Thursday 21 April 2011

KINSHASA MOTOO MOTOO YA PEPE KALLE





sikiliza hizo songi mpaka mwisho kisha uniambie enzi hizo ulikua wapi 90s,kumbukumbu yangu ndogo enzi hizo ulikua ukinikuta huko mitaa ya singapore ya bongo nasoma,tulikua na madisko yetu kule majina kama isuna discotheque na salma disko.
ukisoma boarding unakuta umepewa kajisenti kakutumia shule kwa muhula lakini umekachoma kiberiti kabla hata hujafika shule kameisha na kurudi tena home kuchukua somo halitaeleweka kwanza nauli utapata wapi.
basi tukabuni kamradi ka kucheza show na jamaa yangu nabeel(yeye jamaa mdingi wake alikua mshua halafu alikua anakuja skul na redio kaseti)hivyo ikabidi tuanze zoezi shuleni.
na kweli baada ya muda zoezi likakubali tukaanza kuzirudi hizi bolingo si mchezo,ulikua ukitukuta kwenye hizo club mbili nilizotaja utachoka mwenyewe,nabeel akiitwa bileku mpasi(na alikua anacheza kweli utasema unamuona bileku hapo) na mimi nikiigiza loketo(nyimbo kama washiwa na extra ball) aah tulikua tunapiga hela yaani acha tu,kisha na ka-umaarufu uchwara enzi hizo wakija kina black moses,super ngedere na kina flora tingisha"lango la jiji" walikua wanatukuta tumetawala huko na tunakua wenyeji wao.ujana raha bana

PASAKA NJEMA WADAU

No comments:

Post a Comment