Wednesday 10 November 2010

MSHAURINI HUYU JAMAA


Hii ni story ya kweli. Jamani naomba ushauri kwa sababu mwenzenu nimechanganyikiwa. Nina mchumba wangu ambaye nimefahamiana takribani miaka miwil sasa. Miezi sita ilopita niliamua kutangaza nia ya kweli na kumfisha engagement ring tena mbele ya wanafamilia wote. Tlikua tunapendana sana. Katika harakati za kujiendeleza kimasomo, nlipata nafasi kwenda chuo kwa ajili kuchukua degree ya pili (masters). Na mchumba wangu naye akawa amepata chuo mkoa tofauti na wa kwangu. zengwe limeanza tukiwa likizo wote nyumbani. my wife to be amekuja nyumbani kwangu mida ya saa kumi na mja jion kama kaida yake alikua amependeza sana. Kapika msosi tukala. Yeye amepanga nyumba yake mbali na nyumbani kwao. Ghafla akaniambia, "honey unajua mamangu amekuja kunisalimia kwa maana hio ntaondoka muda sio mrefu kwenda kumuandalia chakula" Nkamwambia, hamna noma baby, nkamsindikiza kisha nkarudi home kwangu kuangalia TV. Tuna mazoae ya kupigianapigiana simu. Siku hio ikawa tofauti kwani hata mawasiliano hayakua smooth as usual, nkamuuliza swiry what are u exactly doin? kaniambia "whatching TV HONEY" Nkamuuliza which channel? Akaniambia "TBC). Kwa vile nlikua naangalia the same channel nkamuuliza anaaangalia nini. Hakujibu mara kigugumizi. Siku hio sikupata hata tone la usingizi. Ilipofika saa kumi na nusu alfajiri, nkachukua gari kwenda nyumbani kwake. Nlipofika getini kwake nkampigia simu kua niko nje aje anifungulie kuna issue muhimu sana nataka nimwambie. Akagoma kua hafungui kwa vile mamake yupo. Nkampigia mdogo wake aje anifungulie naye akakataa. Kwa vile mama mkwe mtarajiwa ananifahamu na ananiamini nkajua yeye sio tatizo la kutofunguliwa. Ok nkamwita atoke nje bila kunifungulia akagoma. Hapo ilikua inakaribia saa kumi na moja unusu. Nikamwambia kua sitoki getin kwake hadi asubuhi ili niweze kuonana naye. Baadae akazima simu yake. Ilipofika saa mbili akawa amewasha simu yake, nkamwambia bado niko getini namsubiria. Alivyoskia niko serious, akaniambia ukweli kua hayuko nyumban na hakulaa nyumbani kwake. Ni kweli hakulala kwake na sio kweli kua mamake alikua amemtembelea. I proved that beyond doubt. Nkaondoka zangu nyumbani nikiwa nimechanganyikiwa ile mbaya. Jioni yake akaja kwangu for reconciliation. Siku hio akanidanganya, nikamfukuza haraka kutoka kwangu na makofi na buti juu. The next day she came and told me nothing but the truth kua alikua na alilala kwa mshikaji (gentleman) ambaye wanafanya kazi pamoja (I know this guy). She apologized. Nkajifanya nmemsamehe ila kichwani nlikua nmeshamdelete. Badae akarudi chuoni, baada ya wiki tatu hivi akaniambia kua ana uja uzito wangu. Nlichomwambia ni kua siutambui huo uja uzito labda aende kwa jamaa yake(mwizi) ndo kamtia hio mimba. Honestly, am heartbroken na simtaki na wala simpendi tena huyu dada. She still instists that am the father hadi anakwenda nyumban kwetu kuambia kua she is expecting my baby. Sijamwambia ndugu yangu yeyote about this saga.

Je niwambie ndugu zangu na marafiki zangu wa karibu full story juu ya huyu mdada? nyumban kwetu anakubalika sana. Ntashukuru sana kwa ushauri wenu

No comments:

Post a Comment