Thursday 25 October 2012

Profesa Anna Tibaijuka ziarani sweden


 Mhe. Anna Tibaijukam Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitia saini kitabu cha wageni Ubalozini, akiwa na balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe  muhammed mwinyi mzale.
Profesa Anna Tibaijuka, Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitia saini kitabu cha wageni Ubalozini, yupo nchini Sweden kwa ziara ya kikazi ya siku tano akiambatana na Maafisa waandamizi wa Wizara yake ambapo pamoja mambo mengine atakutana na kufanya mazungumzo na viongozi kadhaa ikiwa ni pamoja na Mhe. Gunila Carlsson-Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa, Mkurugenzi Mkuu wa Stockholm Environment Insititute. Mkurugenzi Mkuu wa SIDA, Secretary-General wa IDEA (International Institute for Democracy and Electoral Assistance, na Mkurugenzi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Land Survey, ambapo atawasilisha mada "Recent trends in land issues in Tanzania and discussion about interest for cooperation with Sweden.
 Mhe. Anna Tibaijukam Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi akiwa anazungumza akiwa na balozi
wa Tanzania nchini Sweden, Mhe  muhammed mwinyi Mzale pamoja na maafisa wa ubalozini hapo.

No comments:

Post a Comment