Friday 7 September 2012

Ombi la Rais Obama kwa wamarekani



Rais Barrack Obama


Rais wa Marekani Barack Obama, amewaomba wamarekani kumpa fursa nyingine kuiongoza nchi hiyo.
Ombi lake amelitoa katika kilele cha kongamano la chama cha Democratic mjini North Carolina.
Taarifa zinazohusiana
Marekani
Akijiwasilisha kama mgombea wa urais mwenye kuleta matumaini kwa wamarekani, Rais Obama alisema kuwa uchaguzi utakaofanyika mwezi Novemba, utatoa fursa kwa wapiga kura kuchagua kati ya maono mawili tofauti kuhusu hatma ya Marekani.
Aliwataka Wamarekani kuwa wavumilivu akisema kuwa matatizo yanayokabili Marekani yamekuwa yakiongezeka kwa miaka mingi na kuwa itachukua muda kuweza kuyatatua.
Lakini aliongeza kuwa ikiwa watamchagua tena, ataweza kubuni nafasi mpya za kazi, kupunguza madeni na kuimarisha uchumi wa Marekani.
Rais Obama alisema anajiona kama kiongozi aliyekuwa amewekwa kwa mizani kujaribiwa uongozi wake na kuwa amefaulu. Alisema mpinzani wake wa Republican, Mitt Romney, hayuko tayari kwa mashauriano ya kidiplomasia.
Alitofautisha malengo yake na yale ya chama pinzani na kurejelea kauli mbiu yake ya mwaka 2008 , kuwataka watu kuwa na matumaini.
"sikuwahi kusema kuwa safari hii itakuwa rahisi na sitatoa ahadi hiyo hii leo'' Obama aliambia kongamano la wajumbe wa Democrat.
Mitt Romney wa chama cha Republican atapambana na Rais Obama kuwania urais huku kura za maoni zikionyesha wawili hao wakikaribiana.

bbc swahili

No comments:

Post a Comment