Friday 18 May 2012

PATRICK MAFISANGO AAGWA NA WENGI DAR

Mwili wa marehemu Partrick Mafisango ukiwasili viwanja vya TCC Chang'ombe mapema leo Baadhi ya wachezaji wa timu ya Taifa, Juma Nyoso (kushoto) na John Boko, wakiwa wamebeba  jeneza lililokuwa na mwili wa Mafisango kuupeleka sehemu iliyopangwa.

Jeneza likiwa na kombe la ubigwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania lililotwaliwa na Simba mwaka huu.

 Mdogo wa marehemu akisaidiwa baada ya kuishiwa nguvu
Kutoka kushoto ni msemaji wa Simba Ezekiel Kamwaga, Kocha wa Simba Milovan Cirkovic na goalkeeper wa Simba Juma Kaseja wakilia kwa uchungu 
 Baadhi ya waombolezaji msibani hapo
---
Mwili wa Marehemu kwa sasa uko njiani kuelekea nyumbani kwao, Kinshasa Congo ambako ndipo atakapo zikwa. 
Blog hii inapenda kutoa pole kwa Club ya Simba, wapenzi wote wa michezo na familia ya marehemu.

Picha zote kwa hisani ya Globalpublishers

No comments:

Post a Comment