Friday 11 April 2014

Mvua yasomba tuta la reli ya Tazara.


 Shughuli za uchukuzi wa mizigo toka bandarini kwenda mikoani na nchi za jirani kwa njia ya reli ya Tazara zitasimama kwa siku saba,kufuatia  maji ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar-es-Salaam,kusomba tuta la reli ya tazara umbali wa mita arobaini na kuacha mataruma ya reli hiyo yakining'inia.
Meneja mkuu wa mkoa wa mamalaka ya reli ya Tanzania na Zambia Tazara, mhandisi Abdalah Kimweri amesema kuwa mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar-es-Salaam,zimeathiri miundombinu ya mamlaka hiyo umbali wa kilometa nane kati ya maeneo ya kurasini na yombo jijini Dar-es-Salaam.
Mhandisi huyo medai kuwa,katika maeneo mengi inapopita reli hiyo hasa jijini Dar-es-Salaam,makambako mkoani njome na tunduma jijini mbeya baadhi ya wananchi wamejenga karibu kabisa na reli hiyo jambo ambalo ni hatari kwao na kwa reli ya Tazara na kudai kuwa tayari wameisha wajulisha wananchi kuondoa maendeleo yao kabla ya hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.
Mhandisi ujenzi wa mamlaka hiyo ya Tazara kwa upande wa Tanzania mhandisi Richard Festo,amesema kuwa katika maeneo ya temeke jijini Dar-es-salaam,ujenzi holela wa mfumo wa mitaro kuelekezewa kupita kwenye njia ya reli kumechangi kwa kiasi kikubwa kuchangia kuharibu miundombinu ya mamlaka hiyo,huku baadhi ya wananchi wakitaka kulipwa fidia kwa makaburi yao yaliyosombwa na maji.
Reli ya tazara yenye historia ya urafiki baina ya nchi tatu za Tanzania ,Zambia na uchina ikiwa na urefu wa kilometa 1860 kutoka jijini Dar-es-salaam nchini Tanzania hadi new kaplimposhi nchini Zambia ,iliyoanza kutumika kusafirisha abiria na mizigo kwenye mikoa ya Pwani,Morogoro,Iringa na Mbeya iliyo anza kutoa huduma hiyo mwanzaoni mwa miaka ya 1976 ikiwa imejengwa na kampuni kutoka China.

source.itv

No comments:

Post a Comment