Friday 20 September 2013

Masogange na mwenzie wapata dhamana

SHARE

 BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa 
Na Florence Majani

Posted  Ijumaa,Septemba20  2013  saa 24:0 AM
KWA UFUPI
  • Ni katika Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko Johannesburg, Lakini wataendelea kubaki nchini humo wakati kesi dhidi yao ikiendelea.
SHARE THIS STORY
 
 
 
0

Share
Johannesburg. Watanzania Agness Masogange na Melisa Edward waliokamatwa kwa kutuhumiwa kubeba dawa za kulevya huko Afrika Kusini wameachiwa kwa dhamana.
Mkuu wa Kitengo cha Dawa za Kulevya Afrika Kusini, Kamishna Toto Mangaleni aliithibitishia Mwananchi jana kuwa watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana,lakini wataendelea kubaki Afrika Kusini wakati kesi yao ikiendelea.
Mangaleni alisema wanawake hao ambao juzi pia walipanda kizimbani, walipata dhamana hiyo jana kutoka Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko eneo la Kempton Park jijini Johannesburg.
Hata hivyo, Kamishna Mangaleni alisema hawezi kuzungumzia zaidi kuhusu kesi hiyo kwa sababu hataki kuharibu uchunguzi ambao unaendelea dhidi ya Watanzania hao, ambao ni wasanii.
Marafiki wa karibu wa Masogange wanaoishi maeneo ya Midland Johannesburg ambao walikataa kunukuliwa majina yao, walithibitisha kuwa wanawake hao wameachiwa kwa dhamana.
“Ni kweli wameachiwa leo asubuhi. Lakini hatuwezi kuongelea kwa kina habari hizi kwa sababu hatutaki matatizo na polisi. Hii kesi bado inaendelea na wataendelea kubaki hapa hadi kesi yao itakapomalizika,” alisema mmoja wa marafiki zake.
Naye Masogange aliandika kwenye mtandao wa ‘Facebook’.
“Namshukuru Mungu nimeamini wewe ulikuwa pamoja na mimi katika maombi yangu na nashukuru kwa wote mliokuwa mkiniombea Mungu kapokea maombi yenu.”
Masogange na Melissa walikamatwa Julai 2 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg wakiwa wana mabegi sita makubwa ya dawa zinazoaminika kuwa ni `Crystal Methyl Amphetamine’.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aliiambia Mwananchi jijini Dar es Salaam kuwa alikuwa amepata taarifa za kuachiwa kwa wasichana hao, lakini alikuwa anawasiliana na watu wa Afrika Kusini ili kupata uhakika.
Nzowa, hata hivyo alilidokeza gazeti hili juzi kuwa kuna uwezekano wanawake hao wangepata dhamana au kufungwa kifungo chepesi kwani dawa walizokamatwa nazo ni kemikali zinazotumika kutengeneza dawa za aina tofauti kwa matumizi ya binadamu ingawa pia na dawa za kulevya.
Mamlaka yapinga uamuzi wa Mahakama

Chanzo:mwananchi

No comments:

Post a Comment