Monday 24 January 2011

Uwanja wa ndege mjini Moscow walipuliwa

Uwanja wa ndege wa Domodedovo wa Moscow umetikisika baada ya kutokea mlipuko wa bomu ambapo msemaji wa uwanja huo alisema watu 35 wamefariki dunia.
Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa- 20 wakiwa katika hali mbaya sana kutokana na mlipuko huo, ambapo ripoti zinasema shambulio hilo limefanywa na mtu aliyejitoa mhanga.
Mchunguzi mkuu wa Urusi alisema magaidi ndio wamehusika na shambulio hilo.
Uwanja huo, ambao una shughuli nyingi katika mji mkuu wa Urusi, upo kilomita 40 kusini-mashariki mwa mji huo.
Urusi
 
soma  zaidi bofya HAPA

No comments:

Post a Comment