa sana, uongozi wa Global Publishers, ulilazimika kufanya mazungumzo mengine na Chameleone na kumuomba sana kuja nchini kufanya shoo, ambapo this time akakubali kwa masharti ya kulipwa dola 8000 na tiketi nne za ndege.
“Ndugu zangu, sikua na jinsi, nililazimika kumkubalia na kumlipa dola 8000, kwa sababu tayari tamasha lilikuwa limeshatangazwa sana, billboards zimewekwa barabarani na promosheni kubwa ilikuwa inafanyika,” alisema Shigongo kwa uchungu.
Hivyo mara baada ya kukubaliana, safari hii akalazimika kumtuma meneja wake kwenda mpaka Kampala na kukutana na Chameleone ana kwa ana na kumpatia dola 8000 na kusaini mkataba mwingine wa pili.
“Ni dhahairi kabisa alichokifanya Chameleone kilikuwa ni utapeli kwa kushirikiana na ajenti wake, kwa sababu tunamuamini Kidumu ambaye tumeshafanya naye kazi mara Kadhaa kwa uaminifu mkubwa. Pia ni Chameleone ndiye aliyemuidhinisha ajenti wake kuchukua pesa hizo, hivyo ulikuwa ni mchezo wa pamoja,  na hiyo ni tabia ya Chameleone, kwani ameshawafanyia mapromota wengi kiasi kwamba hivi sasa hakanyagi nchini Kenya.
 “Dola 3,500 siyo fedha nyingi, ningeweza kuzisamehe, lakini nimeamua kuzidai kwa manufaa ya watu wengine, Watanzania tusikubali kufanywa wajinga kwa sababu ya upole wetu, tutaendelea kudhauriwa na kufanywa wajinga mpaka lini,” alihoji Shigongo.
Mwisho Shigongo alitoa wito kwa Watanzania kuungana katika suala hili, kwani Chameleone ameonesha dharau kubwa kwa Watanzania kwa kumfuata balozi wetu nchini Uganda na kuondoka ofisi kwake huku akisonya na kubamiza mlango, akiendelea kuonesha dharau kwa Watanzania wote wapatao miloni 40!

GPL

Friday 27 July 2012

KALI YA EXTRA BONGO NIIPENDAYO,TUONANE PALE WADAU

     



                                  
                                                      I LOOOVE THIS SONG, HASA VERSE"
"HAKIKA KIPENDA ROHO,HULA NYAMA MBICHI,NA UKUMBUKE KILA SHETANI NA MBUYU WAKE,MIMI KUMPENDA YEYE WENGINE WANACHUKIA,MIMI KUMPENDA YEYE WENGINE WANANONGONA"

WADAU WA STOCKHOLM NA VITONGOJI VYAKE TUKUTANE TENA BADAEEE AAH BADAEEE KULEE EXTRA BONGO VÄSTBERGA ALLE

                                             WEEK END NJEMA WADAU


NYIMBO KALI UTAZOSIKIA LEO LIVE STOCKHOLM TOKA EXTRA BONGO


LAPTOP

MTAJI WA MASKINI


MJINI MIPANGO



TODAY"S PHOTO


                    "kisanolaaaa eeeh mameee tateee sanola sanolaaaaa tulemonde kisanolaaaaa eeeeh "

ukiwa na watoto 10 kama hawa huna haja kupeleka shule,ni kuleta magitaa na vyombo tu kuanzisha bendi

LONDON 2012 SHEREHE ZA UZINDUZI ZANUKIA



Mwenge wa Olimpiki, London 2012
Baada ya tetesi kuzuka kuhusiana na maandalizi ya michezo hiyo, waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amesema michezo ya mwaka huu itathibitisha kuwa Uingereza ina uwezo wa kufanya maandalizi kabambe.
Lenye Ijumaa ndiyo siku ya ufunguzi rasmi wa mashindano yatakayopeperushwa moja kwa moja kote duniani.

