Sunday 4 November 2012

BRIGITTE AIBUKA MSHINDI REDD'S MISS TANZANIA 2012


HATIMAYE kile kitendawili cha muda mrefu cha Nani ata twaa taji la Redds Miss Tanzania 2012, kimeteguliwa usiku wa Novemba 3, 2012, baada ya Mrembo kutoka Kitongoji cha Sinza na Kanda ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Brigitte Alfred kutwaa taji hilo.

Brigitte ambaye nyota yake katika mashindano hayo ya urembo nchini ilianza kung’aa tangu Kitongoji cha Sinza baada ya kutwaa taji la Sinza na Baade kutwaa Taji la Redds Miss Kinondoni amedhihirisha ukali wake baada ya kuwabwaga warembo wenzake 29 waliokuwa wakiwania taji hilo kutoka Kanda mbambali.

Mpinzani mkubwa wa Brigitte katika shindano hilo alikuwa ni Mrembo kutoka Kanda ya Ziwa ambaye nae alianza kuwika baada ya kutwaa taji la Redds Mkoa wa Mara na baade kutwaa taji la Kanda ya Ziwa, Eugene Fabian.

Enagene alifanikiwa kushika nafasi ya pili katika shindano hilo kubwa ambalo Brigitte ameondoka akiendesha gari aina ya NOAH na kitita cha Shilingi Milioni 8.

Nafasi ya tatu ilikwende kwa Malkia wa Kitongoji cha Kigamboni City na Miss Temeke 2012, Edda Sylvesta huku nafasi ya Nne ikichukuliwa na Mrembo wa Dar Indian Ocean na Kinondoni, Magdalena Roy na nafasi ya Tano ikienda Kanda ya Ziwa tena kwa Mkoa wa Mwanza, Happyness Daniel.
 Brigitte Alfred akipunga mkono kwa furaha mara baada ya kutangazwa kuwa ndie mshindi na kuwabwaga washiriki wenzake 29.
Brigitte Alfred (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Miss Tanzania 2011, Salha Izrael
Mshindi wa Taji la Redds Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred (katikati) akipunga mkono kwa furaha katika picha ya pamoja na mshindi wa Pili, Eugene Fabian (kushoto) na Mshindi wa Tatu, Edda Sylvester mara baada ya warembo hao kutangazwa kuwa washindi wa shindano hilo. Brigitte anatokea Kitongoji cha Sinza na Kanda ya Kinondoni wakati, Eugene anatoka Mkoa wa Mara na Kanda ya Ziwa huku Edda ni Miss Kigamboni na Kanda ya Temeke.//Picha zote na FATHER KIDEVU BLOG
Warembo waliofanikiwa kuingia hatu5 bora ya Redds Miss Tanzania 2012, kutoka kushoto ni Brigitte Alfred, Eugen Fabian, Happyness Daniel, Edda Sylvester na Magdalene Roy wakipozi kwa picha.

Washiriki wakicheza show ya ufunguzi wakati wa kuanza kwa shindano hilo.
Wageni mbalimbali na wadau wa tasnia ya Urembo nchini Tanzania wakifuatilia shindano hilo kwa umakini ndani ya Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa kundi la Ngoma za Asili la Wanne Stars likitoa burudani kwa wageni.
Balozi wa Tanga Beach Resort, Happyness Rweyemamu akijinadi jukwaani na vazi lake la ubunifu.
Mshiriki Flavian Maeda kutoka Kitongoji cha Kurasini na Kanda ya Temeke jijini Dar es Salaam akipozi jukwaani na vazi la ubunifu.
Fina Recatus akipita jukwaani na vazi la ubunifu. Fina ni Balozi wa Tanga Beach Resort 2012.
Naomi Jones nae akipita jukwaani na vazi la ubunifu
Mrembo wa Dar Indian Ocean na Kinondoni, Kudra Lupato nae alikatiza jukwaani na kunaswa na Camera ya Father Kidevu Blog.
 Brigitte akipozi na vazi lake la Ubunifu
 Msanii kutoka THT Rachel nae alipata fursa ya kuonesha kipaji chake na kudhihirisha wazi kuwa yeye ni Mrithi wa Ray C kwa sauti na kiuno Bila mfupa.

Japokuwa ni ufukweni lakini chini walivaa hivi, maana shindano la Dunia ndivyo inavyokuwa
 Warembo mbalimbali wa Redd's Miss Tanzania 2012 wakionekana Jukwaani katika vazi la ufukweni.
Warembo mbalimbali wa Redd's Miss Tanzania 2012 wakionekana Jukwaani katika vazi la ufukweni.
 Warembo mbalimbali wa Redd's Miss Tanzania 2012 wakionekana Jukwaani katika vazi la ufukweni.
 Warembo mbalimbali wa Redd's Miss Tanzania 2012 wakionekana Jukwaani katika vazi la ufukweni.
Mdau Kabula nae hakukosa na haopa akiwajuza waliobaki nyumbani kinachojiri. Siunajua tena mambo ya Tanesco baadhi ya mitaa na mikoa ilikuwa giza tu.
Waongoza Show nzima ya Redds Miss Tanzania 2012, Jocate Mwegelo 'Kidot' na Taji Liundi wakiwajibika.//
 

No comments:

Post a Comment