Saturday 26 July 2014

MAMBO YA ALIKIBA NA DIAMOND

Na Sifael Paul

Hatimaye! Kwa mara ya kwanza staa ‘the big name’ wa Bongo Fleva ndani na nje ya Bongo, Ali Saleh Kiba ameibuka na kumlipua hasimu wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, hali inayotafsiriwa kwamba bifu lao sasa limefika pabaya ikidaiwa kwamba wanagombea nyota (ustaa).
Staa ‘the big name’ wa Bongo Fleva ndani na nje ya Bongo, Ali Saleh Kiba.
Kupitia Kipindi cha The Sporah Show, usiku wa Jumanne wiki hii kwenye CloudsTV, Kiba alimchakaza Diamond ambapo alifunguka mengi ikiwemo chanzo cha ugomvi wao.…
Na Sifael Paul
Hatimaye! Kwa mara ya kwanza staa ‘the big name’ wa Bongo Fleva ndani na nje ya Bongo, Ali Saleh Kiba ameibuka na kumlipua hasimu wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, hali inayotafsiriwa kwamba bifu lao sasa limefika pabaya ikidaiwa kwamba wanagombea nyota (ustaa).
Staa ‘the big name’ wa Bongo Fleva ndani na nje ya Bongo, Ali Saleh Kiba.
Kupitia Kipindi cha The Sporah Show, usiku wa Jumanne wiki hii kwenye CloudsTV, Kiba alimchakaza Diamond ambapo alifunguka mengi ikiwemo chanzo cha ugomvi wao.
Kiba alizungumzia sosi iliyotengeneza bifu kati yake na Diamond ambapo aliulizwa kama ana namba ya simu ya msanii huyo ndipo akatiririka:
“Nilikuwa nayo kipindi fulani, nilipohisi amenikosea nikaona sina ulazima wa kuwa nayo.
“Kuna kipindi alinikosea kwa sababu nilisikia amesema kwamba tulirekodi wote ule Wimbo wa Single Boy, jambo ambalo halikuwa kweli. Halafu akasema mimi ndiyo nilimfuta.
Staa wa muziki Bongo Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’,
“Diamond alinikosea kwa sababu kutokana na mimi ndiye nilifanya wimbo wake wa Lala Salama ambao upo kwenye album yake, akanifuta nikahisi amenikosea sana nilichoimba mimi akawa ameimba yeye, alichoniomba nifanye nilifanya kwa mapenzi yote na mimi namsapoti kila msanii wa Tanzania anayefanya vizuri, sikatai anaimba vizuri, sijui ukisema amekopi, mimi sijamaindi wala nini lakini usiseme kwa watu ukadanganya nikaonekana mimi sifai, siko hivyo mimi.
“Watu wengine ambao hawaelewi vizuri wanaweza wakamwamini Diamond, kila mtu ana mapenzi yake labda kuna wengine wanampenda Diamond wengine wanampenda Ali Kiba. Wanaweza wakawa wengine wanampenda Diamond wakaamini mimi nilimfuta kwenye wimbo wangu wa Single Boy lakini mimi wala, shahidi yangu ni produyuza Manecky (AM Records) kwani ndiye alitengeneza ule wimbo.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo Elizabeth Michael 'Lulu'
“Sikuwahi kwenda studio na Diamond, sikuwahi kufikiria kufanya wimbo naye. Ila alinipigia simu baada ya ule wimbo wa Single Boy kuvuja. Akaomba afanye na mimi, akanipa hadi idea (wazo) ya video, nikamwambia nimeshafanya na Jaydee (Judith Wambura).
Nikamwambia itapendeza zaidi tukifanya wimbo mwingine kwa sababu hii tukifanya mimi na wewe haita-make sense (haitaeleweka), inapendeza ikiwa single boy na single girl, hicho ndicho kitu nilimjibu.
“Baada ya kama wiki moja nikasikia kwenye mablog, nikapigiwa simu kwamba mimi nimemfuta Diamond kwenye ule wimbo wakati yeye ndiye aliyenifuta katika wimbo wake, shahidi prodyuza wangu KGT.
“Kutoka hapo nikaona hakuna tatizo lakini kwa kujua yeye alinifuta katika wimbo wake. Mimi siyo shabiki wa Diamond ni shabiki wa muziki mzuri. “Kuna watu wanasema kachukua kiti changu? Labda kama ni kiti ambacho nilikuwa nimekaa kina vumbi na ninachotakiwa ni kukipangusa tu na kukaa tena, labda yeye yuko siti nyingine ila ya nyuma.
“Niliambiwa alisema vitu vingi, mara nilikopa fedha benki ili nimalizie nyumba na mambo kama hayo so siwezi kufanya naye kazi.” Baada ya Kiba kumchakaza, kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond naye alijibu mapigo bila kutaja jina la Kiba ambapo aliandika: “Tatizo lako wewe unawaza kushindana na mimi ili nishuke…Wakati mwenzako nawaza kushindana na watu wa mataifa mengine ili nilete sifa na heshima nchini kwetu.”