Bwana Cameron ametetea maandalizi ya mashindano hayo baada ya mgombea wa kiti cha urais nchini Marekani Mitt Romney kusema kwenye mahojiano katika runinga ya NBC kwamba kuna matatizo katika usalama na tishio la mgomo wa maafisa katika maeneo ya mipakani.
Lakini baadaye bwana Romney alitabiri kuwa mashindano ya Olimpiki mjini London yatakuwa yenye mafanikio baada ya kukutana na waziri mkuu huko Downing Street.
Hapa Bw. Cameron aliukaribisha mwenge huo wakati uliposimama kwa muda ukiwa njia kuelekea Kasri la Buckingham.
Mwanamfalme William, mkewe na mwanamfalme Harry walikuwepo kuwakaribisha waliokuwa wakiiperusha mwenge huo kabla ya kupelekwa Hyde Park.
Meya wa mji wa London Boris Jonnson akizungumza mbele ya umati mkubwa wa watu 60,000 waliojitokeza kushuhudia sherehe hiyo aliwatakiwa kila la heri na kusema ''mashindano ya London yatakuwa ni ya kukata na shoka.''
Lakini pia alizungumzi mzozo uliokuwepo awali aliposema mbele ya umati huo: "kuna mtu anayeitwa Mitt Romney ambaye anataka kujua ikiwa tuko tayari. Tuko tayari? Ndiyo tuko Tayari!"

BBCSWAHILI

WEMA APATANISHWA NA MAMAKE

Na Shakoor Jongo
KATIKA kukamilisha mfungo wake wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ amekubali kupatanishwa na mama yake mzazi, Miriam Sepetu, hivyo kukamilisha usemi kuwa mtoto hakui kwa mzazi wake, Ijumaa limeshiba.
Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Wema, baada ya staa huyo kutofautiana na mama yake kisa kikiwa ni mahojiano aliyofanya mzazi huyo runingani ambayo hayakumpendeza Wema, hivi karibuni wamekutanishwa na kurejesha amani iliyokuwa imetoweka kati yao.
“Mimi najua undani wa ishu nzima, tangu yale mahojiano na nyiye (Global) mkaandika kuwa mama Wema alimtia aibu mwanaye, hali ilikuwa mbaya hadi juzi walipopatanishwa ndiyo wamerudisha ushosti wao,” kilisema chanzo hicho.
WAZEE WAWAPATANISHA
Chanzo chetu kilidadavua kuwa pamoja na Wema kwenda kumwangukia mama’ke, kuna wazee ambao walitinga nyumbani kwa Wema, Kijitonyama ‘Hollywood’, Dar waliotoka upande wa mzazi huyo ambao walikwenda kumsihi afanye hivyo.
“Hazikuwa jitihada zake peke yake za kutaka kumaliza tofauti kati yake na mama’ke bali wale wazee takriban wanne walizungumza na Wema na kumwelekeza namna ya kumaliza tofauti zake na mzaa chema huyo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Hao wazee ndiyo waliwakutanisha kwa mama Wema, Sinza-Mori, Dar na kumaliza chokochoko zote na sasa Wema na mama’ke mambo ni ‘mswaano’.
HALI ILIKUWA MBAYA SANA
Chanzo hicho kiliendelea kushusha data kuwa kulikuwa na ulazima wa Wema kutinga kwa mama’ke na kumwangukia kwani suala hilo lilikuwa likimpasua kichwa na kusababisha hali kuwa mbaya kati ya wawili hao kwa sababu hakukuwa hata na salamu.
WEMA ASHINDA KWA MAMA’KE
Baada ya kusikiliza maelezo hayo kutoka kwa chanzo, Julai 23, mwaka huu saa 5 na sekunde 35 asubuhi, Ijumaa lilizungumza na Wema kutaka kujua alikuwa wapi wakati huo ambapo alijibu kuwa anaenda kwa dada yake kumchukua mtoto aliyemtaja kwa jina la Sasha kisha kwenda kushinda naye Sinza-Mori kwa mama yake.
Alipoulizwa kama ni kweli kuna wazee walimfuata na kumpatanisha na mama yake, staa huyo wa muvi ya Super Star itakayoingia sokoni Agosti alikiri kutokea kwa suala hilo.
HUKO NYUMA
Wiki kadhaa zilizopita, Wema na mama yake walitibuana baada ya mzazi huyo kuwatemea mbovu mashosti wa mwigizaji huyo alipokuwa akihojiwa runingani.

chanzo:GPL

Drunkard demands police lift to sobering up cell

Drunkard demands police lift to sobering up cell

 

 Officers in a police vehicle in a central part of Stockholm were on Monday afternoon surprised to see a highly inebriated man jump in the back of the vehicle demanding they take him to a drunk tank.

