Friday 29 April 2011

WASOMALI 82 WAKAMATWA MSITUNI BONGO


WATU wapatao 82 raia wa Somalia wamekamatwa jana mchana kwenye msitu wa moja ya vijiji vya Wilaya ya Gairo mkoani hapa wakiwa safarini kuelekea jijini Dar es salaam kutafuta maisha.

Akizungumza na mtandao huu kwenye kituo kikuu cha  polisi mkoani hapa, askari mmoja wa kikosi cha kutuliza ghasia wilayani Gairo maarufu kwa jina la 'voda fasta'alisema Wasomali hao walikamatwa baada ya polisi kupokea taarifa kutoka kwa raia wema.

"Tumepokea taarifa kutoka kwa raia wema wakitujuza kuwa kuna kundi la wasomali wanakata mbuga katika misitu ya Vijiji vya Gairo hivyo baada ya kuwafuatilia tumewakamata na kuwaleta hapa mkoani," alisema afande huyo aliyekataa kutaja jina lake kwa kuwa sio msemaji mkuu wa jeshi la polisi.

Mwandishi wetu aliwashuhudia Wasomali hao wakishushwa kwenye roli huku wakiwa na matope hali inayoonesha kuwa huenda wana muda mrefu hawajaoga kutokana na kutembea kwa muda mrefu

source:GPL

duh wapeni mapepa ya ukimbizi tu hawa jamaa yaonekana wamechoka mbaya


3 comments:

  1. Kumbe bongo kuzuri. Watu wanakuja kwa mguu!!!!!!!

    ReplyDelete
  2. jamani maisha si mzaha now days.haya wasomali wanataka sheria hata ya kibongo jamani!!!

    ReplyDelete
  3. Watanzania lazma kujivunia AMANI inavyo dumu nchi yetu,sio tu Wasomalia hata Wanigeria,Wakongomani,Wahindi wanataka sheria ya Kibongo.

    ReplyDelete