Saturday 26 May 2012

TAIFA STAR IMETOKA SARE 0-0 NA MALAWI

Mpira umekwisha kama wanavyoonekana katika picha wachezaji wa Taifa Stars wakitoka nje ya uwanja kwenda mapumziko, Si Taifa Stars wala Malawi ambayo imepata goli, hata hivyo wamalawi wameshambulia mara nyingi katika lango la Taifa Stars katika kipindi cha kwanza, lakini uimara wa mabeki pamoja na Golikipa Juma Kaseja umesaidia Wamalawi hao kutopata goli ,  Taifa Stars yenyewe imefanya mashambulizi ya hatari mawili tu! hata hivyo haikuwa bahati yao ambapo mpaka mwisho wa mchezo huo timu hizo zimetoka sare ya 0-0.

Timu ya Malawi iko safarini kuelekea nchini Uganda ambako itakipiga na timu ya Uganda Cranes.
Mpambano huo unafanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezaji wa timu ya taifa Taifa Stars Mbwana Samata ambaye anacheza mpira wa kulipwa katika timu ya TP Mazembe nchini DRC Congo akijaribu kumtoka beki wa malawi Foster Namwela wakati timu hizo zikimenyana kwenye uwanja wa Taifa jioni hii
 Wachezaji wa timu ya taifa Taifa Stars wakiingia uwanjani jioni hii kwa ajili ya kupasha mwili kabla ya mpambano wake wa kirafiki na timu ya taifa ya Malawi The Flames
 Wachezaji wa timu ya Malawi wakipasha mwili kabla ya kuingia uwanjani kukwaana na Taifa Stars jioni hii kwenye uwanja wa Taifa.
Wachezaji wa akiba wa timu ya Taifa Stars wakijifua kabla ya mpambano huo jioni hii.

No comments:

Post a Comment