Thursday 19 January 2012

TANZANIA YAWASILISHA OMBI KUDAI ENEO LA NYONGEZA KATIKA BAHARI


 Kutoka  kulia ni Mhe. Zakhia Meghji ( Mb), Bw.  Sergei Tarassenko ambaye ameshika sehemu ya nyaraka za Andiko la kudai eneo la maili 61,000 za bahari, Mhe. Waziri Anna Tibaijuka ( Mb), Mhe. Ombeni Sefue, Balozi wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa,  Mhe. Abulrahman Hassan Shah (Mb) na Bw.  Ayoub Mohamed Mahmoud  Mkurugenzi  wa Sera   na  Mipango Wizara ya Ardhi, Makazi na Madini  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia alimwakilisha Waziri wake katika hafla hiyo.

 Ujumbe wa Tanzania  ukiwa katika  furaha kubwa na Mkurugenzi wa Idara ya Umoja wa Mataifa  ya masuala ya Bahari na Sheria ya Bahari Bw. Sergei Tarassenko  na maofisa wake ,mara baada ya makabidhiano ya Andiko la kudai nyongeza ya eneo la maili ya 61,000 za bahari lililowasilishwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Umoja wa Mataifa. katikati ni  Boksi ambalo ndani yake mnamakabrasha na nyaraka nyeti zinazo husu  Andiko la madai hayo, Andiko ambalo mchakato wake umechukua miaka mitano kuuandaa. Tanzania imewasilisha Andiko hilo kwa mujibu wa Sheria  ya kimataifa  ya masuala ya bahari namba 76 kifungu kidogo cha 4 ambayo inatoa ruksa kwa nchi ambayo iko kando kando ya bahari kudai nyongeza ya eneo la bahari endapo itakidhi  vigezo vilivyotolewa na Umoja wa Mataifa. Tanzania inakuwa nchi ya 59 kuwasilisha dai  hilo.

No comments:

Post a Comment