The man, who clearly had had a few too many, approached the vehicle when it was stopped at traffic lights near Medborgarplatsen square in central Stockholm, got in and demanded to be taken to a holding cell to sleep it off, according to daily Dagens Nyheter (DN).

“The officers were surprised when he sort of fell into the backseat but he just said he wanted to go and sleep it off in a holding cell,” said officer Viktor Adolphson, who tweeted about the incident for the Södermalm police, to the paper.

Officers heeded the unusual request from the man, who was reportedly middle-aged, and drove him straight to the station.

He was brought in and left to sleep it off and after six hours we sent him home,” Adolphson told DN.

According to the police, this was a very unusual occurrence, and one which they found rather funny at that.

“The man was very intoxicated and had obviously realized his situation. It was still a lot better than when they pass out and we are forced to carry them away,“ Adolphson told DN.



(news@thelocal.se)

yaah hii kawaida sweden gari ya polisi inageuka lift na kituo cha polis kinageuka gest na kesho unapelekwa home,fanya hivyo bongo ukiwa bwii simamisha difenda jipakie kisha waambie wakupeleke kituoni ukalale utakiona kilichomnyonyoa kanga manyoya.ila vibaka wanafanya hivyo wakikimbia kipondo

Brand new from SONY MUSIC-SWEDEN

Hej, Hello, Mambo World! Its 27th July 2012. The only RnB king of Scandinavia TROY JAMZ with KASTENHOLT & DEE releasing brand new hit single with SONY MUSIC. The song go by the name of ''I'M IN LOVE'' is DOPE . Dont dare to miss, buy on iTune and listen on Spotify. Listen the preview of the song here: http://www.youtube.com/watch?v=vlx9Cnt3TT0. This new song by Kastenholt & Dee is something you should never dare to miss. 
Troy Jamz is an international RNB artist and music/video producer and song writer. The same guy who did the latest African HIT for an upcoming Tanzanian artists JanB and Obi ''Pretty Girl''. Troy Jamz is CLASSIC and his RnB album will be out soon this year. Listen IM IN LOVE PREVIEW: http://www.youtube.com/watch?v=vlx9Cnt3TT0
Like and Share this link for the support. We always Do good for our people//JanB Multimedia

IDARA YA USALAMA WA TAIFA YAKANUSHA KUMTESA DR ULIMBOKA STEVEN



Katika siku za hivi karibuni, kumejitokeza taarifa zenye tuhuma kadhaa dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa. Taarifa hizo zimekuwa zikitolewa kwenye vyombo vya habari zikiihusisha Idara hii na matukio ambayo yanaidhalilisha na kuzua maswali mengi kwa wananchi. 

Kati ya tuhuma hizo ni tukio la kutekwa kwa Dr. STEPHEN ULIMBOKA, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari na madai ya kufanywa kwa mipango ya kuwadhuru baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Upinzani. Gazeti moja la kila wiki limekuwa likurudia tuhuma hizo mara kwa mara kwa madai kwamba ni
habari za uchunguzi na kuihusisha Idara.

Idara inataka kuwahakikishia wananchi kwamba taarifa hizo ni za UZUSHI NA UONGO ambazo zina nia ya kuharibu jina na sifa ya Idara. Taarifa hizo zimekuwa zikiunganishaunganisha vipande vya taarifa mbalimbali
ili kukidhi malengo yaliyokusudiwa na wanaolitumiagazeti hilo. Idara haikuhusika wala haihusiki na matukio yoyote yaliyotajwa katika tuhuma hizo. Hivyo tunawaomba wananchi wazipuuze taarifa hizo.

Matukio yaliyotajwa katika tuhuma hizo yanachunguzwa na Jeshi la Polisi ambacho ndicho Chombo Chenye Dhamana, na kwa Maslahi ya Taifa si vizuri kuachia upotoshaji huo uendelee.

Aidha, tunapenda kuwahakikishia Watanzania kuwa uzushi na tuhuma zinazotolewa dhidi ya Idara hazitatuvunja moyo bali zitatuunganisha na hivyo kutuimarisha katika azma yetu ya kuhakikisha nchi yetu
inaendelea kubaki salama kwa kushirikiana na wanachi na Vyombo vingine
vya Ulinzi na Usalama.