Hata hivyo, baada ya hayo yote kuliibuka madai kwamba mbali na ishu za muziki, mastaa wa kike wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema Isaac Sepetu wanahusishwa kwenye gogoro hilo kisa wivu wa kimapenzi hivyo ishu hiyo bado ni mbichi. Tusubiri mwisho WAKE!

GPL

Tuesday 22 July 2014

Shehena ya viungo vya binadamu yakamatwa Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam


Itv

Shehena ya viungo vya binadamu yakamatwa Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Shehena yenye viungo vya binadamu vikiwa vimekaushwa na kuwekwa kwenye mifuko ya plastiki zaidi ya 85,imekutwa imetupwa katika dampo lisilo rasmi la Bunju "A" bonde la mto mpiji, mpakani mwa jiji la Dar–es–salaam na Bagamoyo mkoani Pwani,hali iliyozua taharuki,simanzi na mshangao kwa wakazi wa eneo hilo la Bunju.
ITV ilifika katika eneo hilo maarufu kama bonde la mto mpiji na kukumbana na umati wa watu wakienda kushuhudia tukio hilo ambalo wananchi hao walikuwa wakishangaa kutokea katika eneo lao,huku jeshi la polisi kituo cha polisi bunju na wale wa wazo hill,wakijaribu kuzuia umati wa watu wasisogelee katika eneo la tukio.
 
Nao mashuuda wa tukio hilo Bwana Ruta na Bwana Huseni wamesema kuwa mama mmoja aliyekuwa akiponda kokoto katika eneo hilo ambalo si halali kwa shuhguli za machimbo na dampo, aliona gari likija na kumwaga mifuko hiyo,ambapo mara baada ya kuondoka wamwagaji hao alikwenda kutafuta chohote kitu na ndipo alipokumbana na kadhia hiyo na kukimbia na kuomba msaada.
 
katika kituo kidogo cha polisi Bunju, jeshi la polisi chini ya kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni kamishan msaidizi wa polisi Camilius Wambura.walilazimika kuongeza ulinzi ili kudhibiti wananchi hasa bodaboda waliokuwa wamefurika katika kituo hicho ili kujua hatma ya tukio hili mara baada ya kuwepo kwa tetesi za gari dogo maarufu kama kiyoliyoli kufikishwa kituoni hapo huku ndani ya gari hilo likitoa majimaji yaliyoashiria uwepo wa mizigo waliyotilia shaka.
 
Katika eneo la tukio wananchi wakishirikiana na askari wa jeshi la polisi walivalia kiraia, walichukua shehena hiyo na kwenda kuiihifadhi sehemu salama, ambapo licha ya zoezi hilo kufanyika karahisi kwa kuvalia gloves bila ya maski za puani, huku baabdhi ya wadadisi wa mambo wakisema huwenda zoezi hilo likawa na madhara kwa wahusika kwani viungo hivyo havikujulikana mara moja vilikaushwa kwa dawa gani.
 
kamandaa wa polisi mkoa wa kipolisi kinondoni Acp Camilius Wambura amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa bado jeshi linaendelea na upelelezi ili kujua hiyo mifuko zaidi ya 85 yenye viungo vya binadamu vikiwa vimekaushwa kwa ustadi vimetoka wapi na pindi uchunguzi utakapo kamilika watatoa majibu.

Monday 14 July 2014

Dekula Band "Ngoma Ya Kilo" Place: Live "Little Nairobi"18-19/07/2014



"Wezee Wapewe" presents;
Soukous Explosion!
Dekula Band "Ngoma Ya Kilo"
Place: Lilla Wien "Little Nairobi"
Date: 18-19/07/2014
Time: 21.00-01.00
Addr: Swedenborgsg. 20
Pendel: Södra station
New CD Shujaa Mamadou Ndala
But it from itunes, amazon, qabuz

Friday 4 July 2014

Mbasha amshitaki Gwajima

stori: Waandishi Wetu
Mambo juu ya mambo! mvumo mkali wenye kuogofya unaendelea kutamalaki katika ndoa ya wanamuziki zao la upako wa Injili Bongo, Emmanuel na Flora Mbasha, safari hii ‘topiki’ siyo zile tuhuma za ubakaji zilizopo mahakamani.
Wanamuziki zao la upako wa Injili Bongo, Emmanuel na Flora Mbasha,

