Friday 29 January 2010

VIDEO>BEN AELEZA ALICHOKIONA USIKU WA MAUAJI YA SWETU


inatia uchungu sana lakini sielewielewi hawa jamaa kwanini walikuwa busy sana kumshughulikia marehemu,kama ben anavyosema kwamba walimtrick kama wanaenda o,bay kisha wakapotelea mitaani kwenda kuendeleza umafia wa kumfanyizia jamaa basi lazima kuna kitu kimejificha hapo si bure.

Thursday 28 January 2010

TANZANIA FULL MENU


kwa recipe ifuate http://alhidaaya.com

AOKOLEWA BAADA YA SIKU 15 KWENYE KIFUSI


you lucky girl,iliyobaki sasa we ni mipakazo tu,mungu kashakupa go ahead.

WALIOPORA UHAI WA SWETU HAWA HAPA MAHAKAMANI


ningeshukuru sana kama nawao wangenyongelewa mbali basi angalau tupunguzehasira,lakini kwa bongo mmh,usije shangaa ikaundwa tume kufanya uchunguzi,miaka miwili badae ukaambiwa waliuwa bila kukusudia,halafu wakahukumiwa mwaka mmoja,then baada ya miezi mitatu wakachiwa kwa msamaha wa rahisi,bongo sheria kizungumkuti tu

Wednesday 27 January 2010

R.I.P SWETU FUNDIKIRA




WA KARIBU KAULIWA KINYAMA PASI KUWA NA SABABU YOYOTE YA MAANA,NASHINDWA KUELEWA NINAPOSIKIA HAWA WAJESHI WAMEMTOA ROHO RAFIKI ETI KISA KAKWARUZA GARI LAO,HIVI INAINGIA AKILINI KWELI?BONGO
INATIA UCHUNGU SANA NA KUHUZUNISHA PALE UNAPOSIKIA RAFIKI NA MTU WAKOKUPIGANA PASI MBONA KAWAIDA TU MNAELEWANA MNAMALIZANA HAPOHAPO SASA NININI HIKI?UTAMUUAJE MWENZIO ETI KWAAJILI YA KUCHUNA GARI YAKO?IMENIUMA SANA KWAKWELI,KWA UPANDE MWINGINE NINGEWEZA HATA KUELEWA KAMA MAREHEMU SWETU ANA HISTORIA YA UGOMVI AU DHARAU,JAMAA ALIKUWA MTU POA SANA MTARATIBU NA SIKU ZOTE AKISISITIZA USTAARABU,HATA SIWEZI KUAMINI UKINIAMBIA ALIWAJIBU VIBAYA AU KUWATUKANA,NO NAKATAA KWANI MIAKA KUMI NA KITU NILIYOMJUA SIKUWAHI KUONA HATA AKIMDHARAU MTU ACHILIA MBALI KUTUKANA,KWELI BONGO MAISHA YAKO REHANI HAKYANANI,HAYA YAKUTOKEA YAMETOKEA TUNAMUOMBEA MAREHEMU APUMZISHWE KWA AMANI NA MUNGU ABARIKI NDUGU NA FAMILIA YA MAREHEMU,AMINA
N:B,USHAURI SERIKALI IWAJENGEE WANAJESHI BARABARA ZAO BWANA MAANA SASA VIFO VITAONGEZEKA NA VILEVILE KILA MJESHI ANAPOKUA BARABARANI NA GARI YAKE AWEKE ALAMA ILI WATU WAWE WAANGALIFU WAKAE MBALI WASIJE KUTOLEWA UHAI WAKIIGONGA AU KUIPIGA PASI GARI YAKE.

Monday 25 January 2010

Nine bodies found from Ethiopian Airlines crash

Beirut, Lebanon (CNN) -- Rescue crews searched feverishly in poor weather conditions Monday for passengers from an Ethiopian Airlines flight that crashed into the Mediterranean Sea minutes after takeoff with 90 people aboard. By Monday morning, crews had found nine bodies, but no survivors, off the Lebanese coast where the Boeing aircraft had gone down, the Lebanese government said. Prime Minister Saad Hariri announced a day of mourning for the victims of the crash, ordering all government departments to close, the national news agency reported. He praised security forces and the Red Cross for their efforts in the aftermath of the accident. Ethiopian Airlines Flight 409 left Rafik Hariri International Airport in Beirut about 2:30 a.m. and was headed to the Ethiopian capital, Addis Ababa. It disappeared from radar a few minutes after takeoff, said Ghazi El Aridi, Lebanon's minister of public works and transportation. Authorities did not immediately know the cause of the crash. "We don't believe that there is any indication for sabotage or foul play," Lebanese President Michel Sulayman said. habari hizi za kusikitisha zimefika asubuhi hii,mungu awabariki marehemu ambao mpaka sasa ni kumi na nane(18)

Friday 22 January 2010

FALLY IPUPA ZENITH JAN 2, 2010


kama nilivyoahidi show hiyo hapo ni moto mkali vibaya jamaa wanapiga uno kama wamepagawa show imetulia na nyimbo zina mpangilio,sijaona kung fu style wala sarakasi humu ni show la kufa mtu wadau pateni utamu.

