Wednesday 5 March 2014

MAZISHI YA MAREHEMU HUSSEIN SAID HUSSEIN 6/03/2014 - MÄRSTA

Kwa Jumuia ya Watanzania na Marafiki


MAZISHI YA MAREHEMU HUSSEIN SAID HUSSEIN 6/03/2014 - MÄRSTA

Ubalozi umepata taarifa leo asubuhi toka kwa Bi Victoria Hussein, mjane wa Mtanzania mwenzetu Marehemu Hussein Said Hussein kwamba mazishi yatakuwa kesho Alhamisi 6/03/2014 saa 5.30 (tano na nusu)asubuhi. 

Swala ya mazishi itaongozwa na Imaam Zakir na itafanyika Husby Ärlinghundra Kyrkogård, Husby Kyrkby 131, 195 91 Märsta

Baada ya mazishi wote wanakaribishwa kuungana na familia kwa chakula cha mchana katika Mgahawa wa Arlandastad uliopo Pionjärvägen 2, Arlandastad.

Kwa maelezo zaidi tafadhali piga simu Na. 0705263303 kwa Bw. Tengo Kilumanga

Atakayepata taarifa hii amwarifu na mwingine.

Ubalozi wa Tanzania
Stockholm

No comments:

Post a Comment