Mbeba ‘niuzi’ wa awamu hii ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, baada ya Mbasha kuona isiwe tabu, hivyo kuamua kupambana na mtumishi huyo wa Mungu kwa njia ya kiroho zaidi. 
Mbasha baada ya kulieleza gazeti mama la hili, Uwazi lililoandika habari yenye kichwa “Mbasha: Gwajima Niachie Mke Wangu”, akiidadavua dhana yake kwamba hapendi ufadhili wa Gwajima kwa mkewe, yaani Flora sasa ameamua kwenda mbele zaidi.
Habari zinadai kuwa, mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Mkoa wa Dar es Salaam, Bruno Mwakibolwa ambalo Gwajima ni memba hai, ameshapokea mashitaka kuhusu mchungaji huyo kuhusika kuitikisa ndoa ya waimbaji hao wa Neno la Mungu na mlalamikaji ni Mbasha mwenyewe.
Wikiendi iliyopita, Mbasha aliketi na kiongozi huyo na kushusha tuhuma zake dhidi ya Gwajima kama zilivyothibitishwa na mlalamikaji mwenyewe, nazo ni hizi zifuatazo;
MOSI; Gwajima ni kiongozi wa kiimani wa Mbasha na Flora lakini tangu matatizo ya ndoa yao yalipojitokeza, mchunga kondoo huyo wa Bwana hajawahi kufanya lolote kunusuru muunganiko huo uliohalalishwa kwa jina la aliye juu.
Emmanuel Mbasha
PILI; Gwajima anajua kila kitu kuhusu mgogoro wa Mbasha na mkewe lakini kipindi chote cha matatizo, Kanisa la Ufufuo na Uzima limekuwa mfadhili wa Flora kwa sehemu kubwa. Hapa anauliza, huu ufadhili una kipi nyuma yake?
TATU; Gwajima anatambua kuwa Flora ni mke wa mtu, mwenye mali ameshaomba aachiwe mwandani wake bila mafanikio. King’ang’anizi kina msukumo upi?
NNE; Gwajima amekuwa akimuumiza Mbasha kihisia, kiakili na kiroho kwa sababu yeye anagombana na mkewe lakini mchungaji huyo bila kufikiria maumivu aliyonayo, humwita Flora madhabahuni katika ibada na kumpa nafasi ya kuimba.
TANO; Flora anaishi hotelini na yeye mwenyewe alishakiri kuwa fedha za kulipia hoteli alizipata kutokana na michango ya waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima. Hapa Mbasha analalamika, inakuwaje kanisa limfadhili mke wa mtu kuishi hotelini ikiwa mumewe hajui?
SITA; Katika hoja zote hizo, Mbasha amelieleza Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste kuwa hana imani na Gwajima kwa vile kama ni busara baada ya kuona ndoa hiyo imetikisika yeye (Gwajima) angekaa pembeni kwa namna yoyote ile, hivyo Mbasha akaiomba menejimenti ya baraza hilo kumpa adhabu kali mwenzao.
Mbasha alipozungumza na Amani, Jumanne iliyopita, alisema baraza hilo liliahidi kushughulikia shauri lake na uamuzi utachukuliwa baada ya kumwita Gwajima na kumsikiliza kwa upande wake.
WENYE KWENU KWAHERI!
Kesi ya Mbasha kudaiwa kumbaka shemeji yake ilipoanza, mume huyo wa Flora alikimbilia mafichoni, kwa hiyo swali kwamba anaabudu kwenye kanisa gani halikuwa na mashiko kwa sababu mhusika mwenyewe hakuwa akionekana.
Baada ya Mbasha kujitokeza na kufikishwa mahakamani, kupelekwa mahabusu kwenye Gereza la Keko kabla ya kuachiwa kwa dhamana, ndipo swali kuwa anaabudu kanisa gani lilipoanza kutokana na ukweli kuwa yupo uraiani kwa ‘bondi’.
Swali hilo lilitokana na hoja kwamba kabla ya mgogoro na mkewe walikuwa wakisali kwenye Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Gwajima ambaye alishamtuhumu kumfadhili Flora na akamtaka amwachie ‘waubani’ wake huyo ili maisha yaendelee.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima,

