Makamu
  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal 
 ametoa mhadhara kuhusu changamoto za kisayansi katika maadhimisho ya  
miaka 50 ya Idara ya Sayansi za Kimataifa kwa kifupi ISP ya Chuo Kikuu  
cha Uppsala kilichopo Uswidi ambapo amefafanua kuwa, mchango wa  
wanasayansi kutoka katika chuo hiki una manufaa makubwa katika kukuza  
teknolojia katika sayansi kwa nchi za Afrika. 
Makamu
  wa Rais ambaye alikuwa mhadhiri wa somo la Fizikia katika Chuo Kikuu  
cha Dar es Salaam kabla ya kuingia katika siasa, amealikwa na  
wanasayansi wa kariba yake katika maadhimisho haya yaliyo na lengo la  
kutanua uwanda wa tafiti katika nchi za Afrika na hasa Tanzania, ambayo 
 kwa sasa imeanzisha chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson  
Mandela kilichopo Arusha.
Katika
  ziara hii ambayo Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Mawasiliano, 
 Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa nchi 
Ofisi  ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Telezya Huvisa, Naibu Waziri 
wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim pamoja
 na  Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela 
Profesa  Burton Mwamilwa. 
Ujumbe
  wa Makamu wa Rais ulifika hapa na kupata nafasi ya kuzungumza na  
Watanzania waliopo Uppsala ambao wengi walitaka kujua kama Tanzania  
imejipanga vema kukabiliana na tatizo la umeme nchini. Makamu wa Rais  
ambaye katika ziara hii amekuwa akikutana na wanasayansi mbalimbali wa  
Sweden na hasa waliobobea katika sekta ya nishati aliwaeleza Watanzania 
 waliokuwa katika mkutano naye kuwa; kama taifa tuna kila sababu ya  
kukubali kuwa tulifanya makosa huko nyuma kwa kutotambua utanuaji wa  
vyanzo vya umeme wa uhakika hali inayotuumiza sasa lakini pia akawaambia
  kuwa serikali imejipanga vema kuhakikisha kuwa tatizo la umeme 
linapata  tiba katika kipindi kifupi na pia kuwa na umeme wa uhakika 
katika miaka  miwili ijayo.
Maeneo
  makubwa ambayo Makamu wa Rais amekuwa akiwasikiliza kwa ukaribu  
wanasayansi wa Uppsala na Sweden ni kuhusu vyanzo mbalimbali vya  
uzalishaji wa umeme vikiwemo vile vya upepo na maji ya bahari huku pia  
ikiwa Tanzania imeshasaini mkataba wa uzalishaji wa umeme wa makaa yam  
awe na kampuni ya kutoka China, mkataba uliosainiwa wiki mbili  
zilizopita katika ya NDC na kampuni ya China ambazo zitashirikiana  
katika miradi mikubwa katika ukanda wa Mtwara.
Eneo
  jingine ambalo Makamu wa Rais amekuja kulihamasisha ni juu ya uhusiano
  wa chuo hiki kikongwe katika uwanja wa Sayansi na namna chuo hiki  
kitakavyozidisha ushirikiano wake katika kusomesha wataalamu wa Tanzania
  katika ngazi za Shahada za Uzamivu na mchango mkubwa ukiwa kukipatia  
uwezo Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo 
 Arusha. 
Katika
  ziara hii ya kitaaluma aliyoalikwa Makamu wa Rais inayochukua siku  
mbili, Makamu wa Rais pia atakutana na Waziri wa Mambo ya Jamii wa  
Uswidi Ulf Kristersson na Waziri wa Mahusiano na Maendeleo Gunilla  
Carlsson. Katika ratiba hiyo pia Makamu wa Rais atatembelea Taasisi ya  
Mazingira ya Uswidi sambamba na kuzungumzia mafanikio ya Kilimo Kwanza  
kwa wadau wa maendeleo wa Uswidi.

No comments:
Post a Comment