Saturday 13 October 2012

UPDATE KIFO CHA KAMANDA:MAJIBU YA MASWALI MENGI YASIYOJIBIKA KUHUSU KIFO HICHO

-Kamanda Barlow alikuwa na mwanamke ndani ya gari wakiwa peke yao wawili
-Mwanamke si dada yake wala ndugu yake
-Lilikuwa gari la binafsi na Kamanda aliendesha mwenyewe.
-Walitoka kwenye kikao La Kairo Hotel na siyo Florida Hotel kama IGP alivyosema katika taarifa yake
-Walipofika Kitangiri, Kamanda aliamua kumpeleka yule mama ndani kwnye uchochoro badala ya kumwacha barabarani
-Si mara ya kwanza Kamanda kumpeleka mama yule eneo lile
-Walipoingia uchochoroni, waliwakuta the so called "polisi jamii" wakiwa kwenye doria
-Kamanda alishusha kioo na kuwauliza ni kina nani, na wao walimjibu kuwa ni polisi jamii.
-Aliwahoji kwa nini wamevaa mikanda ya polisi wakati waliishazuiwa
-Ulitokea ubishi kidogo
-Kamanda akainua redio call kuwaita vijana wake waje kuwakamata
-Polisi jamii wakamdaka kumnyanganya redio call hiyo na kumpiga risasi ya shingoni
-Wakamvuta na kumlaza chini ya uvungu wa gari
-Yule mama ndiye aliyemwita mlinzi wa RPC na kumwambia aje kumchukua "mzee" maana ameuawawa
-Mama anaisaidia polisi hata sasa.



chanzo:jf member

No comments:

Post a Comment