Thursday 21 January 2010

HARUNA MOSHI*BOBAN*ATUA SWEDEN



Tanzanians Haruna "Boban" Moshi has visa red tape behind. Yesterday he was back on Strömvallen and after training, he could say:
- I am very happy to be here.

karibu sana mkuu tuliendeleze libeneke mikasani,najua tutakutana tu mitaani hapahapa,kama kina credo,machupa,shekhan,kaniki tuko pamoja.

Don't be fooled by Mtagwa's record!


Don't be fooled by Mtagwa's record"Rogers Mtagwa doesn’t have the backing of a high-profile promoter or an influential manager. Nor does he have a television network clearing dates to broadcast his fights. He doesn’t have his own publicist. He’s rarely, if ever, called out by anyone.
He operates far from the spotlight that shines so brightly on guys like Floyd Mayweather Jr., Manny Pacquiao and Shane Mosley. He speaks next to no English and can’t plead his own case, like a Mayweather does so effectively. He struggles to get by on his boxing income, so much so that he still goes to work as a roofer, weather-permitting, in his adopted hometown of Philadelphia.

Yet, know this: Miss a Mtagwa fight at your own peril.
For all the things he’s not, for all the things he doesn’t have, he does have this: A fighting spirit unsurpassed in professional boxing."

ingawa hana record nzuri lakini naona jamaa anakubalika maana jamaa anaitwa(MOYO WA SIMBA) si mchezo,na kinachofanya wamkubali ni uwezo wake wa kuvumilia na kupigana raundi zote bila kukata tamaa na ndiyo inavyotakiwa,endelea na moyo huo MTAGWA iko siku nawewe utaweka historia ya TANZANIA juu.

Wednesday 20 January 2010

RAIN BOW AU UPINDE WA MVUA


zamani tulisimuliwa hadithi nyingi sana juu ya hii kitu,lakini sijui kama ni kweli ingawa mnimi nnachoona na kufurahia hapo ni huo uzuri wa picha uliotukuka

source:mjengwa.blogspot.com

POLISI NA RUSHWA TANZANIA


waziri wa mambo ya ndani lawrence masha na mkuu wa polisi said mwema mmeliona hili?

Tuesday 19 January 2010

Friday 15 January 2010

MAPISHI YA PWANI:BIRIYANI YA NYAMA.




VIPIMO VYA NYAMA



Nyama 2 Ratili (LB)

Chumvi kiasi

Mafuta 1 Kikombe

Samli ½ Kikombe

Kitungu (Kata virefu virefu) 3 Vikubwa

Nyanya (kata vipande) 2

Nyanya kopo 1 Kijiko cha chakula

Thomu 1 Kijiko cha chakula

Tangawazi 1 Kijiko cha chakula

Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai

Pilipili ya unga nyekundu ½ Kijiko cha chai

Kotmiri iliyokatwa 2 Vijiko vya chakula

Viazi 6

Gram masala 1 Kijiko cha chai

Mtindi ¼ Kikombe cha chai



NAMNA YA KUTAYARISHA KUPIKA

1. Kwenya karai au (sufuria) mimina mafuta na samli. Yakishapata moto mimina vitunguu vikaange mpaka viwe rangi ya hudhurungi. Vitowe viweke pembeni.

2. Kaanga viazi na viweke pembeni.

3. Chukua sufuria tia nyama, thomu, tangawizi, pilipili, nyanya, nyanya ya kopo, mtindi, na pilipili ya unga. Chemsha mpaka iive.

4. Tia vile vitungu ulioyovikaanga, tia viazi, gram masala, kotmiri na yale mafuta uliokaangia vitunguu kama ¼ kikombe, acha moto mdogo mdogo kama ¼ saa, epua weka pembeni.

