Friday 19 October 2012

UNDP Yaipongeza Tanzania Kwa Jitihada Za Maendeleo


 
Mwandishi wa Habari wa Radio France International (RFI Kiswahili) Bw. Ali Bilali akifanya mahojiano na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot (kushoto) ikiwa ni wiki ya maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa. 
Na Mwandishi Wetu
Umoja wa Mataifa umeanza kuadhimisha wiki mahsusi kwa ajili ya Umoja huo kwa kufanya shughuli mbalimbali ambapo nchini Tanzania taasisi za Umoja wa Mataifa, Serikali ya Tanzania na mashirika ya kiraia wanakutana kuzungumzia maswala mbalimbali yahusuyo maendeleo, utawala bora na njia za kupiga vita umaskini uliokithiri. 
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Maendeleo nchini Tanzania UNDP Philippe Poinsot, amesema Tanzania ni nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa ambayo inawajibika vizuri kwenye umoja huo. 
Mbali na hayo Mkurugenzi huyo wa UNDP amesema kuwa Umoja wa Mataifa unachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza umasikini uliokithiri nchini Tanzania ambapo takriban dola za Marekani lakini nne milioni hutolewa katika kipindi cha miaka minne. 
Wiki ya Umoja wa Mataifa imeanza kuadhishwa Oktoba 17 na itafikia kilele Oktoba 24 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment