Sunday 13 April 2014

Mzee Gurumo amefariki dunia R.I.P

R.I.P MUHIDIN GURUMO

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Dansi nchini Tanzania ambaye alitangaza kustaafu mwaka uliopita Muhidin Maalim Gurumo amefariki dunia leo April 13, 2014 saa 9 Alasiri katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Taarifa kutoka kwa meneja wake zinasema kuwa Marehemu mzee Gurumo alikuwa akisumbuliwa na taizo la mapafu kujaa maji.

Mipango ya mazishi inafanywa mara baada ya familia yake kukutana kwa kushirikiana na Chama cha Muziki Tanzania.

No comments:

Post a Comment