Friday, 3 February 2012

WAZIRI ATANGAZA UKATA SERIKALINI

0diggsdigg
Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika

SERIKALI imekiri kuwa hali yake kifedha ni mbaya, ndiyo maana halmashauri nchini hazina fedha za kuendesha mambo mbalimbali ya kiutendaji.Desemba 6 mwaka jana gazeti hili liliripoti kwamba Serikali inakabiliwa na ukata uliosababisha wizara, idara na taasisi za Serikali zikiwamo baadhi ya vyuo vyake vikuu, kushindwa kufanya baadhi ya kazi zake, lakini Serikali ilikanusha.

Jana, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Singida Magharibi, Mohammed Missanga alikiri ukata huo na kueleza kuwa ni tatizo kubwa.

Missanga alitaka kupata kauli ya Serikali kuhusu ukata uliozikumba halmashauri nchini kwa kukosa fedha kutoka Serikali Kuu, kitendo ambacho kimesababisha zishindwe kufanya mambo mbalimbali ya kiutendaji ikiwamo kuendesha vikao vyake na kusimamia maendeleo ya miradi.

Akijibu swali hilo, Mkuchika alisema  halmashauri zina tatizo kubwa la fedha ambalo linasababisha baadhi ya mambo ikiwemo kufanyika kwa vikao vya kiutendaji kusimama. Aliongeza 'Kiwango cha fedha ni kidogo na hili liko mikononi mwa Waziri Mkuu."

Alisema tatizo hilo ni kubwa mpaka Chama cha Serikali za Mitaa (ALAT) kimeomba kukutana na uongozi wa juu wa Serikali, ili kuzungumzia tatizo hilo.

Mkuchika alisema katika halmashauri zote nchini hivi sasa kuna matatizo makubwa yanayotokana na ukata wa fedha ambazo kwa muda mrefu hazijapelekwa huko, huku akikiri pia hata fedha za mwaka jana hazijapatikana. Katika kuthibitisha tatizo hilo, Waziri huyo pia alishindwa kueleza lini fedha hizo zitapatikana na kupelekwa kwenye halmashauri.

“Hata za mwaka jana hatujapeleka huko ndio maana wanalalamika, hata ALAT wameomba kukutana na uongozi wa juu serikalini kuzungumzia jambo hilo, lakini, kwa ujumla hali ni mbaya,’’alisema Mkuchika.

Ukata huo ulisababisha kuchelewa kwa ruzuku ya vyama vya siasa vyenye wabunge na madiwani, hali iliyoathiri uendeshaji wa shughuli za ndani za vyama hivyo kikiwamo chama tawala, CCM.

Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC), Augustino Mrema alisema ukata huo umesababisha miradi mingi kukwama kutokana na bajeti iliyopitishwa kutotekelezeka.

Alisema ni kweli Serikali inayumba kwa kuwa hali ya fedha ni mbaya. "Alichosema  Mkuchika ni sahihi na nampongeza kwa kukiri kuwa hawana fedha kwa kuwa mambo hayaendi kabisa huko kwenye halmashauri."

Mrema aliongeza, "Kwa mfano kule Himo waliniambia  wangenipa Sh150m kwa ajili ya mradi wa maji, lakini hadi hivi sasa wametoa Sh50 milioni ambazo haziwezi kufanikisha mradi huo."

mwananchi

Thursday, 2 February 2012

POSHO ZA WABUNGE TAYARI ZINALIWA

 
Spika wa Bunge Anne Makinda.
-Yasema wabunge waliachiwa wapime
-Spika Makinda asema zilipata baraka
WAKATI Spika wa Bunge Anne Makinda, akithibitisha kuanza kulipwa posho mpya za Sh. 200,000 kwa kila kikao cha Bunge baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kibali; Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imekana kuidhinisha viwango hivyo.
Taarifa fupi ya Kurugenzi hiyo iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana ilieleza kwamba “Rais Kikwete anakubali haja ya kuangalia upya posho kwa wabunge, lakini amewataka wabunge kutumia hekima na busara katika kulitafakari suala hili.”
Taarifa hiyo iliyolenga kueleza maelekezo ya Rais kuhusu posho za wabunge ilisema aliwataka wabunge kutumia Mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma hivi sasa “kulizungumza upya suala hilo.”
Ikiwa huo ndio msimamo wa Ikulu, Makinda aliwahakikishia waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge jana asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu kwamba wabunge wamekwishaanza kulipwa posho mpya.
“Sio kwamba tutaanza kutoa, tulishaanza kutoa na Rais (Jakaya Kikwete), ameshatoa kibali chake na mbunge atalipwa katika vikao tu, si kila siku na tena baada ya kukaa kwenye vikao na kusaini,” alisema.

