Saturday 3 March 2012

KIZAA ZAA MIMBA YA UWOYA



JAMBO limezua jambo! Ujauzito anaodaiwa kubebeshwa Irene Pancras Uwoya, umezua kizaazaa, Ijumaa limeshiba data.
Habari zilizozagaa kwenye ulimwengu wa mastaa wa Kibongo zinatonya kuwa, mwanaume anayedaiwa ‘kumshibisha’ Uwoya aliyetajwa kwa jina moja la Ababuu ambaye ni mwenyeji wa Kilimani visiwani Zanzibar, alikuwa mpenzi wa Jacqueline Wolper Masawe.
KUMBE!
Kwa mujibu wa vyanzo makini, kitendo cha Uwoya kuwa ‘klozi’ na mwanaume huyo ndicho kilichovunja uchumba wa Wolper ambaye alikuwa akisubiri ndoa.

NI KIZAAZAA
Wanyetishaji hao walidai kuwa, kwa sasa hali ni mbaya kwani Wolper amekuwa akilia kila kukicha akidai kuharibiwa ‘fyucha’ na Uwoya, jambo ambalo anaamini machozi yake hayawezi kupotea bure.

UNAKUMBUKA UWOYA NA WEMA WALIPOMCHANA WOLPER?
Habari zilizidi kupepeta kuwa, mwishoni mwa mwaka jana, Uwoya akishirikiana na Wema Sepetu walifunguka runingani ‘wakimpaka’ Wolper, kumbe kilichotokea ni kwamba walimzidi ujanja kwani yeye ndiye aliyepaswa kukimbilia kwenye vyombo vya habari baada ya kuzidiwa kete.
“Wolper alizidiwa ujanja kidogo tu, yeye ndiye aliyetakiwa kuwahi kulalamika,” kilisema chanzo chetu.

WOLPER LAIVU
Baada ya kujikusanyia data za kutosha, Ijumaa lilimvutia waya Wolper na kumsomea hatua kwa hatua taarifa iliyokuwa mezani, ndipo alipofunguka kila kitu.
Kwanza mcheza sinema huyo aliyepewa jina la Amber Rose wa Bongo alikiri kuwa Ababuu alikuwa mchumba wake huku akidai Uwoya amemharibia mipango yake ya ndoa na mwanaume huyo.
“Kama kweli mimba ni ya Ababuu, basi ni ya Ex-boy friend wangu.
  “Siyo siri, Uwoya amefanya ndoto yangu ya kuwa mke wa Ababuu kufutika.
“Nilipolalamika kwa mara ya kwanza, nilionekana natunga maneno na kusababisha ugomvi mkubwa, matokeo yake Mungu ameamua kunilipia, hebu ona sasa, anyway, Mungu anajua kilio changu.

KUNA BIFU?
Alipoulizwa mbona ana hasira na kama ana bifu na Uwoya, huku ikiaminika kuwa kuna kitu anachotaka kufanya ili kulipa kisasi, Wolper alisema:
“Sina bifu na Uwoya kwani mapenzi na Ababuu yalikwisha zamani, ya nini malumbano? Namtakia kila la kheri Ababuu.

UWOYA ANASEMAJE?
Wakati Uwoya akifunguka runingani mwaka jana juu ya mwanaume huyo, alidai Wolper alikuwa akijihisi tu baada ya kuona ukaribu wao lakini jamaa huyo alikuwa ni rafiki tu.
Juhudi za kumpata Uwoya ili kuzungumzia ishu hiyo kwa wakati hazikuzaa matunda kwani kila alipopigiwa simu, ilikuwa ikijibu call rejected hivyo zoezi la kumsaka linaendelea.

NDIKUMANA ATOA
TAMKO KUHUSU MIMBA YA UWOYA
Wakati huo huo, mume wa ndoa wa Uwoya, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ amezungumzia madai mazito yalioibuka hivi karibuni ya mkewe kuwa na kibendi nje ya ndoa.

NDIKU ASAKWA
Baada ya kuwepo kwa madai hayo, gazeti hili lilifanya jitihada za kumpata Ndiku bila mafanikio na hata alipopigiwa simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila majibu.

IJUMAA NYUMBANI KWA NDIKU
Jumanne wiki hii saa 1:00 usiku, mapaparazi wetu walifika katika nyumba aliyopanga Ndiku maeneo ya Sinza-Madukani jijini Dar es Salaam na kukuta taa zikiwaka huku milango ikiwa imefungwa.
Waandishi wetu walipojaribu kugonga, hakukuwa na dalili ya kuwepo kwa mtu ndani lakini waliendelea kusubiri getini kuona matokeo.

NDIKUMANA AKATAA KUONANA NA WAANDISHI
Badaa ya dakika takribani 15, ilisikika sauti ya kitasa cha mlango kikifunguliwa ambapo Ndiku alitoka akaonana na mgeni ambaye alikuwa akigonga geti na baada ya wawili hao kuingia ndani, jamaa huyo alibamiza geti huku akiwachungulia waandishi kwenye tundu la fensi.
Waandishi wetu walipogonga geti kwa mara nyingine, Ndiku alitoa sauti ya ukali ya kuwatimua hivyo wakaondoka.

NDIKU ATOA TAMKO
Baadaye Ndiku alituma meseji kwa mmoja wa waandishi hao akimtaka aeleze kilichowapeleka kwake, ndipo akaulizwa juu ya ujauzito wa mkewe na kama anajua mwanaume aliyesababisha, ndipo akatoa tamko:
“Mimi kama Hamad (Ndiku), siwezi kueleza juu ya hilo kwa sababu habari hiyo nimeisoma tu kwenye gazeti hivyo nashauri Irene mwenyewe ndiye anayetakiwa aeleze kila kitu.”

WATU WAMUONEA NDIKU HURUMA
Mara kadhaa, Ijumaa limekuwa likipokea maoni ya watu wa karibu wa Ndiku wakimsikitikia na kumuonea huruma kufuatia maisha anayoishi huku wengine wakishauri bora arudi kwao kuliko kuadhirika hapa Bongo.

chanzo:GPL

No comments:

Post a Comment