Monday 14 February 2011

ABAMBWA LIVE AKIMCHOMOA MTU MIMBA



Dokta Said wa zahanati moja iliyopo Magomeni, Dar es Salaam, amenaswa akimtoa mimba mwanamuziki wa kundi moja la Muziki wa Taarab, Mwanaidi Madani (kama inavyoonekana pichani).

The Biggest IQ, Ijumaa Wikienda liliendesha uchunguzi wa kisayansi wiki iliyopita na kumnasa Dk. Said akimshughulikia Mwanaidi katika kukiua kitoto kisicho na hatia tumboni.

Wakati gazeti hili linapenyeza kamera zake kwenye chumba cha ‘unyofoaji mimba’, dokta huyo alikuwa tayari ameshamdunga Mwanaidi sindano ya nusu kaputi na kuondokewa na fahamu.

UCHUNGUZI WA KISAYANSI
Ijumaa Wikienda lilipata taarifa mapema kuwa Mwanaidi alikuwa akielekea kwa Dk. Said kutoa mimba, baada ya mipango ya awali kuwa imeshafanyika.
Wakati dokta huyo akianza kumshughulikia Mwanaidi, alipigwa na bumbawazi mara alipojikuta akiwekwa chini ya ulinzi na maafande wa Jeshi la Polisi.

Katika kutapatapa, alitaka kuingia chini ya kitanda lakini polisi mmoja alimdaka na kumuuliza alichokuwa anafanya.

Baadaye polisi walimtuliza dokta huyo na kumtaka aendelee kutekeleza kile alichokuwa anamfanyia mgonjwa wake ili asimsababishie matatizo zaidi kiafya.

Kutokana na agizo hilo, dokta huyo aliendelea kukamilisha shughuli yake ya kukichomoa kichanga tumboni kwa Mwanaidi, huku kamera za Ijumaa Wikienda zikiendelea kufanya kazi yake.

DK. SAID NA MAHAKAMA
Ijumaa Wikienda lilifuatilia ‘mechi’ kati ya polisi wa Kituo cha Magomeni, Usalama na dokta huyo lakini mpaka leo hajafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Gazeti hili lina uthibitisho pia kwamba hata Mwanaidi hajafikishwa kwa pilato kujibu tuhuma za kunyofoa mimba na kuua kitoto kisicho na hatia.

DK. SAID KATIKA KIBANO
Ijumaa iliyopita, gazeti hili lilimhoji Dk. Said sababu ya kutofikishwa mahakamani mpaka leo wakati ushahidi upo wazi kwamba alinaswa akimtoa mimba Mwanaidi.
Hata hivyo wakati akijibu, dokta huyo alikuwa akijichanganya na zaidi akawa anasisitiza aonane na mwandishi wetu ili aweze kumsaidia.

“Aaa... la, naomba unisaidie tafadhali, wewe ni mwanaume. Tuonane unisaidie ili tumalize hili tatizo,” alisema Dk. Said huku akirekodiwa sauti na mitambo maalumu.

MWANAIDI NAYE
Mwanamuziki huyo alipozungumza na gazeti hili Ijumaa iliyopita alijibu: “Mimi nilikwenda kwa dokta kusafisha tumbo, lakini polisi walinikamata wakadai nimetoa mimba.”
live from global publishers.
.

No comments:

Post a Comment