VIPIMO VYA WALI

Mchele 5 Magi (Kikombe kikubwa)

Hiliki nzima 4

Mdalasini mzima 1

Zafarani ½ kijiko cha chai

Rangi ya biriani ¼ Kijiko cha chai
Mafuta yaliyokaangiwa vitunguu ½ Kikombe
Chumvi kiasi

Roweka zafarani na rangi kwenye kikombe na ¼ kikombe cha maji. Roweka kabla ya robo saa.


NAMNA YA KUTAYARISHA

1. Osha mchele uroweke kwenye maji muda wa dakika 20.

2. Chemsha maji kwenye sufuria kama magi 10.

3. Tia hiliki na mdalasini.

4. Yakishachemka unatia mchele,chemsha usiive sana, unamwaga maji.

5. Unamimina tena ule mchele ½ yake kwenye sufuria, unatia rangi na zafrani kidogo, halafu unamimina mchele uliyobakia unatia rangi iliyobakia.

6. Mafuta yake unayachemsha mpaka yachemke unamimina juu ya mchele, unarudisha motoni unaweka moto mdogo ukisha kuiva, tayari kupakuliwa.

7. Unapakuwa wali unaweka chini kwenye sahani na juu yake sosi ya nyama.

source:alhidaaya.com

KITCHEN PARTY BONGO MMH!



ndio maana wanaume hatuitajiki kwenda kama mambo yenyewe ndo haya mzuka unaweza ukupande ghafla mwananchi ukamrukia mtu maana mmmh!waende wenyewe sawa tu.

ubunifu:TAXI MJINI MUSOMA


lakini sasa ikipigwa mvua mfululizo si itaoza ama?

Thursday 14 January 2010

TIGER WOOD NA MAKASHESHE YAKE


US automaker General Motors said their agreement with Tiger Woods, seen here in 2009, that allowed the embattled golf star to have use of its cars for free has ended.
ah ndio uanaume ukiamua kuwa chovyachovya inabidi ujiandae na mikasa pindi likisanuka

TETEMEKO LA ARDHI HAITI JAN 13


Turning pickup trucks into ambulances and doors into stretchers, Haitians were frantically struggling to save those injured in this week's earthquake as desperately needed aid from around the world began arriving Thursday.

MAOMBOLEZO YA SIMBA WAVITA STOCKHOLM SWEDEN


kitabu cha maombolezo ya mh RASHID MFAUME KAWAWA kimefunguliwa ubalozini tar 8 jan,hivyo mdau mtanzania uliyeko sweden unaweza kujumuika pia kutia saini pale ubalozini.R.I.P KAWAWA

Friday 8 January 2010

LEO BIRTHDAY YA KANUMBA THE GREATEST


ujumbe wake>
“MWAKA HUU SITOSEMA KITU,NI KAZI TU”
haya mtaalamu wewe wadondoshee mamuvi dabodabo mpaka wakinai nakuaminia.

PAMBANO LA FLOYD MAYWEATHER NA PAQUANO LAAHIRISHWA


pambano hilo la uzito wa welterweight limeahirishwa baada ya floyd kutaka jamaa achukuliwe vipimo vyoote,hadi ngoma kabla hajaingia ulingoni,na jamaa nae akasema ana matatizo ya woga wa kuchomwa sindano hivyo akichukuliwa vipimo ataathirika akiingia ulingoni,pambano ambalo lilikua liwaingizie midola ya kufamtu limefutwa.sasa changamoto kwa mabondia wetu hapo nyumbani sijui itakuwaje hii sheria ikiingia maana juzi nimeona picha tubondia fulani tunapima kwa ajili ya mpambano nikachoka,hata kama wanapigana uzito mdogo afya yao ilikua mgogoro kwakweli,yaani washauriwe wapige msosi na tizi halafu wawe wanacheki afya mara kwa mara vilevile.

Thursday 7 January 2010

OLD IS GOLD WENGE B.C.B.G 4X4 1989


enzi hizo wenge wakitesa na vibao vyao kama djino,dady bitodi,nick d,kipindi hiyo unawakuta manda chante,alain mpela werrason,didier masela,alain makaba,marie paul,na wengine wengi tu wadau mnaweza kumalizia hapo,yaani enzi hizo ilikua balaa style ni bon chik bon gere,moto mkali,hapo JB hakuwepo.

