Wednesday 11 July 2012

Umoja wa Mataifa waapa kulinda Goma



Majeshi ya Umoja wa Mataifa yanaelekea Goma
Jeshi la kulinda usalama la Umoja wa Mataifa linapelekwa katika mji wa Goma ili kuulinda.
Balozi wa Umoja huo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amesema watahakikisha kuwa mji huo hautekwi na waasi wa M23.

Kwa wakati huu kuna taarifa kwamba waasi hao wa M23 wanaukaribia mji huo uliyo mashariki mwa Congo.
Balozi huyo ,Roger Meece amesema jeshi hilo pia litawalinda raia kutokana na waasi hao.
Wakati huo huo , vyanzo vya habari vimeiambia BBC kuwa jeshi la Congo limekomboa miji miwili ambayo hivi karibuni ilikuwa imetekwa na waasi.
Lakini waasi hao wa M23 wamesema kuwa hawana haja ya kuuteka mji wa Goma bali lengo lao kubwa ni kujadiliana na serikali.
Serikali ya Joseph Kabila na Umoja wa Mataifa imekuwa ikidai kuwa Rwanda inawasaidia waasi wa Congo. Hata hivyo Serikali ya Paul Kagema imekanusha madai hayo.
BBC imefahamishwa kwamba majeshi ya Congo yameonekana yakiingia mji muhimu wa Rutshuru ulio kilomita 70 kaskazini mwa Goma.
Nao mji wa Kiwanja, ambao uko kilomita 20 kaskazini na ambao pia ulikuwa umetekwa na waasi wa M23 nao pia umekombolewa.
Waasi hao ambao walianza vita mwezi wa Aprili waliamua kujiita M23 kufuatia mkataba waliotia saini tarehe 23 Machi . Hata hivyo mkataba wenyewe uliporomoka.
Siku ya Jumanne kiongozi wa waasi hao aliambia BBC kwamba watajificha katika maeneo ya milima hadi serikali ikubali kujadikiana nao . Kiongiozi huo alisisitiza kwamba hawana haja ya kuteka maeneo zaidi ya Congo.
M23 linaungwa mkono na Jenerali mtoro Bosco Ntaganda, ambae anatakikana na mahakama ya uhalifu wa kimataifa -ICC.
Jenerali Ntaganda ni M'tutsi sawa na wakuu wengi wa serikali ya Rais Kagame wa Rwanda.

bbcswahili

No comments:

Post a Comment