Imetolewa na Idara ya Usalama wa Taifa,
Makao Makuu,
DAR ES SALAAM
26 Julai, 2012.

Thursday 26 July 2012

CHAMELEON AANDAMANA HADI UBALOZI WA TANZANIA UGANDA KUMTUHUMU ERICK SHIGONGO KWA KUMNYANGANYA PASPORT YAKE ALIPOKUA ZIARANI TZ

 

DEMONSTRATION AGAINST ERIC SHIGONGO OF   GLOBAL PUBLISHERS TANZANIA

                     Shigongo mwenyewe anayetuhumiwa kunyanganya pasport ya  dr Chameleon
"shigongo rudisha pasiport yangu"

 hapa jamaa akimwambia"e bana tartibu basi watu watasikia"

 haya ngoja niandae kabisa na sehemu ya kulala maana leo tunakesha hapa
Hapa akiwaimbia wafuasi wake,inasemekana hili biti liko njiani na linamuhusu huyu huyu mbabe wetu bongo
 na usalama walimsindikiza


 kumekucha tena shughuli ikaendelea mpaka kieleweke
 mkuu wa polisi nae akatoa baraka zote
 hapa akiongea na waandishi

 hapa dr Chameleon kashachoka kaamua akapumzike lakini swala lishafika mahala pake

NA HUU NI UJUMBE WAKE FACEBOOK

I AM AT THE TANZANIAN HIGH COMMISSION IN DEMOSTRATION FOR THE CONFISCATION OF MY PASSPORT BY A TANZANIAN ILLEGALY ERIC SHIGONGO I NEED MY FREEDOM TO TRAVEL AS A UGANDAN!

I NEED MY PASSPORT BACK ASAP!


FOR GOD AND MY COUNTRY UGANDA.
I AM VERY DISAPPOINTED!

I WAS HIRED BY GLOBAL PUBLISHERS A TANZANIAN COMPANY, TO PERFORM AT THE NATIONAL STADIUM ON THE 7th July 2012.


I PERFORMED AS THE CONTRACT AGREED! ON SUNDAY 8th ONE ERIC SHIGONGO THE CEO GLOBAL PUBLISHERS CONFISCATED MY PASSPORT ALLEGING MY MANAGER HAD SWINDLED HIS 3500$, WHICH IN REAL SENSE WAS SWINDLED BY A KAMPALA CONMAN CALLED GEORGE.


I WAS ASSISTED BY THE UG
...ANDAN EMBASSY IN DAR EL SALAAM, WHO GAVE ME A TEMPORARY DOCUMENT TO RETURN ME HOME.
ON RETURN TO UGANDA I HUNTED FOR THE CONMAN, ARRESTED HIM AND HANDED HIM OVER TO POLICE, WHO FREED HIM ON CONDITIONS I DON'T KNOW!

I EXPLAINED TO THE TANZANIAN AMBASSADOR AT THE TANZANIAN HIGH COMMISSION IN UGANDA FOR ASSISTANCE BUT SEEMS IN VAIN.

I HAVE UPCOMING PERFORMANCES IN

SOUTH AFRICA, ENGLAND,BELGIUM, NORWAY,SWEDEN, CANADA ETC!

SO IS ERIC SHIGONGO ABOVE THE LAW TO KEEP MY PASSPORT ILLEGALY?

AM I LIABLE TO HIS NEGLEGANCE THAT HE TRUSTED A CONMAN?

IS IT FAIR THAT AN UNAUTHORIZED TANZANIAN CITZEN CAN KEEP MY PASSPORT FOR OVER A MONTH?