FALLY IPUPA AKIFANYA MAZOEZI KABLA YA KUACHIA SHOW YA KUFAMUTU PARIS


show live yenyewe nzima ntaweka hivi punde,ngoja mwakilishi wangu aliyekuwepo kwenye show anirushie mtaziona hapahapa.tuwe pamoja

RIHANNA NA BOYFRIEND MPYA TENA








Hapo ndo utakoma na mademu,maana wanakomaa nasi kichizi,ukileta kuringa anatambaa sikumbili tatu unamkuta na jamaa mwingine,sasa ndo utajua ujinyonge au uamue uwe mlevi basi yaishe,maana unapomwacha sometime inakua unatingisha kiberiti mwenzio anafanya kweli,halafu jamaa wanaokuwa wamemiliki baada ya hapo wanakuwa wakali kweli wanakaba mpaka golini

MAMBO YA MASEBENE KAMA KAWA TUNAWAKILISHA


hapo mzee kitu kilikuwa kimekubali yaani mserereko mambo ya ngwasuma mshkaji nae ni mzima kweli kwenye maswala hayo na anapiga kiswahili kama mtoto wa uswazi,jamaa mtu wa kujichanganya sana hasa na sisi wamatumbi,BIG UP SANA.

DA!NIMEMISS SANA HAYA MAMBO PALE MANGO GARDEN



hii full menyu maana siku nyingi kweli vitu hivi asilia vinatupita mbali aagh,mchana enzi hizo na washkaji aah mnapiga hiyo kitu na ugali wa kufamtu then baada ya hapo utake nini tena?nyagi au tusker briidi,kingine mnajua wenyewe ni nini baada ya hapo kwa sisi mabachela.

Wednesday 6 January 2010

MITANDAO IMEINGILIWA NA WAPUUZI?

SIKU HIZI MITANDAONI IMEKUA SOO TUPU MAZEE,YAANI HAWA WANAIJERIA WANATUNYANYASA SI MCHEZO MAANA SASA TUNASHINDWA HATA PA KUTOKEA,JAMAA WALIFANIKIWA KUCHOTA PASSWORD YANGU MAHALI,BASI WAKANIFUNGIA MAIL NIKAWA NASHINDWA KULOG IN,SASA KILICHOTOKEA BADO WANAENDELEA KUNIFATILIA KILA MAHALI,BLOG YANGU INGINE IMEBIDI NIFUNGE KWANI SIWEZI KULOG IN MAIL ILE NILIYOFUNGULIA NDIO WANAYO KILA NIKIJARIBU WANANAMBIA MPAKA ADMIN AVERIFY WAKATI ADMIN NI MIMI MWENYEWE,NIKIENDA KULE KWENYE MAIL NYINGINE NILIYOBADILISHA SIONI MAOMBI YA KUVERIFY BLOG MEMBER BALI WANANTUMIA FOMU ZINGINE NIJAZE PASSWORD NA EMAIL HAPO NDO NASHANGAA SASA,LAKINI HAYA MAMBO YA KUTAPELIANA YATAENDA MPAKA LINI SASA???

MAMBO NATURAL*mama yeyoo*MMH

mtoto safi kabisaa toka umasaini,yaani watoto kama hawa wakiingia town sijui inakuwaje maana ni full flavor,yes shes beautifully,so natural au mnasemaje wakubwa

TANZANIA BEAUTY CELEBRITY*AUNT EZEKIEL*



mmoja kati ya wasanii wazuri bongo,sio kuigiza nop,uzuri na mvuto nadhani naeleweka.sijasema kama hajui kuigiza no,sijawahi ona movie zake labda nyinyi wadau mtueleze mnamuonaje ktk kuigiza?maoni buree

ONE OF A DAY IN A PARTY


juu ni mimi na side stockholm सोदर
chini nikiwa na hilaly km kawa mipakazo

mitterand CHAMPAGNE



mmmh one of my favourite song,enjoy
MAESTRO VUMBI KAHANGA+DEKULA BAND
maestro vumbi akilichapa gitaa kama kawaida yake,mzee anakubalika toka enzi za maquees du zaire sasa ukitaka kupata ladha hasa ya muziki wa tanzania usikose kumpitia pale lilla wien stockholm sodra ijumaa na j,mosi.

INTRO (MNAKARIBISHWA)UKUMBINI


karibuni waungwana kwenye kiwanja chetu hiki cha burudani,hapa utapata music,video,picha za matukio ya kila aina hasa michezo,kwa ujumla burudani ya aina yoyote ile,popote pale itawekwa hewani,vilevile mnakaribishwa kutuma maoni,picha za burudani kutoka mahali popote duniani zitawekwa mradi si matusi wala kashfa,picha kutoka kwenye kumbi yoyote ya starehe hasa bongo zinakaribishwa nami ntajitahidi kuwawekea chochote ntachokipata,haya wakubwa tushirikiane kunogesha jukwaa letu hili,ahsanteni