Tuesday 7 December 2010

IVORY COAST NAKO TUNA MA-PREZIDAA WAWILI,KABINET ZA MAWAZIRI MBILI NA IKIWEZEKANA NA MA- BALOZI WAWILI WAWILI


president gbagbo aliyejitangaza mshindi baada ya kushindwa na kuchakachua kura live

prezidaa alasane outara
mshindi halisi kwa kura halali ambaye anatambulika

kichekesho sasa ni kwamba baada ya yule rais wa kwanza kuchakachua na kujitangaza mshindi akaweka na sherehe za kuapishwa bila aibu,huyu naye akaona isiwe tabu si kuapishwa tu,nayeye akaita watu wake akaweka sherehe za kuapishwa kuwa rais vilevile.jamaa aliyechakachua katangaza baraza la mawaziri na huyu nae mpinzani katangaza baraza lake la mawaziri.halafu wote wako jikoni kuandaa list ya mabalozi wao

kicheko zaidi huyu mshindi halisi katoa ofa ya kazi kwa rais aliyeshindwa kasema asikonde atampa kazi yeye na mawaziri wake.fuata habari hiyo HAPA

HAPO NDIO UTAJUA WAAFRIKA HATUPENDI KUCHEZEWA UGALI WETU UKITISHIWA KUMWAGIWA MAJI


No comments:

Post a Comment