Alisema posho hiyo iko katika waraka wa serikali kuhusu posho uliotolewa Julai mwaka jana. Kutokana na waraka huo, wenyeviti wanapata Sh. 200,000, wajumbe ni Sh 150,000 na wengine Sh. 100,000.

Alisema mtu mwingine akipata mshahara unakuwa wake na familia yake, lakini kwa mbunge si hivyo kwa kuwa kuna watu wengi ambao wamekuwa wakihitaji misaada yao
.

“Wabunge wengine wanaondoka na mshahara wa Sh. 45,000 kwa mwezi wengine Sh. 100,000, wanachopata ni kidogo sana kwa kwa sababu utendaji wake wa kazi ni mgumu,” alisema.

Makinda aliyekuwa ameongozana na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah pamoja na maofisa wengine wa Bunge, alisema wabunge wengine wamekuwa wanakopa hadi mafuta ya kwenda bungeni na kwamba si matajiri kama wengine wanavyosema.

Alisema wapo wabunge wengine ambao hufariki dunia muda mfupi mara baada ya kumaliza kipindi chao cha ubunge, “Anamaliza ubunge Februari anakufa, kiinua mkongo chake (gratuity) ameshakopa leo ikifika mwaka 2015 hana kitu.”

Alisema hali hiyo inatia uchungu sana na kwamba hawana la kufanya kuhusiana na jambo hilo na badala yake wanafanya kazi.

Mbali ya posho, kwa mwezi mbunge analipwa mshahara wa Sh. milioni 2.3 na akikatwa kodi anabakiwa na Sh. milioni 1.7 ambazo pia hukatwa mkopo anaokuwa amekopa benki ukiwemo ule wa gari.

Vyanzo vya habari kutoka kwa wabunge vinasema kuwa wabunge wana mlolongo wa madeni ambayo hutokana na maamuzi yao ya kukopa fedha nyingi kutoka taasisi za fedha.

“Wapo waliokopa hadi Sh. milioni 200 mzee, si unajua tena mkutano wa kwanza wa Bunge ukianza tu mabenki nayo hayalazi damu, wanashawishi wabunge wanakopa. Sasa ukikopa halafu hukuwekeza si unajua fedha inavyoteketea, ununue gari la kifahari na mbwembwe nyingine, mara ulipe madeni ya kampeni, yaani baada ya miezi minne huna kitu,” alisema mbunge mmoja aliyeomba jina lake lisitajwe kwa kile alichosema suala la posho kwa sasa ni nyeti mno katika korido za Bunge.

Naye mbunge machachari wa Kigoma Kusini (NCCR), David Kafulila, ambaye yuko kwenye mzozo na chama chake kilichomfukuza uanachama, alisema kinachosumbua kwa sasa ni kukosekana kwa mfumo wenye usawa wa ulipaji mishahara na posho ndani ya serikali.

Kafulila alisema ni aibu kuona daktari akilipwa mshahara wa Sh. 900,000, lakini wapo maofisa wadogo tu katika mashirika ya umma kama Benki Kuu (BoT) au Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanachota hadi milioni saba kwa mwezi.

“Angalia Gavana wa Benki Kuu analipwa mshahara wa Sh. milioni 20, Mkurugenzi wa NSSF Sh. milioni 18, mbunge Sh. milioni 1.8, daktari Sh. 900,000,” alisema na kuhoji hapa haki iko wapi.

Aliongeza kwamba waziri akisafiri nje ya nchi posho yake kwa siku ni Dola za Marekani 420 (sawa na Sh. 672,000) lakini Mkurugenzi wa Mkuu wa Shirika lililo chini yake anachota Dola za Marekani 800 (Sh. 1,280,000) kwa siku.

