Thursday 22 November 2012

FM ACADEMIA NA BONGE LA PARTY KUADHIMISHA MIAKA 15, DESEMBA 14



KATIKA kuadhimisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, bendi ya  muziki wa dansi ya Fm Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ inatarajiwa kufanya onyesho la aina yake siku ya Desemba 14 kwenye ukumbi wa Msasani Club. 
Mratibu wa onyesho hilo, Nassib Mahinya alisema kwamba, usiku huo wa aina yake utaambatana na shamrashamra mbalimbali zilizoandaliwa ili kuwapa raha mashabiki watakaojitokeza. 
Alisema kupitia usiku huo ambao pia utawakutanisha wasanii wote waliopata kupitia bendi tangu kuanzishwa kwake, pia bendi hiyo itaopiga  nyimbo zake kuanzia zile zilizotoka  kwenye albamu yao ya kwanza hadi sasa. 
“Pia kutakuwa na tukio la kukata keki sambamba na kuwapongeza wale wote waliochangia kwa namna moja ama nyingine kuifikisha hapo ilipo bendi hiyo,”alisema 
Mahinya aliongeza kuwa katika kunogesha zaidi usiku huo wasanii na makundi mbalimbali wanatarajia kusindikiza wakiwemo kundi la Mapacha watatu pamoja na wasanii wa kundi la Mtanashati Entertauinment wakiwemo Dogo Janja, PNC na wengineo. 
Onyesho hilo limeandaliwa na Sinai Entertainment na kudhaminiwa na Mabibo Beer Wine & Spirit, Mama Mbaga Catering, Africa Media Group, Chonapi General Supplier, Benny Mlokozi Company , Big Solution, Mtanashati Entertainment, Eliado Point View, Arafa Salon, Friendship Restaurant na Masters Club.

No comments:

Post a Comment