Sunday 1 June 2014

DIAMOND AGONGA SHOW YA NGUVU NEW JERSEY U.S

Mwanamuziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz anayekimbiza vibaya mno kwenye anga za Bongo Flava akipagawisha mashabiki wake New Jersey nchini Marekani.
Diamond na madancer wake wakijaribu kukata kiu ya mashabiki wake wa pwani ya mashariki.
 Wapenzi wa Diamond wakipagawa na show ya Diamond iliyofanyika All Star Club Elezabeth NJ.
Shabiki akidata na show ya prezidaa wa Wasafi.
Shabiki mwingine akidatishwa na moja ya wimbo wa Diamond na kushindwa kujizuia kupanda jukwaani.
Mashabiki wa Diamond wakipagawa huku wengine wakipata taswira za hapa na pale.
 All Star Club Elizabeth New Jersey; Diamond akikamua licha ya show kuchelewa kuanza na wapenzi wa Diamond kushikwa na jazba wakitaka aendelee lakini ikashindika kutokana na muda wa kufunga club kufika.
 AJ nae akifanya yake baada ya kupewa nafasi ya ufunguzi katika show hiyo iliyofanyika New Jersey.
AJ Ubao na Dirty Hary wakishambulia jukwaa kwenye show ya kufungua pazia iliyofanyika New Jersey na baadaye Prezidaa wa Wasafi, Diamond Platnumz kuwapagawisha mashabiki wake wa ukanda wa pwani ya mashariki.
Ni Rais wa Wasafi akishambulia jukwaa akiwa na madancer wake kwenye show ya kukata na shoka iliyofanyika New Jersey na kuvuta mashabiki kutoka kila kona ya pwani ya mashariki ambayo ni DC, PA, NJ, NY, CT, MA na kwingineko.
(Picha zote na Vijimambo Blog)

No comments:

Post a Comment