Tuesday 6 December 2011

tujikumbushe recipe"PILAU YA KUKU WA KIENYEJI"

lunch time leo"PILAU LA KUKU WA KIENYEJI"



kuku mzima wa kienyeji"ama höns"akiwa tayari kasafishwa na kukatwakatwa

unanza kwa kutia huyo kuku ndani ya sufuria
unakaanga kwa kuchanganya na garlic, ginger,garam masala mpaka anaanza kuwa brown,
hakikisha asikauke sana.kisha unaweka maji ya kutosha.
halafu unafunika achemke mpaka alainike,muda 1 hr ama zaidi huku ukiongeza maji.
baada ya kuku kuiva na kulainika,unaipua na kuweka pembeni.
kisha unaweka sufuria ingine motoni,weka mafuta kiasi,kitunguu,viazi ulaya,
unakaanga kwa pamoja mpaka vitunguu vinaanza kuwa brown
,kisha unaweka garlic paste,hiliki nzima kiasi,cinnamon nzima kiasi na cummin seed kiasi.
unakaanga huo mchanganyiko mpaka vitunguu vinakuwa brown kabisa lakini visiungue
.kisha unaweka vipande vya kuku na pilau masala kiasi kidogo tu maana viungo vingi ulivyotumia vimo katika pilau masala.
unakaanga pamoja.kisha unaweka mchele na ile supu ya kuku iliyobaki,
kisha unaweka chumvi unakoroga pamoja vyoote mpaka vichanganyike,unafunika nakusubiri vichemke pamoja kwa dk km 10,
kisha unapunguza moto unaweka chini kabisa no 1,mlio sweden mnaelewa lakini kama unatumia jiko la makaa pia bongo unaelewa namaanisha nini.
unaacha katika moto huo mdogo kwa dk 45 ama saa nzima,mda huo kama una kabia ama kawine shushia kabisa,au hata ukitaka kwenda cheza draft poa,ama hata ukitaka kwenda ku-over-haul tumbo liwe tupu pia wewe tu.

baada ya muda huo pilau lako sasa liko ready kwa kuliwa,usisahau kutengeneza kachumbari yako mapema,recipe kachumbari wengi mnaijua au ni nyanya,kitunguu ndimu piripiri unakata slice slice vyembamba kisha unachanganya na ndimu na chumvi.

pilau lako likiwa tayari kusulubiwa na kachumbari kwa pembeni

hapa unatafuta mkeka au kapeti unakaa,maana si stahili kulia mezani na umma wala kijiko hutapata utamu wake
bila kusahau kilaji baada ya msosi na si kabla,enjoy

baada ya kukosa mwaliko nimeona nijumuike na wadau wangu idd hii pilau tunalilia hapa hapa bloguni.karibuni

MAHITAJI
*kuku mzima
*mchele 1/2 kg
*olive oil 1 spoon
*garam masala 1tea spoon
*garlic paste 1 spoon
*ginger paste 1 tea spoon
*cinammon whole 1
*cummin seed 1 tea spoon
*hiliki nzima 1 tea spoon
MAHITAJI KACHUMBARI
*nyanya 2
*kitunguu kikubwa chekundu 1
*ndimu 1
*pilipili (ukipenda)1

3 comments:

  1. Ahsante kaka na nawatakieni mlo mwema ila hapo naona kama inakosekana SAFARI ...LOL

    ReplyDelete
  2. ha ha haa,da yasinta tuko pamoja,safari imekosekana ila duh nimeijaribu hiyo mi imenishinda kabsaa.naamka mgonjwa siku nikinywa

    ReplyDelete
  3. Mmmmhh? pole sana basi siku nyingine jaribu KILI au Serengeti...

    ReplyDelete