Monday 16 September 2013

Aliyesema Utu uzima dawa namkubali


Mr Isaackin.
Kwa hilo sasa  nauona utu uzima unaingia kwangu  kwa Fujo.nashindwa kukataa maana ndio hali halisi.
Nikikumbuka miaka hiyo sielewi kama ndio Mimi huyu sasa.enzi hizo sijui mashaka gani utauliza sikupitia.wakati nachipukia nilianza na kucheza mabreka,badae nikahamia kwenye kiwanzenza na ndombolo za solo.kutoka hapo ikaja zamu ya vitobo.
Hapo nilipitia Mechi za mchangani,kwenye ligi za kombe la mbuzi mpaka Mechi kubwa kubwa za kitaifa.
Hapo Mechi za ndani nilipiga mpaka zile
Za majaribio kucheza mechi kimataifa.kitengo hicho nilipitia kuanzia kamata nchinje,waluwalu,mwajuma ndala ndefu,n...e nkale,beki tatu.toto za geti saana,mpaka wale popooooz.
Nikachoka nikaanza kugonga Mechi za kimataifa,huko nako nilipiga Mechi kadhaa around kabla ya kufikia maamuzi ya kufunga ndoa
Nilifunga ndoa lakini bado Mechi za ugenini zikaendelea.
Kwa ujumla kitengo cha vitobo ndio nilidumu mpaka hivi karibuni.
Baada ya kupitia mambo yote hayo kwakweli kwasasa najiskia kuchoka.siku hizi pilika zimepungua sana,kwasasa niko kati ya miaka 35-40  na mabadiliko nayaona.
Sasa naweza sema nimekumbuka shuka wakati hakujakucha.mipakazo  sio Kivile sana zaidi ya ku concentrate na maisha yangu.
Nashukuru pia wa midomo vuvuzela maana mlipiga sana firimbi kipindi kile.nia yenu najua ilikua kubomoa lakini imefanya kinyume imejenga.
Asanteni Kazi nzuri endelezeni kwa wengine.
Kwasasa raia tupigiane simu AMA kualikana mambo ya msingi.discussion za nani Ana makaratasi nani hana zishapitwa na wakati.Sweden washatangaza watatoa makaratasi kwa Kila mtu baadae tuende sawa.msikonde sana kuhusu Hilo hatutakuja makwenu kuwamalizia ugali na vibawa.

Kuna wale pia wanaodhani nikimualika Isaac anaongea sana na atamaliza whiskey yenu msikonde mialiko Hiyo siku hizi siitaji sina muda.usipoteze Kadi yako wala SMS kunitumia sihitaji sana ntakutukana kwa unafki.
Wale 


Wapakazaji wenzangu aaaah tutaonana in gawk hatukeshi
Alamsiki

No comments:

Post a Comment