Saturday 15 September 2012

SERENGETI FIESTA DODOMA ILIVYOFANA

Baadhi ya mashabiki wakishangweka vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri,Dodoma.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,mahiri katika miondoko ya miduara,IT akimrusha kimduara duara shabiki wake jukwaani usiku huu,huku shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala kutoka kwa watazamaji.…
Baadhi ya mashabiki wakishangweka vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri,Dodoma.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,mahiri katika miondoko ya miduara,IT akimrusha kimduara duara shabiki wake jukwaani usiku huu,huku shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala kutoka kwa watazamaji.
Wasanii mahiri wa filamu hapa nchini nao walikuwepo kuliunga mkono tamasha la Fiesta usiku huu ndani ya Dodoma,kutoka kulia ni Jacob Steven a.k.a JB,Wema Sepetu pamoja Aunt Ezekiel.
Ray Kigosi akilicheza sebene jukwaani.
Ray akimtambulisha Wema Sepetu kwa mashabiki.
Ray akiwaaga mashabiki wake mara baada ya kuwavunja mbavu mara baada ya kumaliza kulicheza sebene lake jukwaani.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Mh.Dr Rehema Nchimbi akisoma jina la mshindi wa gari aina ya Vitz inayotolewa na kampuni ya Push Mobile,ikiwa ni sehemu ya mchakato wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,pichani kati ni Meneja masoko wa kampuni ya Push Mobile,Rodney Lugambo,Muwakili shi wa michezo ya bahati nasibu ya Taifa,Bwa.Humudi pamoja na Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini,Mh Lephy Gembe. 
Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini,Mh Lephy Gembe akiwasalimia wakazi wa Dodoma waliojitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,kwenye uwanjawa jamuhuri.
Pichani juu na chini Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Linah kutoka THT akitumbuiza jukwaani usiku huu wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea usiku 
Pichani juu na chini ni msanii anaetamba katika miondoko ya R&B hapa bongo,aitwaye Ben Paul akiwarusha wakazi wa mji wa Dodoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta linaleondelea usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri.
Msanii wa bongofleva aitwaye Shetta akiwaimbisha washabiki wake usiku huu.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoco akiwaimbisha washabiki wake kibao waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalofanyika usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Dayna akijitokeza kwa mbwembwe jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linaloendelea hivi sasa kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma,ambapo wakazi wake wamejitokeza kwa wingi kuwashuhudia wasanii mbalimbali wanaotumbuiza kwenye jukwaa hilo.
Wakazi wa mji wa Dodoma wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,ndani ya uwanja wa jamhuri mjini Dodoma.
mmoja wa wasanii chipukizi katika anga ya muziki wa kizazi kipya,ambaye pia aliibuliwa na shindano la Serengeti Supa Nyota kutoka jijini Mwanza,aitwaye Young Killer akikamua jukwaani mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Dodoma usiku huu.
Wasanii kutoka THT wakitumbuiza jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Anaitwa Recho kwa jina la kisanii kutoka nyumba ya Vipati THT,akiimba jukwaani kwa madaha kabisa,huku umati wa watu (haupo pichani) ukishangilia kwa nguvu.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya akiwa amebebwa juu  mara baada ya kujitokeza jukwaani na wasanii waliopa  mtafu kutoka THT.
Kwa hakika wakazi wa mji wa Dodoma wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri,ambako ndiko tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea hivi,shangwe tuu.

No comments:

Post a Comment