Saturday 13 October 2012

KAMANDA WA POLISI MWANZA AUWAWA NA MAJAMBAZI



 Marehemu Kamanda Barlow

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishna Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Barlow ameuawa usiku wa kuamkia leo katika tukio linalohusishwa na ujambazi.
Taarifa kutoka Mwanza ambazo zimethibitishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini zinasema kuwa Kamanda Barlow aliuawa baada ya kumrudisha dada yake kutoka katika kikao cha harusi ya ndugu yao huko Kitangili.
Hata hivyo, taarifa hizo bado hazijaweza kuchunguzwa na vyombo vya habari.


CHANZO:FIKRAPEVU

No comments:

Post a Comment