Thursday 24 May 2012

MNYIKA ASHINDA KESI UBUNGO

Taarifa za uhakika ambazo zimetufikia ni kuwa, Mbunge wa jimbo la Ubungo mkoani Dar es salaam, John Mnyika, ameshinda kesi iliyokuwa imefunguliwa kupinga ushindi wake katika uchaguzi uliompatia ushindi yeye na chama chake (CHADEMA), katika jimbo hilo.

                     Taswira Mbali Mbali mara baada ya Mnyika kushinda Case

 Mbunge wa chadema John Mnyika akiwa amebebewa na wanachama wa chama hicho mara baada ya ushindi leo katikan mahakama kuu ya tanzania katika hukumu ya kesi ilofunguliwa na mpinzani wake Hawa Ng'humbi wa chama cha CCM kupinga matokeo ya uchaguzi.
 Wakereketwa wa vyima mbalimbali wakiwa wamefurika mahakama kuu ya tanzania leo kusikiliza hukumu ya john mnyika
 jeshi la polisi likiakikisha ulinzi unaimarika katika mahakama hiyo leo
 Wakereketwa wa vyima mbalimbali wakiwa wamefurika mahakama kuu ya tanzania leo kusikiliza hukumu ya john mnyika wakiwa wanashangilia nje ya mahakama kuu.
 Jeshi la polisi likiwa kwenye msafara kusindikiza maandamano ya chama hicho kuelekea katika njimbo la la john Mnyika mara baada ya ushindi huo
 kijana ambae akujulikana jina lake akiwa amebebwa baada ya kuanguka kwenye pikipiki
 John Mnyika akionyesha ishara ya ushindi akiwa na wapambe wake pepembeni
 hapa wakielekea jimboni kwake Ubungo

  hivi ndo vituko vya ushindi wa CHADEMA
 Wanafunzi wa shule ya msingi Dr Omari mansipaa ya kinondoni nao wakisherekea ushindi huo
 maandamano ya kusindikiza John Mnyika 
 waandishi wa habari wakiwa kwenye kupata habari walipowasili katika jimbo la John Mnyika
John mnyika akiutubia katika jimbo lake mara baada ya kuwasili 
Picha zote na Philemon Solomon wa Fullshangwe Blog

No comments:

Post a Comment