Saturday 2 February 2013

TWANGA , MASHAUZI ZAPAGAWISHA MAISHA CLUB, MANGO



Shabiki wa Mashauzi akionyesha uwezo wake.
Mashabiki wa Mashauzi wakizidi kujimwaya ndani ya Mango Garden.
Midundo ya taarab imewapandisha mzuka.
Waimbaji wa 'Twanga Pepeta', wakitumbuiza  Maisha Club.
Mcharaza gitaa wa Twanga, Miraji Shakashia, akisongesha burudani hiyo.
Wanenguaji wa wakitwanga na kupepeta.
Ilikuwa furaha mtupu.
Kiongozi wa Mashauzi Classic, Isha Ramadhan ‘Mashauzi', akiwajibika katika ukumbi wa Mango Garden.
Baadhi ya waimbaji wa Mashauzi wakitumbuiza.
Mwanaume ‘tata’ akiwa amevalia shanga tayari kwa kusakata taarab.
… Akicheza na rafiki yake.
BENDI za muziki wa dansi na taarab nchini,  African Stars 'Twanga Pepeta', na Mashauzi Classic, usiku wa kuamkia leo zimemwaga burudani ya kufa mtu katika kumbi mbili tofauti ambapo Twanga walikuwa ukumbi wa New Maisha Club, Msasani,  huku Mashauzi Classic wakiwa Mango Garden Kinondoni,  jijini Dar es Salaam.
          
 (Habari/Picha: Musa Mateja/GPL

No comments:

Post a Comment