Monday 24 September 2012

MAJIBU YA LADY JAY DEE KWA FANS WAKE FACEBOOK

 

Habari,

Kama nilivyoahidi kujibu maswali ya walio andika facebook inbox. Ambayo mengi yao yana fanana, ila kwa yale ambayo yatakuwa hayajajibiwa ni kutokana na kuwa sikupata majibu yake. Au sina majibu yake kabisa.

1. WANAOOMBA KUFANYA NYIMBO ZA KUSHIRIKIANA, COLLABO/FEAT
Jibu: Ningependa kufanya nyimbo nyingi kwa kushirikiana na wasanii tofauti, lakini kutokana na ukweli halisi ni kwamba Duniani popote. Haiwezekani kwa msanii yoyote kufanya Collabo na kila msanii anaeomba kufanya nae.

Hii ni kutokana na kwamba hata wasikilizaji watachoka kusikia kila siku sauti ya mtu huyo huyo mmoja  kwenye kila wimbo. Pia wakati mwingine inahitajika kuupa muda katikati ya Collabo na Collabo
Na ni vema kuwa niwe nimeshawahi hata kumsikia mtu ambae anaomba nifanye nae wimbo.
Mengi mengine yanakuwa nje ya uwezo wangu.

2. WANAOTAKA KUWA MEMBER WA LA FAMILLE
Jibu: Vigezo vya kuwa member ni kwa wale ambao tumekuwa tukishirikiana nao kwa mambo mbali mbali katika mitandao, tukazoeana baadae tukakutana uso kwa uso na kujenga undungu.

Kwasasa tunaiboresha Familia iliopo, watu wazoeane na kufahamiana kwa ukaribu kabla ya kuongeza members wengine wapya.

Nilifikiria kuunda kundi la pili, litakaloitwa LA FAMILLE 2
Ili lile la kwanza libakie kuwa vile vile, kwakuwa wamekwisha zoeana sana
Na la pili waunde mazoea pia uwe ni umoja mwingine.

3. WANAOOMBA KUWA NDUGU ZANGU WA HIARI -DADA, KAKA, WADOGO
Jibu: Mtu yoyote ambae anapenda kuwa ndugu yangu kwa hiari yake anakaribishwa. Tatizo linakuja pale anapotaka tuwe tuna chat muda wote
Ku chat haitawezekana kutokana na muda kuwa hautoshi.
Ila kunipenda na kuniandikia ni vizuri, nikipata muda nitakuwa najibu, Mkitaka kunitembelea, karibuni Nyumbani Lounge....Sina maneno....Karibuni sana

4. NAFASI ZA KAZI
Jibu: Kuhusiana na wanaohitaji nafasi za kazi
Mnaweza kuandika e-mail: nyumbanilounge@gmail.com
Huko mtapata majibu kutoka kwa wahusika.

5. MISAADA
Jibu: Kwa wale wanaoniomba misaada ya pesa, za ada, chakula na mahitaji mengine.
Ukweli ni kwamba uwezo wangu sio mkubwa sana wa kuweza kumsaidia kila mtu. Japo ningependa kusaidia, na huwa nasaidia pale ninapoweza.
Bahati mbaya maombi yamekuwa mengi kuliko uwezo wangu.

Misaada ya kimuziki naweza kutoa ushauri, ila sina uwezo wa kumlipia Studio kila msanii mchanga anaeniomba.
Ila mnaweza kwenda kwa wenye Studio zao wakawasaidia kuwarekodi bure, endapo watavutiwa na kazi zenu ila hiyo itakuwa ni kazi kwenu kuwashawishi kuwa mna vipaji na mnastahili kusaidiwa bure bila malipo yoyote

6. CD ZINAPOPATIKANA
Jibu: Dar es salaam zinapatikana SHEAR ILLUSIONS -   Mlimani City na
         NYUMBANI LOUNGE
         Au kwa walioko mbali piga simu +255 767 884 007/
        +255 784 884 007

7. VIDEO MPYA
Jibu: Itatoka baada ya wiki moja

8. PROJECT NYINGINE ZINAZOKUJA
Jibu: Kwa sasa kuna project iko njiani na itaanza kuonekana mnamo mwezi wa October katikati
Nitawafahamisha pindi kila kitu kitakapokuwa tayari

9. BEI NA BOOKINGS ZA LADY JAYDEE & MACHOZI BAND
Jibu: Wasiliana na Gardner G Habash
          +255 767 884 007/ +255 784 884 007
           E-mail: nyumbanilounge@gmail.com
           Au fika Nyumbani Lounge kwa maonano ya uso kwa uso


Asanteni kwa kuniandikia, natumaini nimejitahidi kujibu kama mlivyotarajia. Nasikitika kwa ubinaadamu wangu pengine kuna maswali sikuweza kuyajibu, ila uwezo wangu wa kujibu umefikia hapo kwa leo

Kwa mazungumzo ya hapa na pale, na news zozote kunihusu.
Unaweza ku like page yangu www.facebook.com/ladyjaydee

Au nifuate twitter.com kwa jina la JideJayDee

Au niandikie e-mail: judyjaydee@yahoo.com kuhusiana na maswala ya kimuziki tu lakini sio bookings, wala mambo binafsi.

With Love
JIDE

No comments:

Post a Comment