Kuna watumishi wa umma wako hoi sana, walimu, mahakimu na hata ndani ya serikali wapo wasiojua kesho watakula nini: “Tatizo ni la kimfumo zaidi, tunahitaji kuufumua na kuusuka upya. Hii ndiyo njia pekee ya kutibu matatizo haya.”

chanzo:nipashe

Wednesday, 1 February 2012

Bomb attack rocks Malmö police station


Bomb attack rocks Malmö police station


A police station in central Malmö was hit by a powerful explosion early Wednesday morning, leaving a hole in the building.

“Several people reacted to the powerful explosion and we received a number of calls,” Skåne police duty officer Marie Keimar told the TT news agency.

Two men dressed in dark clothing were seen placing what is believed to be a bomb outside the building before fleeing the scene.

The blast, which took place around 2.30am, left a hole in the police station's brick wall and caused extensive damage to the offices inside.

Police say there are a number of witnesses to the incident, but Keimar was unable to elaborate on what witnesses may have said about what they saw.

However, eye witness Tomas Holmqvist told Svergies Television (SVT) that he had seen two men dressed in black place the charge outside the station.

The two men then fled the scene on a black scooter.

The police station singled out in the attack is located on Eriksfältsgatan in central Malmö.

According to police, there were people present in the station shortly before the explosion occurred.

“It was lucky there wasn't anyone in there, but it was still a serious attack against us,” said Keimar.

“It's unclear how seriously the building was damaged or if there is any risk that it might collapse.”

By 4am, investigators had begun examining the scene in order to assess the damage.

The police station is located in Malmö's Fosie neighbourhood, the same area where a man was fatally shot just hours before.

Shortly before 7pm, police found a 48-year-old father of four shot in a car. He was rushed to hospital but later died from his injuries.

TL

MILTON!SOON 1 YEAR BIRTHDAY



maganga wangu anaendelea vizuri asante mungu,muda si mrefu tutasherehekea siku yake ya kuzaliwa na kutimiza mwaka

ICTR yawaombea hifadhi walioachiwa huru


 31 Januari, 2012 - Saa 18:46 GMT

ICTR
Majaji katika mahakama ya ICTR
Mahakama inayoendesha kesi za mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda mwaka 1994 imetoa wito kwa mataifa kutoa hifadhi kwa wale walioondolewa mashtaka.
Watu 5 kati ya watu 10 walioondolewa lawama za kuhusishwa katika mauaji hayo wanasema hawawezi kurejea nchini Rwanda.
Wanaishi chini ya ulinzi wa Polisi katika nyumba moja mjini Arusha, Tanzania, ambako ndiko makao ya mahakama hiyo ya ICTR.
Mahakama hiyo ya ICTR inatarajiwa kufunga mwishoni mwa mwaka huu.
Watu 800,000 kutoka jamii ya waTutsis na waHutus wenye msimamo wa kadiri waliuwawa katika kipindi cha siku 100 nchini Rwanda mwaka 1994.
Msemaji wa ICTR Roland Amoussouga ameambia BBC kupatikana nchi za kuwahifadhi wale ambao hawakupatikana na hatia ndio changamoto kuu inayokabili mahakama.
"Ni mzigo mkubwa kwetu kuendelea kuwahifadhi watu hawa walioachiwa huru kwa muda wa miaka mingi hivi, na tumeshirikiana nao, pamoja na mawakili wao kutafuta nchi ambako wanaweza kupelekwa. Hadi sasa hatujafanikiwa," alisema.
Wote 5 walioko mjini Arusha ni kutoka kabila la waHutu na miongoni mwao ni afisa wa zamani wa jeshi wa cheo cha Brigadier generali, mawaziri wa zamani na mfanya biashara mmoja.
Wanaishi pamoja katika nyumba inayolindwa, wanaweza kwenda mjini na kanisani, lakini hawawezi kuondoka huko.
Waziri wa zamani wa uchukuzi Andre Ntagerura amekuwa akisubiri kupata hifadhi kwa kipindi cha miaka 6 tangu mashtaka dhidi yake yalipoondolewa.
Wengine wawili wameshatumika vifungo vyao lakini hawana pa kwenda.
Wote wana familia nchini Ubelgiji, Canada na Ufaransa lakini hadi sasa hawawezi kupewa vibali kujiunga na familia zao, licha ya maombi kutoka baraza la usalama la umoja wa mataifa.

