Friday 9 November 2012

Ufisadi Wa Mabilioni Uswisi Watikisa Nchi






MJADALA mkali uliibuka bungeni jana baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) kuwalipua baadhi ya viongozi waandamizi wa Serikali akitaka wachunguzwe kwa makosa ya kuficha mabilioni ya fedha nje ya nchi.

 Zitto alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akiwasilisha hoja yake binafsi kuhusu kulitaka Bunge kuchunguza na kuielekeza Serikali kuchukua hatua dhidi ya raia wa Tanzania walioficha fedha na mali haramu nje ya nchi.

 Bila ya kuwataja kwa majina, mbunge huyo aliwataja watu hao kwa nyadhifa kuwa ni watu wote walioshika nyadhifa za uwaziri mkuu katika kipindi cha 2003 hadi 2010, walioshika nyadhifa za uwaziri wa nishati na madini katika kipindi hicho na waliokuwa makatibu wakuu Wizara ya Nishati na Madini. 

Inaendelea... 

www.kwanzajamii.com/?p=4231

No comments:

Post a Comment