Thursday, 17 June 2010

NIGHT&OUTSTOCKHOLM SODRA WITH VUMBI DEKULA BAND

huyo ni mr lavalava jamaa huwa anaondoka ndombolo utafikiri yuko kazini lol
hapa nikiwa na kipa wa kilimanjaro star kablau

hapa nikiwa na mdau alikibwa vidole kama kawa.

NGOMA LUMBESA HADI MAMTONI DUH


teh teh mtaalam gerry nae akionyesha matukio yake jamaa akifurahi aah utafurahi maana ni viroja tuu,lakini poa ndio maana ya burudani.

MAMBO YA KUPAKAZA NA MIPAKAZO MINGI

big mama isabell always lookin fresh mupenzi.
mdogo mdogo na kilaji
ndio maana yake hapo ngoma ilikua ishakolea vizuuuri sana dah raha jipe mwenyewe bana.

MNAWAKUMBUKA HAWA WATAALAM WA MUZIKI?

mtaaluma loketo nae alikua mbaya enzi zake,akiingia na kitana basi na zile style zake anazuga kama anaanguka halafu anatoa kitana anachana nywele si mchezo,mambo ya tulemonde loketo e e loketooo,tulemonde washiwaa e e washiwa ilikuwa raha mpaka kisogoni dah.
yondo sister enzi hizo mbuta mutu mwana mama eeh mamaaanalingakayo mwana mama eeh mama,likitandikwa solo hapo utakimbia,kipindi hiyo nakaa temeke tazara jirani na njaro uswazi kulikua na baa ya tap tap basi ni mbuta mutu mpaka kichwa kinauma.

kanda bongo man,jamaa kwa sasa anajipigia boksi lake manchester UK,magitaa kayatupilia mbali.

Thursday, 10 June 2010

MISS INDIAN OCEAN NI LEO WADAU


yale mashindano ya miss dar indian ocean sasa yamefikia muda wake,kinyanganyiro hicho kitafanyika leo katika ukumbi wa double tree hilton hotel,kiingilio kitakuwa ni tshs 30,000-tu.na mshindi wa kwanza atajipatia tshs 1.2 mil,wa pili tsh 800000 na watatu ataondoka na tshs 500000,haya wadau mambo ya burudani ndio hayo mjumuike.

NEW SONG:MAMA NTILIEEE,UNIJAZIEEE

songi limetulia kinoma daah,ray c naona bado yupoyupo,jamaa wamejitahidi sana at least tumeona kitu tofauti sio kila mbongofleva ni kubana pua tu.