Tuesday 29 January 2013

LULU AKIWA URAIANI BAADA YA KUACHIWA LEO HII



 Lulu na mama yake mzazi wakilia baada ya kukutana nje ya Mahakama, Lulu amechiwa huru na Mahakama leo january 29 2013 mchana, pembeni ni mwigizaji Dr. Cheni ambae amekua karibu na familia ya Lulu kwa muda mrefu sana.
 Lulu akitokwa na machozi ya furaha
Lulu akiingia kwenye gari
---
Baada ya jana kushindikana kwa sababu zisizo zuilika hatimaye msanii maarufu Elizbeth 'Lulu' Michael ametoka kwa dhamana baada ya kutimiza masharti yote ya dhamana yake yaliyo tolewa na mahakama kuu.

Mara baada yakutoka Lulu alieyeonekana akiwa mwenye majonizi na furaha kiasi aliomba watanzania wote wamuombee maana hii ni dhamana tu na kesi yake bado inaendela. Ali washukuru watu wote waliokuwa pamoja nae katika mkasa huuu  amabao bado unamzunguka na pia alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa pamoja nae katika kipindi chote cha matatizo yanayo mkablia.

Wakili wake Ndugu Flugence Massawe amesema kwamba hii ni hatua ya kwanza kwasababu case bado inaendelea. Kwa sasa wanasubiri mahakama itoe tarehe ya Lulu kurudi mahakamani.

BY-KIFBLOG

No comments:

Post a Comment