Thursday 30 May 2013

HABARI GANI KIFO!!



Kifoo we kifoooo,haya leo umemwondoa ngwea kesho utamchukua nani kifo wee?lile gheto lake la k'nyama unapangisha bei gani tukulipe sasa ufurahi
.kifo ulimwondoa kanumba kabla hajamaliza asali ya lulu kifo kwanini usingoje amalize?
kifo ukamwondoa sharo mali-onea wakati bado yuko njiani kumpelekea mamaake hela ya ubwabwa
.kifo uliwahi kumuondoa rafiki yangu j3 huku nikiwa nimeagana nae j4 nimpelekee pesa ya eid kwanini?kifo ni ww tu ulimuondoa babaangu akiwa na siku moja tu kutoka mjini daslaam hata zawadi alizotuletea hatujafungua kaenda kukutana na rafiki yake ikawa ndio kimoja.
kifo ukamuua hata mjomba wangu mikononi mwangu kwa uchungu mkubwa ndio nikakujua we katili sana.
Bado wakati nakutafutia dawa ya panya kifo na mimi ukanionjaonja kunimaliza,mi sikukwambia lakini kama nimechoka kula ugali ukataka kuniondoa mpaka sasa naona mawenge wenge tu.
sasa bwana kifo imefika mda tumalize tofauti maana mi nimechoka kulia,bora ningemjua ndugu yako japo mmoja nimfanye km we unavyotufanya tuelewane lugha.ila ndio hivyo kila siku nalia mimi tu bora tuelewane bana.
kama we wa kike basi bora nikuoe tu ili uwapende ndugu zangu na marafiki badala ya kuwaua,kama wewe wa kiume basi bora useme unakaa wapi nije nikulipe.sitakuja kulipa kisasi kifo,bali kukulipa na kukuletea zawadi na nishani maana we ni shujaa sana.

Shikamoo kifo na gdnyt!
By mtu mdogo sana

No comments:

Post a Comment