bbcswahili

sakata la posho:jk amkana pinda na makinda

ASEMA ALIWATAKA WATUMIE BUSARA,  SPIKA ASISITIZA ALIRUHUSU, WANANCHI WACHACHAMAA

Waandishi Wetu
SIKU moja baada ya Waziri Mkuu Mkuu, Mizengo Pinda kusema tayari Rais Jakaya Kikwete amesaini kuidhinisha ongezeko la posho za vikao (sitting allowance) kwa wabunge kutoka Sh70,000 hadi Sh200,000 kwa siku, Ikulu imetoa taarifa kukanusha madai hayo.Wakati Ikulu ikitoa taarifa hiyo, jana Spika wa Bunge, Anne Makinda aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema: “Siyo kwamba tutaanza kutoa, tulishaanza kutoa na Rais (Jakaya Kikwete), ameshatoa kibali chake na mbunge atalipwa katika vikao tu, si kila siku na tena baada ya kukaa kwenye vikao na kusaini.”
Lakini katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imesema: “Maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu suala hili yako wazi kabisa na hakuna mahali ambako Rais Kikwete amebariki posho hizi.”
“Kwanza, Mheshimiwa Rais Kikwete anakubali haja ya kuangalia upya posho kwa wabunge lakini amewataka wabunge kutumia hekima na busara katika kulitafakari suala hili. Pili, Mheshimiwa Rais Kikwete amewataka wabunge kutumia Kikao cha sasa cha Bunge kulizungumza upya suala hilo.”

Juzi, Pinda aliwaambia wabunge ndani ya kikao cha utangulizi kuwa tayari Rais Kikwete alikuwa ameidhinisha ongezeko la posho za vikao kutoka Sh70,000 hadi Sh200, 000. Baada ya Waziri Mkuu kusema hivyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) alisimama na kudai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba Rais Kikwete alikuwa hajasaini kuidhinisha posho hizo.

Kauli ya Zitto ilisababisha Mbunge wa Kondoa Kaskazini (CCM), Juma Mkamia kusimama na kuhoji iwapo Zitto ni miongoni mwa wasemaji wa Rais kabla ya Pinda kusimama na kuthibitisha kusainiwa posho hizo akisema, siyo ajabu  kwani hata watumishi wa Serikali wanalipwa kati ya Sh50,000 na Sh200,000.

Hata hivyo, Zitto alitetea msimamo wake kwamba alitarajia baada ya kusainiwa kwa posho hizo na Rais, angepewa masharti mapya ya kazi za ubunge. Wengine walioshambuliwa katika kikao hicho ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba na Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Khamis Kigwangwallah kwa kupinga posho hadharani.Wanaodhaiwa kuwashambulia wabunge hawa wanaopinga posho ni Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, Mbunge wa Sikonge,  Said Nkumba, Nkamia na Mbunge wa Gando (CUF),  Khalifa Suleiman Khalifa.

Jana baada ya kuripotiwa kwa habari hiyo wananchi kutoka kila kona ya nchi walipinga huku wasomi wakitahadharisha kuwa kitendo hicho kinaweza kuligawa taifa.

Wananchi wa kada mbalimbali waliotuma maoni yao kwenye mtandao wa gazeti hili na wasomi ambao walihojiwa walisema kwamba kitendo hicho ni hatari hasa katika kipindi hiki cha mgomo wa madaktari.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Profesa Gaudence Mpangala alisema nyongeza hiyo inaleta utata na kwamba inaonyesha wazi kuwa nchi inanyemelewa na dalili za kuwepo kwa matabaka... “Hii inaonyesha kuwa wapo wanaopendelewa na wengine wanaminywa, jambo hili kiutawala si zuri hata kidogo linaweza kuleta migomo na maandamano nchi nzima.”

Alisema Serikali inatakiwa kuzitazama sekta nyingine huku akitolea mfano mgomo wa madaktari na kuongeza: “Yaani baada ya kutatua hali hii ya mgomo wao ndiyo wanapandisha posho za wabunge. Gharama za maisha ziko juu sana, hilo lazima Serikali ilitambue.”

Mhadhiri mwingine mwandamizi wa chuo hicho, Dk Kitila Mkumbo alisema kauli ya Waziri Mkuu Pinda imetoa majibu sahihi kwamba Serikali ina fedha za kutosha za kuwalipa madaktari.”