Jawabu la swali hilo, lilijibiwa Jumapili iliyopita baada ya Mbasha kutinga Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), maarufu kama Mito ya Baraka, linaloongozwa na Mchungaji Bruno Mwakibolwa, na kukamilisha haja zake za kuabudu pale.
Mbasha alipozungumza na Amani kuhusu kusali kwa Mchungaji Mwakibolwa badala ya kwa Gwajima, alijibu: “Nimehama Kanisa la Ufufuo na Uzima, sisali tena kule. Kuanzia sasa shughuli zangu za kuabudu nitazifanyia Mito ya Baraka kwa Mchungaji Mwakibolwa.
“Siwezi kwenda kwa Gwajima kwa sababu simuelewi na ndiyo maana nimeamua kumshtaki kwa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste. Roho yangu ya kuabudu isingekuwa timilifu, ingejaa mashaka kwenda sehemu ambayo imenijeruhi na nisiyoiamini.
“Kwa kifupi si kwamba nimeanza kuabudu Mito ya Baraka hili ndilo kanisa letu tangu zamani, mimi na mke wangu. Tulihamia Kanisa la Ufufuo na Uzima baada ya Gwajima kutushawishi, kwa hiyo nimerejea kundini.
MCHUNGAJI MWAKIBOLWA
Juzi, Amani lilimsaka Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Mkoa wa Dar es Salaam, Mchungaji Mwakibolwa lakini simu yake ilipokelewa na kusikika sauti za watu wakiwa kwenye maombi kama si ibada.
GWAJIMA
Baada ya hapo, Amani lilimsaka Mchungaji Gwajima kwa njia ya simu yake ya mkononi lakini yeye hakupokea hata pale alipopigiwa kwa kurudiarudia.
KESI YA MBASHA
Kesi ya Mbasha kudaiwa kubaka itatajwa tena Julai 17, mwaka huu kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam.
VIPI KUHUSU KUPATANA?
Wiki iliyopita katika Gazeti la Risasi Jumamosi kuliandikwa habari yenye kichwa; MBASHA, FLORA WAPATANA. Katika habari hiyo ilidaiwa wawili hao walipatana lakini walibakiza kikao kimoja cha kumalizia taratibu zote.
Habari zinasema, taratibu hizo zinandelea licha ya Mbasha kumshitaki Gwajima kwenye Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Mkoa wa Dar es Salaam.    

Video-Racist Australian woman caught on Camera abusing Asian


Mwanamke mbaguzi achunguzwa Australia

australia
Bbcswahili
Polisi nchini Australia wanamchunguza mwanamke anayedaiwa kuwatusi abiria wenzake matusi ya kibaguzi mjini Sydney.
Aliwatukana akitumia ishara za kibaguzi, akiwakemea kuhusu lafudhi zao na kumtaja mwanamke mmoja kuwa 'Gook'
Mmoja wa abiria waliokuwa kwenye treni hiyo alimnasa mwanamke huyo akitoa matusi hayo kwa kutumia simu yake kisha kuiweka kanda hiyo kwenye mtandao wa Youtube.
Kanda hiyo ya dakika tatu na nusu, imejaa matusi ya kibaguzi tu.
Iliwekwa kwenye mtandao wa Youtube, Jumatano, na mmoja wa abiria waliokuwemo ndani ya treni hiyo.
Kanda hiyo inaanza kwa mwanamke huyo kueleza hasira yake kwa watoto ambao walikataa kumsimamia ili aweze kuketi.
Kisha akaanza kumtukana mwanamke aliyemuita mtu wa Asia' pamoja na mwanamume aliyedhani alikuwa mpenzi wa mwanamke huyo.
Mwangalieni huyu 'bogan' hapa,'' anasema mwanamke huyo, akitumia lugha ya mtaa ya Australia ambayo ni sawa na kusema 'takataka'. Unaweza kupata tu 'gook', huna uwezo wa kupata msichana wa kaiwada? alimuuliza mwanamume aliyekuwa ameketi na mwanamke huyo. Nina kuhurumia sana wewe 'gook' . Neno Gook hutumika kumkejeli mtu na lilitumika wakai wa vita vya Vietman.
Kanda hiyo imetazamwa zaidi ya mara 150,000 kwenye Youtube pamoja na mjadala kwenye Twitter na Facebook kuhusu ubaguzi wa rangi.
Chini ya sheria za Australia kuhusu ubaguzi, ni kinyume na sheria kumuudhi mtu , kumtukana, kumadhalilisha na hata kumtisha kwa sababu ya rangi yake au kabila lake.
Lakini serikali kwa sasa inajadili ikiwa itafutulia mbali kipengee hicho .Mpago huo ni tatanishi, na baadhi wamezungumzia sheria hiyo katika mjadala.
Baadhi ya watu wamemtetea mwanamke huyo wakisema kuwa wahamiaji wamejaa Australia na wanjidai sana utadhani huko ndio kwao.
Lakini wananchi wengi wa Australia waliomba msamahakwa niaba ya mwanamke huyo.
''Mwanamke huyo hawakilishi maoni ya watu wa Australia, pole kwa walioudhika sana na ni aibu sana kwetu,'' walisema watu wengi nchini humo.

Mwanamke huyo anajulikana kama Sue Wilkins, mwenye umri wa miaka 55 na inaarifiwa aliomba msahama kwa matamshi yake na kusema kuwa alikosa sana.