Wednesday 18 April 2012

Wanunuzi wa ndege ya Rais Cameroon mbaroni




                                                                       Paul Biya

Viongozi wawili mashuhuri nchini Cameroon wamekamatwa kwa kuhusika na ununuzi wa ndege mbovu ya rais.

Wawili hao ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani Ephraim Inoni na aliyekua Waziri wa mambo ya ndani Marafa Hamidou Yaya.
Taarifa zinazohusiana

Afrika

Wanasiasa hao waliongoza ujumbe Marekani kununua ndege ya rais kwa jina Albatross, kwa gharama ya dola milioni 31. Rais Paul Biya, Mkewe Chantal na wanawe walikuwa kwenye ndege hiyo wakati ilipopata hitilafu ya mitambo, na kumlazimu rubani kutua ghafla.

Wakati huo Bw Yaya alikuwa katibu wa afisi ya Rais huku Inoni akiwa naibu wake. Baadaye Inoni aliteuliwa Waziri Mkuu na Yaya akapalekwa Wizara yenye ushawishi ya mambo ya ndani. Wadadisi wamesema Yaya alionekana kuwa mrithi wa kiti cha urais kabla ya kuachishwa kazi mwaka 2011.

Punde baada ya habari kutokea kukamatwa kwa viongozi hao, raia wengi walijitokeza kushuhudia wawili hao wakisafirishwa katika jela kuu la nchi.

Wengine ambao wanashikiliwa kufuatia sakata hiyo ni pamoja na Aliyekuwa Waziri,Jean-Marie Atangana Mebara, Balozi wa Zamani nchini Marekani,Jerome Mendouga na aliyekuwa mkuu wa shirika la ndege nchini Cameroon Yves Michel Fotso.

No comments:

Post a Comment