“Pinda alikaririwa akisema kuwa Serikali haina fedha za kuwalipa madaktari, lakini hizo za kuwalipa wabunge zimepatikana, sijui hapa inakuwaje?,” alihoji Dk Mkumbo.

Alisema kiwango cha fedha za nyongeza hizo za posho ambacho watalipwa wabunge katika kikao cha Bunge la Juni, zinaweza kuwalipa madaktari waliogoma nchi nzima.

“Mwezi wa sita wabunge hukaa bungeni miezi miwili, sasa ukipiga hesabu za haraka haraka kiwango cha posho watakazolipwa kinatosha kabisa kumaliza kero ya madaktari,” alisema Dk Mkumbo.

Kwa upande wake, Mhadhiri mwingine wa UDSM , Dk Benson Bana alielezea kushangazwa kwake na kitendo cha Serikali kupandisha kiwango cha posho licha ya kuwa suala hilo limepigwa kelele na wananchi... “Posho za vikao (Sitting allowances) siyo kipaumbele chetu, posho hizi hazina uhusiano na utendaji wa mbunge.”

Alisema suala hilo licha ya kutia wasiwasi, linaibua maswali mengi kwa kuwa walimu na madaktari nao wanataka kulipwa vizuri ikiwa ni pamoja na nyongeza ya posho.

“Ningewaelewa kama wangeongeza mishahara ya wabunge lakini siyo posho…, posho ambazo wanalipwa katika saa za kazi, haiingii akilini hata kidogo.” alisema Dk Bana.

Naye Profesa Tolly Mbwete wa Chuo Kikuu Huria (OUT), alisema nyongeza hiyo ya posho inatakiwa kufanyika katika sekta zote ili kupunguza malalamiko ya watu wa kada mbalimbali. “Binafsi naona suala hili linatakiwa kutazamwa katika sekta zote kuliko kujikita kwa wabunge tu.”
Mwanasheria wa kujitegemea, Profesa Abdallah Safari alisema posho hizo hazina mashiko kwa kuwa wanaolipwa wanakuwa katika majukumu yao ya kazi ambayo huwafanya walipwe mshahara mwisho wa mwezi.

Spika atetea
Spika Makinda, jana aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake kwamba wabunge wameshaanza kulipwa posho mpya za Sh200,000 kwa kila kikao kuanzia Bunge lililopita akisema ni baada ya idhini ya Rais.
Alisema posho hiyo iko katika waraka wa Serikali  kuhusu posho uliotolewa Julai mwaka juzi akisema wenyeviti wanapata Sh200,000, wajumbe Sh150,000 na wengine Sh100,000.
Kitendo cha kuongezeka kwa posho za wabunge kinaiweka Serikali katika wakati mgumu kutokana na watu wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, wanasiasa, wanaharakati na wasomi kuzipinga.
Hata hivyo, Makinda alisema ni jambo la kawaida kwa wananchi kuhoji uhalali wa posho za wabunge wakati mishahara ya wengine haihojiwi.
“Mtu mwingine akipata mshahara unakuwa wake na familia yake lakini, kwa mbunge si hivyo kwa kuwa kuna watu wengi ambao wamekuwa wakihitaji misaada kutoka kwa wabunge na hivyo si jambo la kawaida zinapoongezwa posho,’’ alisema na kuongeza:
“Wabunge wengine wanaondoka na mshahara wa Sh45,000 kwa mwezi wengine Sh100,000, wanachopata ni kidogo sana kwa kwa sababu utendaji wake wa kazi ni mgumu.”
Makinda aliyekuwa ameongozana na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah pamoja na maofisa wengine wa Bunge alisema wabunge wengine wamekuwa wanakopa hadi mafuta ya kuja bungeni na kwamba si matajiri kama baadhi ya watu wanavyofikiri.
Alisema wapo wabunge ambao hufariki dunia muda mfupi mara baada ya kumaliza kipindi chao cha ubunge kutokana na ugumu wa maisha.
“Anamaliza ubunge Februari anakufa, kiinua mgongo chake  ameshakopa leo ikifika mwaka 2015 hana kitu unadhani inakuwaje hapo?”

mwananchi