Friday 15 January 2010

MAPISHI YA PWANI:BIRIYANI YA NYAMA.




VIPIMO VYA NYAMA



Nyama 2 Ratili (LB)

Chumvi kiasi

Mafuta 1 Kikombe

Samli ½ Kikombe

Kitungu (Kata virefu virefu) 3 Vikubwa

Nyanya (kata vipande) 2

Nyanya kopo 1 Kijiko cha chakula

Thomu 1 Kijiko cha chakula

Tangawazi 1 Kijiko cha chakula

Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai

Pilipili ya unga nyekundu ½ Kijiko cha chai

Kotmiri iliyokatwa 2 Vijiko vya chakula

Viazi 6

Gram masala 1 Kijiko cha chai

Mtindi ¼ Kikombe cha chai



NAMNA YA KUTAYARISHA KUPIKA

1. Kwenya karai au (sufuria) mimina mafuta na samli. Yakishapata moto mimina vitunguu vikaange mpaka viwe rangi ya hudhurungi. Vitowe viweke pembeni.

2. Kaanga viazi na viweke pembeni.

3. Chukua sufuria tia nyama, thomu, tangawizi, pilipili, nyanya, nyanya ya kopo, mtindi, na pilipili ya unga. Chemsha mpaka iive.

4. Tia vile vitungu ulioyovikaanga, tia viazi, gram masala, kotmiri na yale mafuta uliokaangia vitunguu kama ¼ kikombe, acha moto mdogo mdogo kama ¼ saa, epua weka pembeni.

VIPIMO VYA WALI

Mchele 5 Magi (Kikombe kikubwa)

Hiliki nzima 4

Mdalasini mzima 1

Zafarani ½ kijiko cha chai

Rangi ya biriani ¼ Kijiko cha chai
Mafuta yaliyokaangiwa vitunguu ½ Kikombe
Chumvi kiasi

Roweka zafarani na rangi kwenye kikombe na ¼ kikombe cha maji. Roweka kabla ya robo saa.


NAMNA YA KUTAYARISHA

1. Osha mchele uroweke kwenye maji muda wa dakika 20.

2. Chemsha maji kwenye sufuria kama magi 10.

3. Tia hiliki na mdalasini.

4. Yakishachemka unatia mchele,chemsha usiive sana, unamwaga maji.

5. Unamimina tena ule mchele ½ yake kwenye sufuria, unatia rangi na zafrani kidogo, halafu unamimina mchele uliyobakia unatia rangi iliyobakia.

6. Mafuta yake unayachemsha mpaka yachemke unamimina juu ya mchele, unarudisha motoni unaweka moto mdogo ukisha kuiva, tayari kupakuliwa.

7. Unapakuwa wali unaweka chini kwenye sahani na juu yake sosi ya nyama.

source:alhidaaya.com

No comments:

Post a Comment