I NEED ADVICE

hii kasheshe ilitokea siku chache hapo nyuma na ni baada ya chameleon kumaliza kutumbuiza uwanja wa taifa na kutaka kuondoka ndipo shigongo na genge lake wakamwambia hakuna kuondoka mpaka afanye tamasha jingine,Chameleon alipotoa nje kwani haikuwa kwenye mkataba na licha ya hivyo ni kwamba alikua anatakiwa pia akatumbuize south africa kwenye tamasha la MTN.
 hivyo isingewezekana hata kama angeongezwa hela,
inasemekana ndipo Shigongo na genge lake kibabe alimnyanganya pass yake asiondoke kwa madai kwamba alimlipa dola 3500 kwa ajili ya kutumbuiza huko.
inasemekana Chameleon akaongea na wakubwa kwao huko Uganda na ikatolewa order toka kwa mzee Kaguta mwenyewe kwamba aruhusiwe kuondoka haraka sana.ndio kuondoka kama diplomat ila pasi hakurudishiwa,
kwa hiyo ndo ameamua kulizimua tena.

HABARI ZAIDI BOFYA CHINI

DEMONSTRATION AGAINST ERIC SHIGONGO OF GLOBAL PUBLISHERS TANZANIA



MREMBO WA LEO!



                                 anaitwa Nancy Danny
ametokea kiafrika zaidi usisahau pia kumtembelea katika           libeneke lake bofya Africa for Life

FRi 27th Siku ya peke Ali Choki & Extra Bongo(wazee wa kizigo) Live Band direkt from Tanzania & Dj Rich Bongo Flavor


FRi 27th Siku ya peke
Ali Choki & Extra Bongo(wazee wa kizigo)
Live Band direkt from Tanzania & Dj Rich Bongo Flavor in Stockholm Västbarga Allé.Vrätenvägen 21 Buss 165
More info 0737787846 or 0762333917
Entrée 100Kr in Adv 
@the door 150 Kr

EEH!


mi mgeni mahali hapa

RAIS JK ATUA NA KUZINDUA UWANJA MPYA WA SONGWE



Picha mbalimbali zikimuonyesha raisi Jakaya Mrisho Kikwete alipotua katika kiwanja cha ndege cha songwe mjini mbeya mara baada ya kukamilika kwa kiwanja hicho kwenye eneo la kurukia na kutua ndege,Raisi ahimiza kukamilishwa kwa jengo la abiria ambalo liko kwenye hatua za mwisho ili kurahisisha utumiaji wa kiwanja hicho.

Waasi wa M23 washambuliwa zaidi Goma



Helikopta za majeshi ya Umoja wa Mataifa yameshambulia maeneo ya waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Ripoti zinasema kuwa mapigano makali yanaendelea kilomita 50, kaskazini mwa moji wa Goma.
Watu wanaotoroka makaazi hao wamewaambia BBC kuwa wanajeshi wa serikali wamekuwa wakitoroka vita.
Vita hivi vya sasa vilianza tangu mwezi wa April ambapo Umoja wa Mataifa nad Congo zikilaumu Rwanda kuwa kusaidia waasi.
Hata hivyo Rwanda imekanusha madai hayo.
Kufuatia mapigano hayo watu zaidi ya 200,000 wametoroka makaazi yao .
Wiki iliyopita waasi wa vuguvugu la M23, ambao Umoja wa mataifa unasema wanafadhiliwa na Rwanda, walitisha kuuteka mjini wa Goma, ambao ni kituo muhimu cha jeshi la kitaifa.
Kwa wakati huu mapigano bado yanaendelea umbali wa kilomita hamsini kaskazini mwa Goma katika eneo la Rutshuru.
Mwandishi wa BBC katika eneo hilo anasema raia wengi wamehama makwao na kukimbilia mjini Goma na kutafuta afueni katika kambi za Umoja wa mataifa katika eneo hilo.

