Tuesday 22 July 2014

Shehena ya viungo vya binadamu yakamatwa Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam


Itv

Shehena ya viungo vya binadamu yakamatwa Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Shehena yenye viungo vya binadamu vikiwa vimekaushwa na kuwekwa kwenye mifuko ya plastiki zaidi ya 85,imekutwa imetupwa katika dampo lisilo rasmi la Bunju "A" bonde la mto mpiji, mpakani mwa jiji la Dar–es–salaam na Bagamoyo mkoani Pwani,hali iliyozua taharuki,simanzi na mshangao kwa wakazi wa eneo hilo la Bunju.
ITV ilifika katika eneo hilo maarufu kama bonde la mto mpiji na kukumbana na umati wa watu wakienda kushuhudia tukio hilo ambalo wananchi hao walikuwa wakishangaa kutokea katika eneo lao,huku jeshi la polisi kituo cha polisi bunju na wale wa wazo hill,wakijaribu kuzuia umati wa watu wasisogelee katika eneo la tukio.
 
Nao mashuuda wa tukio hilo Bwana Ruta na Bwana Huseni wamesema kuwa mama mmoja aliyekuwa akiponda kokoto katika eneo hilo ambalo si halali kwa shuhguli za machimbo na dampo, aliona gari likija na kumwaga mifuko hiyo,ambapo mara baada ya kuondoka wamwagaji hao alikwenda kutafuta chohote kitu na ndipo alipokumbana na kadhia hiyo na kukimbia na kuomba msaada.
 
katika kituo kidogo cha polisi Bunju, jeshi la polisi chini ya kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni kamishan msaidizi wa polisi Camilius Wambura.walilazimika kuongeza ulinzi ili kudhibiti wananchi hasa bodaboda waliokuwa wamefurika katika kituo hicho ili kujua hatma ya tukio hili mara baada ya kuwepo kwa tetesi za gari dogo maarufu kama kiyoliyoli kufikishwa kituoni hapo huku ndani ya gari hilo likitoa majimaji yaliyoashiria uwepo wa mizigo waliyotilia shaka.
 
Katika eneo la tukio wananchi wakishirikiana na askari wa jeshi la polisi walivalia kiraia, walichukua shehena hiyo na kwenda kuiihifadhi sehemu salama, ambapo licha ya zoezi hilo kufanyika karahisi kwa kuvalia gloves bila ya maski za puani, huku baabdhi ya wadadisi wa mambo wakisema huwenda zoezi hilo likawa na madhara kwa wahusika kwani viungo hivyo havikujulikana mara moja vilikaushwa kwa dawa gani.
 
kamandaa wa polisi mkoa wa kipolisi kinondoni Acp Camilius Wambura amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa bado jeshi linaendelea na upelelezi ili kujua hiyo mifuko zaidi ya 85 yenye viungo vya binadamu vikiwa vimekaushwa kwa ustadi vimetoka wapi na pindi uchunguzi utakapo kamilika watatoa majibu.

No comments:

Post a Comment