Thursday 18 February 2010

STOCKHOLM SODRA WITH VUMBI DEKULA BAND

mimi na bella mdau namba moja wa blog ya mipakazo,siku hiyo tulikua na furaha zetu tukaamua kupakaza na kweli mambo yalienda kama inavyotakiwa wadau kama mnavyoona picha hapo chini.
hapo nimimi mwenyewe na bwana mkubwa ndizii,au banana ukipenda muite mzee wa..........!
hapa nikiwa na mtaalamu mwenyewe mukulu vumbi kahanga dekula.
hawa wataalamu wanakung`uta vingoma hivyo kama tumba yaani tunapata burudani kamili kwakweli-
pia kuna mtaalam wa gitaa kasule kutoka jirani na huyo mdada mkewe namuitaga J,LO wote wanawajibika timu imekamilika.
mtu nyomi kama mango garden vile watu wakisebeneka
naona mtaalamu akirekebisha mic,jamaa ni mkali sana kwa kuimba copy,akikuimbia wimbo MAZE wa tabu ley utafurahi maana anaimba utasema mwenyewe`rochereau´yuko pale big up.

ndugu yetu onyango toka hapo jirani kwa obama nayeye akijumuika nasi kama kawa sodra east africa "dugu moya"

No comments:

Post a Comment