BBCSWAHILI

JACK PATRICK ADAIWA KUMTOSA MUMEWE

Na Waandishi Wetu
Mwanamitindo Jacqueline Patrick ambaye pia ni Miss Ilala no.3, 2005 anadaiwa kumtelekeza mumewe Abdullatif Fundikira aliyepo mahabusu katika Gereza la Segerea, jijini Dar es Salaam kwa madai ya kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya.
Akizungumza na Amani, rafiki wa karibu na mwanamitindo huyo alisema kuwa wenzake wanamshangaa Jack kwa kitendo cha kumtosa mumewe wakati anafahamu yupo katika matatizo makubwa.
“Kiukweli anachofanya Jack si uungwana kabisa, we fikiria tangu mumewe akamatwe (Mei mwaka huu), hajawahi kwenda mahabusu kumtembelea au hata siku ya mahakamani kuhudhuria kusikiliza kesi yake inavyoendelea, yeye na starehe, starehe na yeye,” alisema shostito huyo akiomba kuhifadhiwa kwa jina lake.
Akiendelea kuzungumza, rafiki huyo alisema kuwa kitu kingine ambacho anaamini kuwa ndoa ya Jack ni ndoano ni kitendo cha kuondoka nyumbani kwake na kutimkia nje ya nchi bila mumewe kuwa na taarifa.
“Yaani huyu mwanamke ni wa ajabu sana, hivi ninavyokwambia yupo nje ya nchi huku mumewe akiwa anateseka mahabusu, mbaya zaidi mume hajui,” alisema.
Baada ya kusikia kauli hiyo, Amani lilianza kumsaka Jack kupitia simu yake ya mkononi ambapo muda wote ilionekana haipo hewani lakini kupitia udodosi wa paparazi wetu, lilimnasa staa huyo juu kwa juu kupitia mtandao wa What’s Up ambapo mahojiano yalikuwa hivi:
Shakoor: Jack ningependa kufahamu upo wapi kwa sasa maana nakutafuta kwenye simu yako ya mkononi sikupati?
Jack: Shida yako nini? Sihitaji stori wala promo ya aina yoyote kutoka kwenu.
Shakoor: Mbona umefika mbali? Hata ninachotaka kukwambia hujakisikia unaanza kuwa mkali.
Jack: Hapa hatuchezi drama hicho ndicho ninachoongea, nipo bize na mambo yangu, naomba niache.
Hata hivyo, Jumatatu iliyopita, paparazi wetu mmoja alifunga safari hadi nyumbani kwa nyota huyo, Mbezi, Dar es Salaam ambapo watu waliokutwa ndani walisema Jack amesafiri kwenda ughaibuni bila kutaja jina la nchi aliyoenda.
Mtu wa karibu na Jack alipopatikana na kuulizwa alipo mwanandoa huyo, aliweka wazi kuwa yupo nchini Finland lakini hakusema amefuata nini huko.
“Mimi ninavyojua Jack yuko Finland, sasa lini atarudi au amefuata nini huko, sijui,” alisema.

Wednesday 25 July 2012

SHEREHE ZA MASHUJAA ZAFANA DAR

Maofisa mbalimbali wa vyombo vya ulinzi na usalama wakimsuburi Rais Kikwete nje ya geti la kuingilia ili kuagana naye.
Gari la Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt, Shein ‘hayupo pichani’ likiwa tayari kumchukua kiongozi huyo baada ya sherehe hizo kumalizika.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange  na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema wakiwa  mstari wa mbele kuagana na viongozi mbalimbali waliohudhuiria sherehe hizo.
Rais Mstaafu, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiagana na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya sherehe hizo kumalizika.
Mmoja wa askari wa enzi za kikoloni ambaye hakufahamika jina lake, akihojiwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na umuhimu wa siku ya mashujaa.
Hawa ni wakuu wawili wa vyombo viwili tofauti na muhimu vya ulinzi na usalama JWTZ na POLISI ambao ni Jenerali Mwamunyange na Inspekta Jenerali Said Mwema wakiwa wamesimama kikakamavu uwanjani hapo.
  Hawa ni maofisa wenye vyeo vya meja Jenerali ambao hawakufahamika majina yao, lakini mmoja ni kutoka Division ya vikosi vya anga  na mwingine kutoka Division ya vikosi vya nchi kavu wametambuliwa kutokana na mavazi yao, walinaswa na kamera yetu wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kama mwenyeji wao katika sherehe hizo. 
Askari wa zamani waliopigana vita enzi za ukoloni wakiwa katika picha ya pamoja baada ya sherehe hizo kufikia tamati.
---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za mashujaa zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Mohamed Shein na baadhi ya maofisa kutoka  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Kama ilivyoada, Rais Kikwete alifanya shughuli zote zinazostahili ikiwa ni pamoja kusimika kisu, jembe na ngao kama ishara ya kuwakumbuka mashujaa wetu.
Pia askari wa zamani waolipigana vita kuu ya pili ya dunia ambao wako hai, walihudhuria sherehe hizo.
 
(Picha/Habari na GPL)