Tuesday 5 July 2011

USINYWE RED BULL -- NI HATARI KWA MAISHA YAKO – HASA VIJANA

RED BULL Huuzwa katika maduka makubwa (Supermarkets) na madogo (Retail Shops) katika nchi ya Tanzania na watu wazima na watoto wetu wengi wana mazoea ya kunywa kinywaji hiki ambacho kinaweza kusababisha kifo!
Kemikali zinazopatikana katika kinywaji cha RED BULL zilitengenezwa maalum katika maabara za kijeshi za Marekani kwa ajili ya kutuliza mzuka wa maaskari wao wakati wakitekeleza mauaji ya kikatili sana dhidi ya wananchi wa Vietnam miaka ya sitini na sabini. Kemikali hizo zilitumika pia kama dawa ya kuwazindua watu waliozirai (“stress coma”).
Hazikukusudiwa kutumiwa kama kinywaji au kilevi cha kawaida!
Duniani kinywaji hiki (RED BULL) huuzwa kama kitu cha kuleta msisimko (Energizer Drink) na matangazo yake yanataja sifa zake kama ifuatavyo.

“Ni kinywaji kinachompa mtu nguvu ya kustahimili na umakini. Humpa mtu kasi ya vitendo” ... na kadhalika.
RED BULL imesambaa katika nchi 100 kwa mpigo (nchi masikini!).. Na matangazo yake kuwalenga vijana na watoto, hasa wanamichezo. Hawa ni rahisi kushabikia kinywaji hiki kibaya na kudhurika kiafya baadaye.
Katika hali yake ya matumizi ya sasa kinywaji hiki kiligunduliwa na Mjerumani Dietrich Mateschitz ambaye alikikuta huko Hong Kong kikiwa ni
mojawapo ya madawa yaliyotumika katika kutengeneza dawa ya mswaki wa meno. Dawa hiyo ilitengenezwa kwa kemikali ambazo zina kafeni na taurini
(“caffeine and “taurine). Mjerumani huyo aliona vijana wajinga wa huko wakishabikia unywaji wake, akaona mwanya wa kufanya biashara na akafanikiwa kukileta Ulaya.

ATHARI ZA KUNYWA RED BULL
Kinywaji kinachotengenezwa na kusambazwa leo hivi kina kemikali mbaya iitwayo “Glucuronolactone”, kemikali hatari ambayo ilitengenezwa na idara ya jeshi la Marekani wakati wa vita na Vietnam kwa ajili ya kutuliza mvurugiko wa mawazo wa maaskari wake uliotokana na mauaji ya kinyama waliyokuwa wanafanya huko Vietnam.
Kwa sababu ya madhara makubwa ya kinywaji hiki nchi za UFARANSA na DENMARK zimepiga marufuku kinywaji hiki na kibatiza jina la “MKOROGO WA UMAUTI”. Katika nchi hizi, utafiti uligundua kuwa maaskari wa Marekani waliotumia kinywaji chenye kemikali ya “GLUCURONOLACTONE” waliishia kupata madhara ya maumivu makali ya kichwa, uvimbe wa ubongo na hata ugonjwa wa ini (Migraines, Cerebral tumours and liver diseases). Ni kwa sababu hiyo Wamarekani waliacha kuwapa maaskari wao hicho kinywaji katika miaka ya sitini na sabini.

Jambo la kushangaza ni kuwa lebo ya RED BULL inaonyesha wazi kuwa kinwaji hiki kimetengenezwa kwa kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE”! Ni kwa sababu hiyo serikali za DENMARK na UFARANSA nazo zikapiga marufuku unywaji wa RED BULL.
Pamoja na wauzaji wa RED BULL kuweka bayana kuwa ndani mwake mna hiyo kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE” lebo ya RED BULL haielezi madhara makubwa yanayoletwa na kemikali hiyo. Madhara ambayo hayakuwekwa bayana kwa mnywaji ni kama yafuatayo:
1. Ni hatari kwa mtu ambaye hafanyi kazi au mazoezi mazito sana kukitumia, kwani kina tabia ya kuongeza msukumo wa damu na kasi ya mapigo ya moyo kiasi kwamba mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa moyo.

2. Mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa damu kuvuja ubongoni kwani RED BULL ina kemikali zinazoifanya damu iwe nyembaba ili moyo upate kusukuma damu nyingi bila kutumia nguvu nyingi.
3. Ni hatari kuchanganya RED BULL na pombe ya aina yoyote, kwani mchanganyiko wake huwa ni sumu (“Deadly Bomb”) inayoathiri misuli ya ini la mtumiaji na kuiacha katika hali ambayo haitapona kamwe.
4. RED BULL Ina vitamini B12 kwa wingi, vitamini ambayo hutumiwa kama dawa ya kuwazindua wagonjwa mahututi. Matumizi ya vitamini hii katika watu wazima ina athari za kuleta shinikizo la damu na humfanya mtu ajisikie
kama mlevi.

5. Unywaji wa RED BULL mara kwa mara huvuruga mfumo ya neva za fahamu na husababisha maradhi mithili ya mfadhaiko wa akili usioponyeka.
HITIMISHO:
RED BULL ni kinywaji HATARI SANA ambacho hapana budi kipigwe marufuku katika nchi zote zinazoendelea kwani ni dhahiri kimetengenezwa na kusambazwa ili kuathiri afya za wananchi wasiojiweza wa nchi hizi masikini. Kwa kuwa wengi katika nchi hizi hutumia pombe za kila aina ni wazi kuwa kinywaji hiki kinalenga kuwamaliza watu wetu – kana kwamba
ukimwi uliobuniwa na hao wabaya wetu hautoshi!

NI VYEMA TUKAWALINDA
WATOTO NA VIJANA WETU LA SIVYO HATUNA WARITHI!



IMEWEKWA KAMA ILIVYOLETWA

2 comments:

  1. Mhhhhhhh!!!sasa nchi zote hizi hazioni hayo mazala na kupiga marufuku?kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyeweeeeeeeeeee.Ahsante kwa Ujumbe.

    ReplyDelete
  2. ndio hivyo mama,kama kudhurika tushadhurika maana tushatafuna hizo red bull za kutosha.hii kampeni inabidi waipige huko mitaani bongo maana jamaa wanakula hizi red bull kama wamelogwa.mtu kule anaona akipiga red bull ndo advertise kuliko kunywa fanta.

    ReplyDelete